Tafsiri ya Sura Al-Inshikak kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Al-Inshikak
Itapo chanika mbingu,
Verse 2
ﭧﭨﭩ
ﭪ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
Verse 3
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Na ardhi itakapo tanuliwa,
Verse 4
ﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
Verse 5
ﭴﭵﭶ
ﭷ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
Verse 6
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
Verse 7
ﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
Verse 8
ﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
Verse 9
ﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Na arudi kwa ahali zake na furaha.
Verse 10
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
Verse 11
ﮘﮙﮚ
ﮛ
Basi huyo ataomba kuteketea.
Verse 12
ﮜﮝ
ﮞ
Na ataingia Motoni.
Verse 13
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
Verse 14
ﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
Verse 15
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
Verse 16
ﯔﯕﯖ
ﯗ
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
Verse 17
ﯘﯙﯚ
ﯛ
Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
Verse 18
ﯜﯝﯞ
ﯟ
Na kwa mwezi unapo pevuka,
Verse 19
ﯠﯡﯢﯣ
ﯤ
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
Verse 20
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Basi wana nini hawaamini?
Verse 21
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
Verse 22
ﯲﯳﯴﯵ
ﯶ
Bali walio kufuru wanakanusha tu.
Verse 23
ﯷﯸﯹﯺ
ﯻ
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
Verse 24
ﯼﯽﯾ
ﯿ
Basi wabashirie adhabu chungu!
Verse 25
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.
تقدم القراءة