Tafsiri ya Sura An-Nazi'at kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮢﮣ
ﮤ
An-Nazi'at
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
Verse 2
ﮥﮦ
ﮧ
Na kwa wanao toa kwa upole,
Verse 3
ﮨﮩ
ﮪ
Na wanao ogelea,
Verse 4
ﮫﮬ
ﮭ
Wakishindana mbio,
Verse 5
ﮮﮯ
ﮰ
Wakidabiri mambo.
Verse 6
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
Verse 7
ﯖﯗ
ﯘ
Kifuate cha kufuatia.
Verse 8
ﯙﯚﯛ
ﯜ
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
Verse 9
ﯝﯞ
ﯟ
Macho yatainama chini.
Verse 10
ﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
Verse 11
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
Verse 12
ﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
Verse 13
ﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
Verse 14
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
Verse 15
ﯺﯻﯼﯽ
ﯾ
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
Verse 16
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
Verse 17
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
Verse 18
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
Verse 19
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
Verse 20
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
Verse 21
ﭧﭨ
ﭩ
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
Verse 22
ﭪﭫﭬ
ﭭ
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
Verse 23
ﭮﭯ
ﭰ
Akakusanya watu akanadi.
Verse 24
ﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
Verse 25
ﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
Verse 26
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
Verse 27
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
Verse 28
ﮋﮌﮍ
ﮎ
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
Verse 29
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
Verse 30
ﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
Verse 31
ﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
Verse 32
ﮞﮟ
ﮠ
Na milima akaisimamisha,
Verse 33
ﮡﮢﮣ
ﮤ
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
Verse 34
ﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
Verse 35
ﮪﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
Verse 36
ﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
Verse 37
ﯖﯗﯘ
ﯙ
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
Verse 38
ﯚﯛﯜ
ﯝ
Na akakhiari maisha ya dunia,
Verse 39
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
Verse 40
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
Verse 41
ﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
Verse 42
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
Verse 43
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Una nini wewe hata uitaje?
Verse 44
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
Verse 45
ﰁﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
Verse 46
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
تقدم القراءة