Tafsiri ya Sura Al-Ma'arij kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Al-Ma'arij
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
Verse 2
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
Verse 3
ﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
Verse 4
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
Verse 5
ﯪﯫﯬ
ﯭ
Basi subiri kwa subira njema.
Verse 6
ﯮﯯﯰ
ﯱ
Hakika wao wanaiona iko mbali,
Verse 7
ﯲﯳ
ﯴ
Na Sisi tunaiona iko karibu.
Verse 8
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
Verse 9
ﯺﯻﯼ
ﯽ
Na milima itakuwa kama sufi.
Verse 10
ﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
Verse 11
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
Verse 12
ﭜﭝ
ﭞ
Na mkewe, na nduguye,
Verse 13
ﭟﭠﭡ
ﭢ
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
Verse 14
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
Verse 15
ﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
Verse 16
ﭯﭰ
ﭱ
Unao babua ngozi ya kichwa!
Verse 17
ﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
Verse 18
ﭷﭸ
ﭹ
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
Verse 19
ﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Hakika mtu ameumbwa na papara.
Verse 20
ﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Inapo mgusa shari hupapatika.
Verse 21
ﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na inapo mgusa kheri huizuilia.
Verse 22
ﮊﮋ
ﮌ
Isipo kuwa wanao sali,
Verse 23
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Ambao wanadumisha Sala zao,
Verse 24
ﮓﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
Verse 25
ﮙﮚ
ﮛ
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
Verse 26
ﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
Verse 27
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
Verse 28
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
Verse 29
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Na ambao wanahifadhi tupu zao.
Verse 30
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
Verse 31
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
Verse 32
ﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
Verse 33
ﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
Verse 34
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
Verse 35
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
Verse 36
ﯽﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
Verse 37
ﰃﰄﰅﰆﰇ
ﰈ
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
Verse 38
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
Verse 39
ﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
ﰘ
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
Verse 40
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
Verse 41
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
Verse 42
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
Verse 43
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
Verse 44
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.
تقدم القراءة