Tafsiri ya Sura Al-Kamar kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮬﮭﮮﮯ
ﮰ
Al-Kamar
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
Verse 2
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
Verse 3
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
Verse 4
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
Verse 5
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
Verse 6
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
Verse 7
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
Verse 8
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
Verse 9
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
Verse 10
ﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!
Verse 11
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
Verse 12
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
Verse 13
ﮅﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
Verse 14
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
Verse 15
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
Verse 16
ﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
Verse 17
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?
Verse 18
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
Verse 19
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
Verse 20
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.
Verse 21
ﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
Verse 22
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?
Verse 23
ﯬﯭﯮ
ﯯ
Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
Verse 24
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!
Verse 25
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!
Verse 26
ﰅﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
Verse 27
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.
Verse 28
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.
Verse 29
ﭛﭜﭝﭞ
ﭟ
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
Verse 30
ﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
Verse 31
Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
Verse 32
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?
Verse 33
ﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
Verse 34
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
Verse 35
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
Verse 36
ﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
Verse 37
Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!
Verse 38
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
Verse 39
ﮥﮦﮧ
ﮨ
Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!
Verse 40
Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?
Verse 41
ﮱﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.
Verse 42
Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.
Verse 43
Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?
Verse 44
ﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
Verse 45
ﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
Verse 46
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
Verse 47
ﯽﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.
Verse 48
Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!
Verse 49
ﰍﰎﰏﰐﰑ
ﰒ
Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
Verse 50
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
Verse 51
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
Verse 52
ﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
Verse 53
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
Verse 54
ﭪﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
Verse 55
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
تقدم القراءة