Tafsiri ya Sura Al-Infitar kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Al-Infitar
Mbingu itapo chanika,
Verse 2
ﭕﭖﭗ
ﭘ
Na nyota zitapo tawanyika,
Verse 3
ﭙﭚﭛ
ﭜ
Na bahari zitakapo pasuliwa,
Verse 4
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Na makaburi yatapo fukuliwa,
Verse 5
ﭡﭢﭣﭤﭥ
ﭦ
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
Verse 6
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
Verse 7
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
Verse 8
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
Verse 9
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
Verse 10
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
Verse 11
ﮃﮄ
ﮅ
Waandishi wenye hishima,
Verse 12
ﮆﮇﮈ
ﮉ
Wanayajua mnayo yatenda.
Verse 13
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
Verse 14
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
Verse 15
ﮔﮕﮖ
ﮗ
Wataingia humo Siku ya Malipo.
Verse 16
ﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Na hawatoacha kuwamo humo.
Verse 17
ﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
Verse 18
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
Verse 19
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
تقدم القراءة