سورة العنكبوت

Ali Muhsin Al - Swahili translation

Tafsiri ya Sura Al-Ankabut kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation

Ali Muhsin Al - Swahili translation

Verse 1

Al-Ankabut


Alif Lam Mim (A. L. M.)

Na hapana shaka Mwenyezi Mungu atawatambulisha walio amini, na atawatambulisha wanaafiki.

Nasi tukamwokoa yeye na wenziwe wa katika safina, na tukaifanya kuwa ni Ishara kwa walimwengu wote.

Lakini walimkanusha basi ukawatwaa mtikiso wa ardhi, wakapambazukiwa ndani ya nyumba zao nao wamefudikia.

Na wanakuhimiza waletewe adhabu kwa haraka. Na lau kuwa hapana wakati maalumu ulio wekwa, basi adhabu ingeli wajia, na ingeli watokea kwa ghafla, na hali wao hawana khabari.

Wanakuhimiza waletewe adhabu kwa haraka, na hali Jahannamu kwa hakika imewazunguka makafiri!
تقدم القراءة