Tafsiri ya Sura An-Najm kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑﭒﭓ
ﭔ
An-Najm
Naapa kwa nyota inapo tua,
Verse 2
ﭕﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.
Verse 3
ﭛﭜﭝﭞ
ﭟ
Wala hatamki kwa matamanio.
Verse 4
ﭠﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;
Verse 5
ﭦﭧﭨ
ﭩ
Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,
Verse 6
ﭪﭫﭬ
ﭭ
Mwenye kutua, akatulia,
Verse 7
ﭮﭯﭰ
ﭱ
Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.
Verse 8
ﭲﭳﭴ
ﭵ
Kisha akakaribia na akateremka.
Verse 9
ﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.
Verse 10
ﭼﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.
Verse 11
ﮂﮃﮄﮅﮆ
ﮇ
Moyo haukusema uwongo uliyo yaona.
Verse 12
ﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona?
Verse 13
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Na akamwona mara nyingine,
Verse 14
ﮒﮓﮔ
ﮕ
Penye Mkunazi wa mwisho.
Verse 15
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa.
Verse 16
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.
Verse 17
ﮠﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.
Verse 18
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.
Verse 19
ﮭﮮﮯ
ﮰ
Je! Mmemuona Lata na Uzza?
Verse 20
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Na Manaat, mwingine wa tatu?
Verse 21
ﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?
Verse 22
ﯛﯜﯝﯞ
ﯟ
Huo ni mgawanyo wa dhulma!
Verse 23
Hayo hayakuwa ila ni majina mliyo wapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.
Verse 24
ﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Ati mtu anakipata kila anacho kitamani?
Verse 25
ﰁﰂﰃ
ﰄ
Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.
Verse 26
Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipo kuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.
Verse 27
Hakika wasio amini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.
Verse 28
Nao hawana ujuzi wowote kwa hayo isipo kuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.
Verse 29
Basi mwachilie mbali anaye upa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.
Verse 30
Huo ndio mwisho wao wa ujuzi. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuongoka.
Verse 31
Ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, ili awalipe walio tenda ubaya kwa waliyo yatenda, na walio tenda mema awalipe mema.
Verse 32
Ambao wanajiepusha na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipo kuwa makosa khafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipo kuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipo kuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijisifu usafi. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga na maovu.
Verse 33
ﯢﯣﯤ
ﯥ
Je! Umemwona yule aliye geuka?
Verse 34
ﯦﯧﯨ
ﯩ
Na akatoa kidogo, kisha akajizuia?
Verse 35
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Je! Anayo huyo ilimu ya ghaibu, basi ndio anaona?
Verse 36
Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?
Verse 37
ﯸﯹﯺ
ﯻ
Na vya Ibrahimu aliye timiza ahadi?
Verse 38
ﯼﯽﯾﯿﰀ
ﰁ
Ya kwamba hakika nafsi iliyo beba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?
Verse 39
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
ﰈ
Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyo yafanya mwenyewe?
Verse 40
ﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?
Verse 41
ﰎﰏﰐﰑ
ﰒ
Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa ukamilifu.
Verse 42
ﰓﰔﰕﰖ
ﰗ
Na kwamba kwao Mola wako Mlezi ndio mwisho.
Verse 43
ﰘﰙﰚﰛ
ﰜ
Na kwamba Yeye ndiye anaye leta kicheko na kilio.
Verse 44
ﰝﰞﰟﰠ
ﰡ
Na kwamba Yeye ndiye anaye fisha na kuhuisha.
Verse 45
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike
Verse 46
ﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.
Verse 47
ﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.
Verse 48
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.
Verse 49
ﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.
Verse 50
ﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza,
Verse 51
ﭰﭱﭲ
ﭳ
Na Thamudi hakuwabakisha,
Verse 52
Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhaalimu zaidi, na waovu zaidi;
Verse 53
ﭿﮀ
ﮁ
Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua.
Verse 54
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Vikaifunika vilivyo funika.
Verse 55
ﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka?
Verse 56
ﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Hili ni Onyo katika maonyo yale yale ya zamani.
Verse 57
ﮑﮒ
ﮓ
Kiyama kimekaribia!
Verse 58
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Hapana wa kukifichua isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
Verse 59
ﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Je! Mnayastaajabia maneno haya?
Verse 60
ﮠﮡﮢ
ﮣ
Na mnacheka, wala hamlii?
Verse 61
ﮤﮥ
ﮦ
Nanyi mmeghafilika?
Verse 62
ﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.
تقدم القراءة