Tafsiri ya Sura Yasin kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭬ
ﭭ
Yasin
Ya-Sin (Y. S.).
Verse 2
ﭮﭯ
ﭰ
Kwa Haki ya Qur'ani yenye hikima!
Verse 3
ﭱﭲﭳ
ﭴ
Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,
Verse 4
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Juu ya Njia Iliyo Nyooka.
Verse 5
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
Verse 6
Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi wao wamekuwa wenye kughafilika.
Verse 7
Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.
Verse 8
Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.
Verse 9
Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.
Verse 10
Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.
Verse 11
Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.
Verse 12
Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha.
Verse 13
Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.
Verse 14
Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.
Verse 15
Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.
Verse 16
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
ﭼ
Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu.
Verse 17
ﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.
Verse 18
Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu.
Verse 19
Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka.
Verse 20
Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa.
Verse 21
Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.
Verse 22
NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?
Verse 23
Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.
Verse 24
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.
Verse 25
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!
Verse 26
Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua
Verse 27
Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa.
Verse 28
Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.
Verse 29
Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!
Verse 30
Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
Verse 31
Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.
Verse 32
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.
Verse 33
Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanazila!
Verse 34
Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem ndani yake,
Verse 35
Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?
Verse 36
Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.
Verse 37
Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.
Verse 38
Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.
Verse 39
Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.
Verse 40
Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.
Verse 41
Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.
Verse 42
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda.
Verse 43
Na tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi,
Verse 44
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Isipo kuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.
Verse 45
Na wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa...
Verse 46
Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni wenye kuipuuza.
Verse 47
Na wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru huwaambia walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli walisha mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri.
Verse 48
Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?
Verse 49
Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.
Verse 50
Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.
Verse 51
Na litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao Mlezi.
Verse 52
Watasema: Ole wetu! Nani aliye tufufua kwenye malazi yetu? Haya ndiyo aliyo yaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.
Verse 53
Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhuruishwa mbele yetu.
Verse 54
Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyo kuwa mkiyatenda.
Verse 55
Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi.
Verse 56
Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fakhari.
Verse 57
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakacho kitaka.
Verse 58
ﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
"Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu.
Verse 59
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na enyi wakosefu! Jitengeni leo!
Verse 60
Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet'ani? Hakika yeye ni adui dhaahiri kwenu.
Verse 61
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
Verse 62
Na bila ya shaka yeye amekwisha lipoteza kundi kubwa miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkifikiri?
Verse 63
ﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Hii basi ndiyo Jahannamu mliyo kuwa mkiahidiwa.
Verse 64
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Ingieni leo kwa vile mlivyo kuwa mkikufuru.
Verse 65
Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyo kuwa wakiyachuma.
Verse 66
Na tungeli penda tungeli yafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wange ionaje?
Verse 67
Na tungeli taka tunge wageuza sura hapo hapo walipo, basi wasinge weza kwenda wala kurudi.
Verse 68
Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii?
Verse 69
Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur'ani inayo bainisha.
Verse 70
Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri.
Verse 71
Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyo fanya mikono yetu wanyama wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki.
Verse 72
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanao wapanda, na baadhi yao wanawala.
Verse 73
Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?
Verse 74
Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati wapate kusaidiwa!
Verse 75
Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio watakuwa askari wao watakao hudhurishwa.
Verse 76
Basi maneno yao yasikuhuzunishe. Hakika Sisi tunayajua wanayo yaweka siri na wanayo yatangaza.
Verse 77
Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri!
Verse 78
Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika?
Verse 79
Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba.
Verse 80
Aliye kujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo mnawasha.
Verse 81
Kwani aliye ziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi.
Verse 82
Hakika amri yake anapo taka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa.
Verse 83
Basi Ametakasika yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake Yeye mtarejeshwa.
تقدم القراءة