Tafsiri ya Sura Al-Lail kwa السواحلية kutoka Ali Muhsin Al - Swahili translation
Verse 1
ﮡﮢﮣ
ﮤ
Al-Lail
Naapa kwa usiku unapo funika!
Verse 2
ﮥﮦﮧ
ﮨ
Na mchana unapo dhihiri!
Verse 3
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Na kwa Aliye umba dume na jike!
Verse 4
ﮮﮯﮰ
ﮱ
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
Verse 5
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
Verse 6
ﯘﯙ
ﯚ
Na akaliwafiki lilio jema,
Verse 7
ﯛﯜ
ﯝ
Tutamsahilishia yawe mepesi.
Verse 8
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
Verse 9
ﯣﯤ
ﯥ
Na akakanusha lilio jema,
Verse 10
ﭑﭒ
ﭓ
Tutamsahilishia yawe mazito!
Verse 11
ﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
Verse 12
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
Verse 13
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
Verse 14
ﭤﭥﭦ
ﭧ
Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
Verse 15
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Hatauingia ila mwovu kabisa!
Verse 16
ﭭﭮﭯ
ﭰ
Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
Verse 17
ﭱﭲ
ﭳ
Na mchamngu ataepushwa nao,
Verse 18
ﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
Verse 19
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
Verse 20
ﮀﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
Verse 21
ﮆﮇ
ﮈ
Naye atakuja ridhika!
تقدم القراءة