Tafsiri ya Sura At-Tur kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮞ
ﮟ
At-Tur
Naapa kwa mlima wa T'ur,
Verse 2
ﮠﮡ
ﮢ
Na Kitabu kilicho andikwa
Verse 3
ﮣﮤﮥ
ﮦ
Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
Verse 4
ﮧﮨ
ﮩ
Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
Verse 5
ﮪﮫ
ﮬ
Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
Verse 6
ﮭﮮ
ﮯ
Na kwa bahari iliyo jazwa,
Verse 7
ﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
Verse 8
ﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Hapana wa kuizuia.
Verse 9
ﯛﯜﯝﯞ
ﯟ
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
Verse 10
ﯠﯡﯢ
ﯣ
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
Verse 11
ﯤﯥﯦ
ﯧ
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
Verse 12
ﯨﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
Verse 13
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
Verse 14
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
ﯻ
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
Verse 15
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
Verse 16
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
Verse 17
ﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
Verse 18
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
Verse 19
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
Verse 20
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
Verse 21
Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
Verse 22
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
Verse 23
Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
Verse 24
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
Verse 25
ﯓﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Wataelekeana wakiulizana.
Verse 26
Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
Verse 27
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
Verse 28
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
Verse 29
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
Verse 30
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
Verse 31
ﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
Verse 32
Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
Verse 33
Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
Verse 34
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
Verse 35
Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
Verse 36
Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
Verse 37
Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
Verse 38
Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
Verse 39
ﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
Verse 40
Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
Verse 41
ﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
Verse 42
Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
Verse 43
Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
Verse 44
Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
Verse 45
Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
Verse 46
Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
Verse 47
Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
Verse 48
Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
Verse 49
ﰋﰌﰍﰎﰏ
ﰐ
Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.
تقدم القراءة