Tafsiri ya Sura Ar-Rahman kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭷ
ﭸ
Ar-Rahman
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
Verse 2
ﭹﭺ
ﭻ
Amefundisha Qur'ani.
Verse 3
ﭼﭽ
ﭾ
Amemuumba mwanaadamu,
Verse 4
ﭿﮀ
ﮁ
Akamfundisha kubaini.
Verse 5
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
Verse 6
ﮆﮇﮈ
ﮉ
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
Verse 7
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
Verse 8
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Ili msidhulumu katika mizani.
Verse 9
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
Verse 10
ﮛﮜﮝ
ﮞ
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
Verse 11
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
Verse 12
ﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
Verse 13
ﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 14
ﮯﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
Verse 15
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
Verse 16
ﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 17
ﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
Verse 18
ﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 19
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
Verse 20
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
Verse 21
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 22
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
Verse 23
ﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 24
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
Verse 25
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 26
ﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Kila kilioko juu yake kitatoweka.
Verse 27
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
ﮀ
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
Verse 28
ﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 29
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
Verse 30
ﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 31
ﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
Verse 32
ﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 33
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
Verse 34
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 35
Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
Verse 36
ﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 37
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
Verse 38
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 39
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
Verse 40
ﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 41
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
ﰇ
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
Verse 42
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 43
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
Verse 44
ﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
Verse 45
ﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 46
ﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
Verse 47
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 48
ﭳﭴ
ﭵ
Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
Verse 49
ﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 50
ﭻﭼﭽ
ﭾ
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
Verse 51
ﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 52
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
Verse 53
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 54
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
Verse 55
ﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 56
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
Verse 57
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 58
ﮮﮯﮰ
ﮱ
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
Verse 59
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
Verse 60
ﯘﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
Verse 61
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 62
ﯣﯤﯥ
ﯦ
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
Verse 63
ﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 64
ﯬ
ﯭ
Za kijani kibivu.
Verse 65
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 66
ﯳﯴﯵ
ﯶ
Na chemchem mbili zinazo furika.
Verse 67
ﯷﯸﯹﯺ
ﯻ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 68
ﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
Verse 69
ﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 70
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Humo wamo wanawake wema wazuri.
Verse 71
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 72
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
Verse 73
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 74
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
Verse 75
ﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 76
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
Verse 77
ﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Verse 78
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
تقدم القراءة