ترجمة معاني سورة الماعون باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation .

Al-Ma'un


Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo?

Huyo ndiye anaye msukuma yatima,

Wala hahimizi kumlisha masikini.

Basi, ole wao wanao sali,

Ambao wanapuuza Sala zao;

Ambao wanajionyesha,

Nao huku wanazuia msaada.