Tafsiri ya Sura Al-Muddasir kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮪﮫ
ﮬ
Al-Muddasir
Ewe uliye jigubika!
Verse 2
ﮭﮮ
ﮯ
Simama uonye!
Verse 3
ﮰﮱ
ﯓ
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
Verse 4
ﯔﯕ
ﯖ
Na nguo zako, zisafishe.
Verse 5
ﯗﯘ
ﯙ
Na yaliyo machafu yahame!
Verse 6
ﯚﯛﯜ
ﯝ
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
Verse 7
ﯞﯟ
ﯠ
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
Verse 8
ﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Basi litapo pulizwa barugumu,
Verse 9
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
Verse 10
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
Verse 11
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Niache peke yangu na niliye muumba;
Verse 12
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
Verse 13
ﯺﯻ
ﯼ
Na wana wanao onekana,
Verse 14
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
Verse 15
ﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Kisha anatumai nimzidishie!
Verse 16
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
ﰌ
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
Verse 17
ﰍﰎ
ﰏ
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
Verse 18
ﰐﰑﰒ
ﰓ
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
Verse 19
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
Verse 20
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
Verse 21
ﭚﭛ
ﭜ
Kisha akatazama,
Verse 22
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
Verse 23
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
Verse 24
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
Verse 25
ﭬﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
Verse 26
ﭲﭳ
ﭴ
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
Verse 27
ﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
Verse 28
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Haubakishi wala hausazi.
Verse 29
ﭿﮀ
ﮁ
Unababua ngozi iwe nyeusi.
Verse 30
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Juu yake wapo kumi na tisa.
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
Verse 32
ﯥﯦ
ﯧ
Hasha! Naapa kwa mwezi!
Verse 33
ﯨﯩﯪ
ﯫ
Na kwa usiku unapo kucha!
Verse 34
ﯬﯭﯮ
ﯯ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
Verse 35
ﯰﯱﯲ
ﯳ
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
Verse 36
ﯴﯵ
ﯶ
Ni onyo kwa binaadamu,
Verse 37
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
Verse 38
ﯿﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
Verse 39
ﰅﰆﰇ
ﰈ
Isipo kuwa watu wa kuliani.
Verse 40
ﰉﰊﰋ
ﰌ
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
Verse 41
ﰍﰎ
ﰏ
Khabari za wakosefu:
Verse 42
ﰐﰑﰒﰓ
ﰔ
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
Verse 43
ﰕﰖﰗﰘﰙ
ﰚ
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.
Verse 44
ﰛﰜﰝﰞ
ﰟ
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
Verse 45
ﰠﰡﰢﰣ
ﰤ
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
Verse 46
ﰥﰦﰧﰨ
ﰩ
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
Verse 47
ﰪﰫﰬ
ﰭ
Mpaka yakini ilipo tufikia.
Verse 48
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
Verse 49
ﭖﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
Verse 50
ﭜﭝﭞ
ﭟ
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
Verse 51
ﭠﭡﭢ
ﭣ
Wanao mkimbia simba!
Verse 52
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
Verse 53
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
Verse 54
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
Verse 55
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Basi anaye taka atakumbuka.
Verse 56
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
تقدم القراءة