Tafsiri ya Sura Taha kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭵ
ﭶ
Taha
T'AHA!
Verse 2
ﭷﭸﭹﭺﭻ
ﭼ
Hatukukuteremshia Qur'ani ili upate mashaka.
Verse 3
ﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Bali ni mawaidha kwa wenye kunyenyekea.
Verse 4
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
Materemsho yatokayo kwa aliye umba ardhi na mbingu zilizo juu.
Verse 5
ﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Arrahmani, Mwingi wa Rehema, aliye tawala juu ya Kiti cha Enzi.
Verse 6
Ni vyake vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, na viliomo baina yao, na viliomo chini ya ardhi.
Verse 7
Na ukinyanyua sauti kwa kusema... basi hakika Yeye anajua siri na duni kuliko siri.
Verse 8
Mwenyezi Mungu! Hapana mungu isipo kuwa Yeye. Yeye ana majina mazuri kabisa.
Verse 9
ﮭﮮﮯﮰ
ﮱ
Na je! Imekufikia hadithi ya Musa?
Verse 10
Alipo uona moto, akawaambia watu wake: Ngojeni! Mimi nimeuona moto, huenda nikakuleteeni kijinga kutoka huo moto, au nikapata uongofu kwenye moto.
Verse 11
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Basi alipo ufikia akaitwa: Ewe Musa!
Verse 12
Hakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani upo katika bonde takatifu la T'uwa.
Verse 13
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Nami nimekuteua wewe; basi sikiliza unayo funuliwa.
Verse 14
Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu. Hapana mungu ila Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na ushike Sala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi.
Verse 15
Hakika Saa itakuja bila ya shaka. Nimekaribia kuificha, ili kila nafsi ilipwe kwa iliyo yafanya.
Verse 16
Kwa hivyo asikukengeushe nayo yule ambaye haiamini na akafuata pumbao lake ukaja kuhiliki.
Verse 17
ﭹﭺﭻﭼ
ﭽ
Na nini hicho kilichomo mkononi mwako wa kulia, ewe Musa?
Verse 18
Akasema: Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine.
Verse 19
ﮌﮍﮎ
ﮏ
Akasema: Itupe, ewe Musa!
Verse 20
ﮐﮑﮒﮓﮔ
ﮕ
Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio.
Verse 21
Akasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza.
Verse 22
Na uambatishe mkono wako kwenye ubavu. Utatoka mweupe pasipo kuwa na madhara yoyote. Hiyo ni ishara nyengine.
Verse 23
ﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Ili tukuonyeshe baadhi ya ishara zetu kubwa.
Verse 24
ﮰﮱﯓﯔﯕ
ﯖ
Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka.
Verse 25
ﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
(Musa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,
Verse 26
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Na unifanyie nyepesi kazi yangu,
Verse 27
ﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu,
Verse 28
ﯦﯧ
ﯨ
Wapate kufahamu maneno yangu.
Verse 29
ﯩﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na nipe waziri katika watu wangu,
Verse 30
ﯯﯰ
ﯱ
Harun, ndugu yangu.
Verse 31
ﯲﯳﯴ
ﯵ
Kwake yeye niongeze nguvu zangu.
Verse 32
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Na umshirikishe katika kazi yangu.
Verse 33
ﯺﯻﯼ
ﯽ
Ili tukutakase sana.
Verse 34
ﯾﯿ
ﰀ
Na tukukumbuke sana.
Verse 35
ﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Hakika Wewe unatuona.
Verse 36
ﰆﰇﰈﰉﰊ
ﰋ
Akasema: Hakika Umepewa maombi yako, ewe Musa!
Verse 37
ﰌﰍﰎﰏﰐ
ﰑ
Na hakika tulikwisha kufanyia hisani mara nyengine...
Verse 38
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Pale tulipo mfunulia mama yako yaliyo funuliwa,
Verse 39
Ya kuwa mtie katika kisanduku, na kisha kitie mtoni, na mto utamfikisha ufukweni. Atamchukua adui yangu naye ni adui yake. Na nimekutilia mapenzi yanayo tokana kwangu, na ili ulelewe machoni mwangu.
Verse 40
Dada yako alipo kwenda na akasema: Je! Nikujuulisheni mtu wa kuweza kumlea? Basi tukakurejesha kwa mama yako ili macho yake yaburudike, wala asihuzunike. Na ulimuuwa mtu, nasi tukakuokoa katika dhiki, na tukakujaribu kwa majaribio mengi. Ukakaa miaka kwa watu wa Madyana. Kisha ukaja kama ilivyo kadiriwa, ewe Musa!
Verse 41
ﮖﮗ
ﮘ
Na nimekuteuwa kwa ajili ya nafsi yangu.
Verse 42
Nenda, wewe na ndugu yako, pamoja na ishara zangu, wala msichoke kunikumbuka.
Verse 43
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Nendeni kwa Firauni. Hakika yeye amepindukia mipaka.
Verse 44
Mwambieni maneno laini, huenda akazingatia au akaogopa.
Verse 45
Wakasema: Ewe Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tunaogopa asije akapindukia mipaka juu yetu au kufanya jeuri.
Verse 46
Akasema: Msiogope! Hakika Mimi ni pamoja nanyi. Nasikia na ninaona.
Verse 47
Basi mwendeeni, na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola wako Mlezi! Basi waache Wana wa Israili watoke nasi, wala usiwaadhibu. Sisi tumekuletea ishara itokayo kwa Mola wako Mlezi. Na amani itakuwa juu ya aliye fuata uwongofu.
Verse 48
Hakika tumefunuliwa sisi kwamba hapana shaka adhabu itamsibu anaye kadhibisha na akapuuza.
Verse 49
ﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
(Firauni) akasema: Basi Mola wenu Mlezi ni nani, ewe Musa?
Verse 50
Akasema: Mola wetu Mlezi ni yule aliye kipa kila kitu umbo lake, kisha akakiongoa.
Verse 51
ﰘﰙﰚﰛﰜ
ﰝ
Akasema: Nini hali ya karne za kwanza?
Verse 52
Akasema: Ilimu yake iko kwa Mola wangu Mlezi katika Kitabu. Mola wangu Mlezi hapotei wala hasahau.
Verse 53
Ambaye amekufanyieni ardhi kuwa tandiko, na akakupitishieni humo njia, na akakuteremshieni kutoka mbinguni maji. Na kwa hayo tukatoa namna mbali mbali za mimema.
Verse 54
Kuleni, na mchunge wanyama wenu. Hakika katika hayo zipo ishara kwa wenye akili.
Verse 55
Kutokana nayo (ardhi) tumekuumbeni, na humo tunakurudisheni, na kutoka humo tutakutoeni mara nyengine.
Verse 56
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Na hakika tulimwonyesha ishara zetu zote. Lakini alikadhibisha na akakataa.
Verse 57
Akasema: Ewe Musa! Hivyo umetujia kututoa katika nchi yetu kwa uchawi wako?
Verse 58
Basi sisi hakika tutakueletea uchawi kama huo. Basi weka miadi baina yetu na wewe, ambayo tusiivunje sisi wala wewe, mahali patapo kuwa sawa.
Verse 59
Akasema: Miadi yenu ni siku ya Sikukuu; na watu wakusanywe kabla ya adhuhuri.
Verse 60
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Basi Firauni akarudi na akatengeneza hila yake, kisha akaja.
Verse 61
Musa akamwambia: Ole wenu! Msimzulie Mwenyezi Mungu uwongo, asije akakufutilieni mbali kwa adhabu. Na mwenye kuzua lazima ashindwe!
Verse 62
ﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Basi wakazozana kwa shauri yao wenyewe kwa wenyewe, na wakanong'ona kwa siri.
Verse 63
Wakasema: Hakika hawa wawili ni wachawi, wanataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wao, na waondoe mila zenu zilizo bora kabisa.
Verse 64
Kwa hivyo kusanyeni hila zenu zote, kisha mfike kwa kujipanga safu, na kwa yakini atafuzu kweli kweli leo atakaye shinda.
Verse 65
Wakasema: Ewe Musa! Je! Utatupa wewe, au tutakuwa sisi wa kwanza kutupa?
Verse 66
Akasema: Bali tupeni nyinyi! Tahamaki kamba zao na fimbo zao zikaonekana mbele yake, kwa uchawi wao, kuwa zinapiga mbio.
Verse 67
ﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Basi Musa akaingia khofu nafsi yake.
Verse 68
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
ﭷ
Tukasema: Usikhofu! Hakika wewe ndiye utakaye shinda.
Verse 69
Na kitupe kilicho katika mkono wako wa kulia; kitavimeza walivyo viunda. Hakika walivyo unda ni hila za mchawi tu, na mchawi hafanikiwi popote afikapo.
Verse 70
Basi wachawi wakaangushwa wanasujudu. Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa Harun na Musa!
Verse 71
(Firauni) akasema: Oh! Mnamuamini kabla sijakupeni ruhusa? Hakika yeye ndiye mkubwa wenu aliye kufundisheni uchawi. Basi kwa yakini nitakukateni mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakutundikeni misalabani katika vigogo vya mitende, na hapo kwa yakini mtajua ni nani katika sisi aliye mkali wa kuadhibu na kuiendeleza adhabu yake.
Verse 72
Wakasema: Hatutokukhiari wewe kuliko ishara waziwazi zilizo tujia, na kuliko yule aliye tuumba. Basi hukumu utavyo hukumu; kwani wewe unahukumu haya ya maisha ya duniani tu.
Verse 73
Hakika sisi tumemuamini Mola wetu Mlezi ili atusamehe makosa yetu na uchawi ulio tulazimisha kuufanya. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mbora na Mwenye kudumu zaidi.
Verse 74
Hakika ataye mjia Mola wake Mlezi naye ni mkhalifu, basi kwa yakini, yake huyo ni Jahannamu. Hafi humo wala haishi.
Verse 75
Na atakaye mjia naye ni Muumini aliye tenda mema, basi hao ndio wenye vyeo vya juu.
Verse 76
Bustani za milele zipitazo mito kati yake, wadumu humo. Na hayo ni malipo ya mwenye kujitakasa.
Verse 77
Na tulimfunulia Musa: Toka usiku na waja wangu, na uwapigie njia kavu baharini. Usikhofu kukamatwa, wala usiogope.
Verse 78
Firauni akawafuata pamoja na majeshi yake. Basi kiliwafudikiza humo baharini kilicho wafudikiza.
Verse 79
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na Firauni aliwapoteza watu wake wala hakuwaongoa.
Verse 80
Enyi Wana wa Israili! Hakika tulikuokoeni na adui yenu, na tukakuahidini upande wa kulia wa mlima. Na tulikuteremshieni Manna na Salwa.
Verse 81
Kuleni katika vitu vizuri hivyo tulivyo kuruzukuni, wala msiruke mipaka katika hayo, isije ikakushukieni ghadhabu yangu. Na inaye mshukia ghadhabu yangu basi huyo ameangamia.
Verse 82
Na hakika Mimi ni Mwingi wa Kusamehe kwa anaye tubia, na akaamini, na akatenda mema, tena akaongoka.
Verse 83
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Na nini kilicho kutia haraka ukawaacha watu wako, ewe Musa?
Verse 84
Akasema: Hao wapo nyuma yangu wananifuatia. Na nimefanya haraka kukujia, Mola wangu Mlezi, ili uridhike.
Verse 85
(Mwenyezi Mungu) akasema: Sisi tumewatia mtihani watu wako baada yako, na Msamaria amewapoteza.
Verse 86
Musa akarudi kwa watu wake kwa ghadhabu na kusikitika. Akasema: Enyi watu wangu! Kwani Mola wenu Mlezi hakukuahidini ahadi nzuri? Je, umekuwa muda mrefu kwenu au mmetaka ikushukieni ghadhabu ya Mola wenu Mlezi, ndio maana mkavunja miadi yangu?
Verse 87
Wakasema: Sisi hatukuvunja miadi yako kwa khiari yetu, lakini tulibebeshwa mizigo ya mapambo ya watu, basi tukaitupa. Na hivyo ndivyo alivyo toa shauri Msamaria.
Verse 88
Na akawaundia ndama, kiwiliwili chenye sauti. Na wakasema: Huyu ndiye mungu wenu, na mungu wa Musa, lakini alisahau.
Verse 89
Je! Hawakuona kuwa hakuwarudishia neno, wala hakuweza kuwadhuru wala kuwafaa?
Verse 90
Na hakika Harun alikwisha waambia kabla yake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmetiwa mtihanini tu kwa kitu hiki. Na kwa yakini Mola wenu Mlezi ni Arrahmani, Mwingi wa Rehema. Basi nifuateni mimi, na t'iini amri yangu!
Verse 91
Wakasema: Hatutaacha kumuabudu mpaka Musa atapo rejea kwetu.
Verse 92
(Musa) akasema: Ewe Harun! Ni nini kilicho kuzuia, ulipo waona wamepotea,
Verse 93
ﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Hata usinifuate? Je, umeasi amri yangu?
Verse 94
Akasema: Ewe mwana wa mama yangu! Usinishike ndevu zangu, wala kichwa changu. Kwa hakika naliogopa usije sema: Umewafarikisha Wana wa Israil, na hukungojea kauli yangu.
Verse 95
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
(Musa) akasema: Ewe Msamaria! Unataka nini?
Verse 96
Akasema: Niliona wasiyo yaona wao, nikashika gao katika unyao wa Mtume. Kisha nikalitupa. Na hivi ndivyo ilivyo nielekeza nafsi yangu.
Verse 97
(Musa) akasema: Basi ondoka! Na kwa yakini utakuwa katika maisha ukisema: Usiniguse. Na hakika una ahadi kwako isiyo vunjwa. Na mtazame huyo mungu wako uliye endelea kumuabudu - Sisi kwa hakika tutamchoma moto, kisha tutamtawanya baharini atawanyike.
Verse 98
Hakika Mungu wenu ni Allah, Mwenyezi Mungu, tu. Hapana Mungu isipo kuwa Yeye. Ujuzi wake umeenea kila kitu.
Verse 99
Namna hivi tunakuhadithia katika khabari za yaliyo tangulia. Na hakika tumekuletea kutoka kwetu mawaidha ya kukumbukwa.
Verse 100
Atakaye jitenga nayo, basi kwa yakini Siku ya Kiyama atabeba mzigo.
Verse 101
Wadumu humo. Na ni mzigo muovu kwao kuubeba Siku ya Kiyama!
Verse 102
Siku litakapo pulizwa barugumu, na tukawakusanya wakhalifu Siku hiyo, hali macho yao ya kibuluu.
Verse 103
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Watanong'onezana wao kwa wao: Hamkukaa ila siku kumi tu.
Verse 104
Sisi tunajua zaidi watakayo yasema, atakapo sema mbora wao katika mwendo: Nyinyi hamkukaa ila siku moja tu.
Verse 105
Na wanakuuliza khabari za milima. Waambie: Mola wangu Mlezi ataivuruga vuruga.
Verse 106
ﮘﮙﮚ
ﮛ
Na ataiacha tambarare, uwanda.
Verse 107
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Hutaona humo mdidimio wala muinuko.
Verse 108
Siku hiyo watamfuata muitaji asiye na upotofu. Na sauti zote zitamnyenyekea Arrahmani Mwingi wa Rahema. Basi husikii ila mchakato na mnong'ono.
Verse 109
Siku hiyo uombezi haufai kitu, ila wa aliye mruhusu Arrahmani Mwingi wa Rehema na akamridhia kusema.
Verse 110
Yeye anajua yaliyo mbele yao, na yaliyo nyuma yao. Wala wao hawawezi kumjua Yeye vilivyo.
Verse 111
Na zitadhalilika nyuso mbele ya Aliye Hai Milele, Mwangalizi Mkuu. Na atakuwa ameharibikiwa mwenye kubeba dhulma.
Verse 112
Na anaye tenda mema, naye ni Muumini, basi hatakhofu kudhulumiwa wala kupunjwa.
Verse 113
Na namna hivi tumeiteremsha Qur'ani kwa Kiarabu, na tumekariri humo maonyo ili wapate kuogopa na kujilinda na iwaletee makumbusho.
Verse 114
Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki. Wala usiifanyie haraka hii Qur'ani, kabla haujamalizika ufunuo wake. Na sema: Mola wangu Mlezi! Nizidishie ilimu.
Verse 115
Na hapo zamani tuliagana na Adam, lakini alisahau, wala hatukuona kwake azma kubwa.
Verse 116
Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam! Wakasujudu, isipo kuwa Iblisi, alikataa.
Verse 117
Tukasema: Ewe Adam! Hakika huyu ni adui yako na wa mkeo. Basi asikutoeni katika Bustani hii, mkaingia mashakani.
Verse 118
Hakika humo hutakuwa na njaa wala hutakuwa uchi.
Verse 119
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Na hakika hutapata kiu humo wala hutapata joto.
Verse 120
Lakini Shet'ani alimtia wasiwasi, akamwambia: Ewe Adam! Nikujuulishe mti wa kuishi milele na ufalme usio koma?
Verse 121
Basi wakaula wote wawili, na uchi wao ukawadhihirikia na wakaanza kujibandika majani ya Bustani. Na Adam akamuasi Mola wake Mlezi, na akapotea njia.
Verse 122
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Kisha Mola wake Mlezi akamteuwa, naye akamkubalia toba yake, naye akamwongoa.
Verse 123
Akasema: Ondokeni humu nyote, hali ya kuwa ni maadui nyinyi kwa nyinyi. Na ukikufikieni uwongofu kutoka kwangu basi atakaye ufuata uwongofu wangu, hatapotea wala hatataabika.
Verse 124
Na atakaye jiepusha na mawaidha yangu, basi kwa yakini atapata maisha yenye dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya kuwa kipofu.
Verse 125
Aseme: Ewe Mola wangu Mlezi! Mbona umenifufua kipofu, nami nilikuwa nikiona?
Verse 126
(Mwenyezi Mungu) atasema: Ndivyo vivyo hivyo. Zilikufikia ishara zetu, nawe ukazisahau; na kadhaalika leo unasahauliwa.
Verse 127
Na hivi ndivyo tutakavyo mlipa kila apitaye kiasi, na asiye amini ishara za Mola wake Mlezi. Na hakika adhabu ya Akhera ni kali zaidi, na inadumu zaidi.
Verse 128
Je! Haikuwabainikia tu; vizazi vingapi tuliviangamiza kabla yao, nao wanatembea katika maskani zao? Hakika katika hayo zimo ishara kwa wenye akili.
Verse 129
Na lau kuwa si neno lililo kwisha tangulia kutoka kwa Mola wako Mlezi na muda ulio wekwa, bila ya shaka inge fika adhabu (hapa hapa).
Verse 130
Yavumilie haya wayasemayo. Na umtakase Mola wako Mlezi kwa kumsifu kabla ya kuchomoza jua, na kabla halijachwa, na nyakati za usiku pia umtakase, na ncha za mchana ili upate ya kukuridhisha.
Verse 131
Wala usivikodolee macho tulivyo wastareheshea baadhi ya watu miongoni mwao, kwa ajili ya mapambo ya duniani, ili tuwajaribu. Na riziki ya Mola wako Mlezi ni bora na inadumu zaidi.
Verse 132
Na waamrishe watu wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo. Sisi hatukuombi wewe riziki, bali Sisi ndio tunakuruzuku. Na mwisho mwema ni kwa mchamngu.
Verse 133
Na walisema: Kwa nini hakutuletea muujiza kutoka kwa Mola wake Mlezi? Je! Haikuwafikilia dalili wazi ya yaliyomo katika Vitabu vya kale?
Verse 134
Na lau kuwa tuliwaangamiza kwa adhabu kabla yake, wangeli sema: Ewe Mola wetu Mlezi! Kwa nini usituletee Mtume tukazifuata ishara zako kabla hatujadhilika na kuhizika.
Verse 135
Sema: Kila mmoja anangoja. Basi ngojeni! Hivi karibuni mtajua nani mwenye njia sawa na nani aliye ongoka.
تقدم القراءة