Tafsiri ya Sura As-Shu'ara kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑ
ﭒ
As-Shu'ara
T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)
Verse 2
ﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
Verse 3
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
Verse 4
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
Verse 5
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
Verse 6
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
Verse 7
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
Verse 8
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
Verse 9
ﮖﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
Verse 10
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
Verse 11
ﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Watu wa Firauni. Hawaogopi?
Verse 12
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰ
ﮱ
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
Verse 13
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
Verse 14
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
Verse 15
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
Verse 16
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 17
ﯵﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
Verse 18
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?
Verse 19
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?
Verse 20
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
Verse 21
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
Verse 22
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
Verse 23
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
Verse 24
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
Verse 25
ﭾﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
Verse 26
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
Verse 27
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
Verse 28
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
Verse 29
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
Verse 30
ﮦﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
Verse 31
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.
Verse 32
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.
Verse 33
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
Verse 34
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
Verse 35
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
Verse 36
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
Verse 37
ﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
Verse 38
ﰁﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
Verse 39
ﰇﰈﰉﰊﰋ
ﰌ
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
Verse 40
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
Verse 41
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?
Verse 42
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
Verse 43
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
Verse 44
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
Verse 45
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
Verse 46
ﮈﮉﮊ
ﮋ
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.
Verse 47
ﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 48
ﮑﮒﮓ
ﮔ
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
Verse 49
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
Verse 50
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
Verse 51
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.
Verse 52
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
Verse 53
ﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
Verse 54
ﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
Verse 55
ﯸﯹﯺ
ﯻ
Nao wanatuudhi.
Verse 56
ﯼﯽﯾ
ﯿ
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
Verse 57
ﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
Verse 58
ﰅﰆﰇ
ﰈ
Na makhazina, na vyeo vya hishima,
Verse 59
ﰉﰊﰋﰌﰍ
ﰎ
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
Verse 60
ﰏﰐ
ﰑ
Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.
Verse 61
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!
Verse 62
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
Verse 63
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
Verse 64
ﭱﭲﭳ
ﭴ
Na tukawajongeza hapo wale wengine.
Verse 65
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
Verse 66
ﭻﭼﭽ
ﭾ
Kisha tukawazamisha hao wengine.
Verse 67
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.
Verse 68
ﮉﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
Verse 69
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na wasomee khabari za Ibrahim.
Verse 70
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
Verse 71
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
Verse 72
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?
Verse 73
ﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?
Verse 74
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
Verse 75
ﯕﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-
Verse 76
ﯛﯜﯝ
ﯞ
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
Verse 77
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 78
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,
Verse 79
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
Verse 80
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.
Verse 81
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
Verse 82
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
Verse 83
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
ﰉ
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.
Verse 84
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
Verse 85
ﭘﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
Verse 86
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
Verse 87
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.
Verse 88
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
Verse 89
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
ﭷ
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
Verse 90
ﭸﭹﭺ
ﭻ
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.
Verse 91
ﭼﭽﭾ
ﭿ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
Verse 92
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
Verse 93
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
Verse 94
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
Verse 95
ﮔﮕﮖ
ﮗ
Na majeshi ya Ibilisi yote.
Verse 96
ﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
Verse 97
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
Verse 98
ﮤﮥﮦﮧ
ﮨ
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 99
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.
Verse 100
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Basi hatuna waombezi.
Verse 101
ﯔﯕﯖ
ﯗ
Wala rafiki wa dhati.
Verse 102
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
Verse 103
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
Verse 104
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
Verse 105
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
Verse 106
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
Verse 107
ﯽﯾﯿﰀ
ﰁ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Verse 108
ﰂﰃﰄ
ﰅ
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
Verse 109
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 110
ﰓﰔﰕ
ﰖ
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
Verse 111
ﰗﰘﰙﰚﰛﰜ
ﰝ
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
Verse 112
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?
Verse 113
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!
Verse 114
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
Verse 115
ﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
Verse 116
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
Verse 117
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
Verse 118
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.
Verse 119
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.
Verse 120
ﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.
Verse 121
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.
Verse 122
ﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
Verse 123
ﮡﮢﮣ
ﮤ
Kina A'd waliwakanusha Mitume.
Verse 124
Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?
Verse 125
ﮭﮮﮯﮰ
ﮱ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Verse 126
ﯓﯔﯕ
ﯖ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
Verse 127
Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 128
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
Verse 129
ﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!
Verse 130
ﯯﯰﯱﯲ
ﯳ
Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.
Verse 131
ﯴﯵﯶ
ﯷ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
Verse 132
ﯸﯹﯺﯻﯼ
ﯽ
Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.
Verse 133
ﯾﯿﰀ
ﰁ
Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.
Verse 134
ﰂﰃ
ﰄ
Na mabustani na chemchem.
Verse 135
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
ﰋ
Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.
Verse 136
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
Verse 137
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
Verse 138
ﭗﭘﭙ
ﭚ
Wala sisi hatutaadhibiwa.
Verse 139
Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Verse 140
ﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
Verse 141
ﭮﭯﭰ
ﭱ
Kina Thamud waliwakanusha Mitume.
Verse 142
Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?
Verse 143
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Verse 144
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
Verse 145
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 146
ﮐﮑﮒﮓﮔ
ﮕ
Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
Verse 147
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Katika mabustani, na chemchem?
Verse 148
ﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.
Verse 149
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
Verse 150
ﮥﮦﮧ
ﮨ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
Verse 151
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,
Verse 152
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.
Verse 153
ﯖﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.
Verse 154
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
Verse 155
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
Verse 156
Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.
Verse 157
ﯺﯻﯼ
ﯽ
Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.
Verse 158
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Verse 159
ﰋﰌﰍﰎﰏ
ﰐ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
Verse 160
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.
Verse 161
Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?
Verse 162
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
Verse 163
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.
Verse 164
Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 165
ﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
Verse 166
Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!
Verse 167
Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!
Verse 168
ﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.
Verse 169
ﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
Verse 170
ﮛﮜﮝ
ﮞ
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,
Verse 171
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.
Verse 172
ﮤﮥﮦ
ﮧ
Kisha tukawaangamiza wale wengine.
Verse 173
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.
Verse 174
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Verse 175
ﯛﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
Verse 176
ﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
Verse 177
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?
Verse 178
ﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Verse 179
ﯲﯳﯴ
ﯵ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
Verse 180
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 181
Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.
Verse 182
ﰋﰌﰍ
ﰎ
Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;
Verse 183
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.
Verse 184
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.
Verse 185
ﭗﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.
Verse 186
Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
Verse 187
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
Verse 188
ﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.
Verse 189
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.
Verse 190
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Verse 191
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
Verse 192
ﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 193
ﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Ameuteremsha Roho muaminifu,
Verse 194
ﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,
Verse 195
ﮣﮤﮥ
ﮦ
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
Verse 196
ﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
Verse 197
Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?
Verse 198
ﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,
Verse 199
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.
Verse 200
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.
Verse 201
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
Verse 202
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.
Verse 203
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Na watasema: Je, tutapewa muhula?
Verse 204
ﯽﯾ
ﯿ
Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?
Verse 205
ﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,
Verse 206
ﰅﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,
Verse 207
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?
Verse 208
Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -
Verse 209
ﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
Verse 210
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,
Verse 211
ﭪﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
Verse 212
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Hakika hao wametengwa na kusikia.
Verse 213
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.
Verse 214
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
Verse 215
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.
Verse 216
Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.
Verse 217
ﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
Verse 218
ﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Ambaye anakuona unapo simama,
Verse 219
ﮜﮝﮞ
ﮟ
Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.
Verse 220
ﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
Verse 221
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?
Verse 222
ﮬﮭﮮﮯﮰ
ﮱ
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
Verse 223
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.
Verse 224
ﯘﯙﯚ
ﯛ
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
Verse 225
Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
Verse 226
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?
Verse 227
Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.
تقدم القراءة