Tafsiri ya Sura Al-Waki'ah kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮃﮄﮅ
ﮆ
Al-Waki'ah
Litakapo tukia hilo Tukio
Verse 2
ﮇﮈﮉ
ﮊ
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
Verse 3
ﮋﮌ
ﮍ
Literemshalo linyanyualo,
Verse 4
ﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
Verse 5
ﮓﮔﮕ
ﮖ
Na milima itapo sagwasagwa,
Verse 6
ﮗﮘﮙ
ﮚ
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
Verse 7
ﮛﮜﮝ
ﮞ
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
Verse 8
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
Verse 9
ﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
Verse 10
ﮫﮬ
ﮭ
Na wa mbele watakuwa mbele.
Verse 11
ﮮﮯ
ﮰ
Hao ndio watakao karibishwa
Verse 12
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Katika Bustani zenye neema.
Verse 13
ﯖﯗﯘ
ﯙ
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
Verse 14
ﯚﯛﯜ
ﯝ
Na wachache katika wa mwisho.
Verse 15
ﯞﯟﯠ
ﯡ
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
Verse 16
ﯢﯣﯤ
ﯥ
Wakiviegemea wakielekeana.
Verse 17
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
Verse 18
ﭖﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
Verse 19
ﭜﭝﭞﭟﭠ
ﭡ
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
Verse 20
ﭢﭣﭤ
ﭥ
Na matunda wayapendayo,
Verse 21
ﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
Verse 22
ﭫﭬ
ﭭ
Na Mahurulaini,
Verse 23
ﭮﭯﭰ
ﭱ
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
Verse 24
ﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
Verse 25
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
ﭽ
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
Verse 26
ﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
Verse 27
ﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
Verse 28
ﮉﮊﮋ
ﮌ
Katika mikunazi isiyo na miba,
Verse 29
ﮍﮎ
ﮏ
Na migomba iliyo pangiliwa,
Verse 30
ﮐﮑ
ﮒ
Na kivuli kilicho tanda,
Verse 31
ﮓﮔ
ﮕ
Na maji yanayo miminika,
Verse 32
ﮖﮗ
ﮘ
Na matunda mengi,
Verse 33
ﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Hayatindikii wala hayakatazwi,
Verse 34
ﮞﮟ
ﮠ
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
Verse 35
ﮡﮢﮣ
ﮤ
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
Verse 36
ﮥﮦ
ﮧ
Na tutawafanya vijana,
Verse 37
ﮨﮩ
ﮪ
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
Verse 38
ﮫﮬ
ﮭ
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
Verse 39
ﮮﮯﮰ
ﮱ
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
Verse 40
ﯓﯔﯕ
ﯖ
Na fungu kubwa katika wa mwisho.
Verse 41
ﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
Verse 42
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
Verse 43
ﯡﯢﯣ
ﯤ
Na kivuli cha moshi mweusi,
Verse 44
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
Verse 45
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
Verse 46
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
Verse 47
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
Verse 48
ﰀﰁ
ﰂ
Au baba zetu wa zamani?
Verse 49
ﰃﰄﰅﰆ
ﰇ
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
Verse 50
ﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
Verse 51
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
Verse 52
ﭗﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
Verse 53
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
Verse 54
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
Verse 55
ﭦﭧﭨ
ﭩ
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
Verse 56
ﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
Verse 57
ﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
Verse 58
ﭴﭵﭶ
ﭷ
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
Verse 59
ﭸﭹﭺﭻﭼ
ﭽ
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
Verse 60
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
Verse 61
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
Verse 62
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
Verse 63
ﮗﮘﮙ
ﮚ
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
Verse 64
ﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
Verse 65
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
Verse 66
ﮨﮩ
ﮪ
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
Verse 67
ﮫﮬﮭ
ﮮ
Bali sisi tumenyimwa.
Verse 68
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
Verse 69
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
Verse 70
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
Verse 71
ﯤﯥﯦﯧ
ﯨ
Je! Mnauona moto mnao uwasha?
Verse 72
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
Verse 73
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
Verse 74
ﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
Verse 75
ﯻﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
Verse 76
ﰁﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
Verse 77
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
Verse 78
ﭕﭖﭗ
ﭘ
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
Verse 79
ﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Hapana akigusaye ila walio takaswa.
Verse 80
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Verse 81
ﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
Verse 82
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
Verse 83
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
Verse 84
ﭲﭳﭴ
ﭵ
Na nyinyi wakati huo mnatazama!
Verse 85
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
Verse 86
ﭾﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
Verse 87
ﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
Verse 88
ﮉﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
Verse 89
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
Verse 90
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
Verse 91
ﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
Verse 92
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
Verse 93
ﮨﮩﮪ
ﮫ
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
Verse 94
ﮬﮭ
ﮮ
Na kutiwa Motoni.
Verse 95
ﮯﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
Verse 96
ﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.
تقدم القراءة