سورة طه

Ali Muhsin Al - Swahili translation

Tafsiri ya Sura Taha kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation

Ali Muhsin Al - Swahili translation

Verse 5

Arrahmani, Mwingi wa Rehema, aliye tawala juu ya Kiti cha Enzi.
Verse 41

Na nimekuteuwa kwa ajili ya nafsi yangu.
Verse 49

(Firauni) akasema: Basi Mola wenu Mlezi ni nani, ewe Musa?

Basi wakazozana kwa shauri yao wenyewe kwa wenyewe, na wakanong'ona kwa siri.

Na hakika Harun alikwisha waambia kabla yake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmetiwa mtihanini tu kwa kitu hiki. Na kwa yakini Mola wenu Mlezi ni Arrahmani, Mwingi wa Rehema. Basi nifuateni mimi, na t'iini amri yangu!

(Mwenyezi Mungu) atasema: Ndivyo vivyo hivyo. Zilikufikia ishara zetu, nawe ukazisahau; na kadhaalika leo unasahauliwa.

Na lau kuwa si neno lililo kwisha tangulia kutoka kwa Mola wako Mlezi na muda ulio wekwa, bila ya shaka inge fika adhabu (hapa hapa).
تقدم القراءة