Tafsiri ya Sura Ad-Dukhan kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑ
ﭒ
Ad-Dukhan
H'a Mim
Verse 2
ﭓﭔ
ﭕ
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
Verse 3
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
Verse 4
ﭠﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
Verse 5
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
Verse 6
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
Verse 7
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
Verse 8
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
Verse 9
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Lakini wao wanacheza katika shaka.
Verse 10
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
Verse 11
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
Verse 12
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
Verse 13
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
Verse 14
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
Verse 15
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
Verse 16
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
Verse 17
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
Verse 18
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
Verse 19
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
Verse 20
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
Verse 21
ﭣﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
Verse 22
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
Verse 23
ﭰﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
Verse 24
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
Verse 25
ﭾﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
Verse 26
ﮄﮅﮆ
ﮇ
Na mimea na vyeo vitukufu!
Verse 27
ﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
Verse 28
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
Verse 29
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
Verse 30
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
Verse 31
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
Verse 32
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
Verse 33
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
Verse 34
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Hakika hawa wanasema:
Verse 35
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
Verse 36
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
Verse 37
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
Verse 38
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
Verse 39
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
Verse 40
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
Verse 41
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
Verse 42
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
Verse 43
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Hakika Mti wa Zaqqum,
Verse 44
ﭯﭰ
ﭱ
Ni chakula cha mwenye dhambi.
Verse 45
ﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
Verse 46
ﭷﭸ
ﭹ
Kama kutokota kwa maji ya moto.
Verse 47
ﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
Verse 48
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
Verse 49
ﮈﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
Verse 50
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
Verse 51
ﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
Verse 52
ﮛﮜﮝ
ﮞ
Katika mabustani na chemchem,
Verse 53
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
Verse 54
ﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
Verse 55
ﮪﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
Verse 56
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
Verse 57
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
Verse 58
ﯦﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
Verse 59
ﯬﯭﯮ
ﯯ
Ngoja tu, na wao wangoje pia.
تقدم القراءة