Tafsiri ya Sura Al-Muddasir kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﮪﮫ
ﮬ
Ewe uliojifinika nguo zako!
Verse 2
ﮭﮮ
ﮯ
Inuka kutoka kwenye malazi yako owaonye watu adhabu ya Menyezi Mungu.
Verse 3
ﮰﮱ
ﯓ
Na umkusudie Mola wako, Peke Yake, kwa kumtukuza, kumpwekesha na kumuabudu.
Verse 4
ﯔﯕ
ﯖ
Na usafishe nguo zako kutokana na najisi, kwani usafi wa nje ni katika kutimia usafi wa ndani.
Verse 5
ﯗﯘ
ﯙ
Na uendelee daima kuyaepuka masanamu na mizimu, na matendo ya ushirikina yote usiyakaribie.
Verse 6
ﯚﯛﯜ
ﯝ
Na usitoe kitu kumpa mtu kwa lengo la kupata zaidi ya hiko. Na kwa ajili ya kupata radhi ya Mwenyezi Mungu,
Verse 7
ﯞﯟ
ﯠ
vumilia juu ya maamrisho na makatazo.
Verse 8
ﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Pindi patakapopulizwa kwenye barugumu mpulizo wa Ufufuzi na Uenezaji,
Verse 9
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
wakati huo ni wakati ambao ni mgumu kwa makafiri;
Verse 10
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
si rahisi kwao kusalimika na yale walionayo ya kujadiliwa hesabu zao na vituko vingine vikubwa.
Verse 11
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Niache mimi, ewe Mtume, na huyu niliyemuumba ndani ya tumbo la mamake akiwa peke yake, hana mali wala watoto.
Verse 12
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Nikamfanya awe na mali mengi yenye kuenea na watoto waliyoko na yeye hapo Makkah hawamuondokei. Na
Verse 13
ﯺﯻ
ﯼ
nikamsahilishia kwa kumrahisishia njia za maisha. Kisha yeye anatarajia, baada ya vitu hivi alivyopewa,
Verse 14
ﯽﯾﯿ
ﰀ
nimuongezee kwenye mali yake na watoto wake na huku yeye amenikanusha. Mambo sivyo kama anavyodai huyu mwenye kuasi, mtenda dhambi.
Verse 15
ﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Simuongezei zaidi ya hiko nilichompa,
Verse 16
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
ﰌ
kwa kuwa yeye alikuwa mshindani mkanushaji wa Qur’ani na hoja za Mwenyezi Mungu kwa viumbe Wake.
Verse 17
ﰍﰎ
ﰏ
Nitambebesha mateso magumu na usumbufu usio na mapumziko. Anayekusudiwa hapa ni Al-Walid mwana wa Al-Mughi rah aliyekuwa akishindana na haki na akijitokeza kupigana vita na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Haya ndiyo malipo ya kila mwenye kushindana na haki na kuipiga vita.
Verse 18
ﰐﰑﰒ
ﰓ
Kwa kweli yeye aliwaza ndani ya nafsi yake akatayarisha la kusema kumtukana Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani.
Verse 19
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Hivyo basi akalaaniwa na akastahili, kwa hilo, maangamivu: alijiandaa vipi ndani ya nafsi yake kwa hayo matukano?
Verse 20
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Kisha pia akalaaniwa.
Verse 21
ﭚﭛ
ﭜ
Kisha yeye alifikiria kuhusu kile alichokipanga na kukitayarisha cha kuitia dosari Qur’ani.
Verse 22
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Kisha akafinya uso wake na akazidi katika hali ile ya ukunjaji uso kwa kukosa hila za kufanya na kutopata ila yoyote ya kuitia dosari Qur’ani.
Verse 23
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Kisha akarudi kuipa mgongo haki na akajiona ni mkubwa wa kutofaa kuikubali,
Verse 24
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
hapo akasema kuhusu Qur’ani, «Haya anayoyasema Muhammad si chochote isipokuwa ni uchawi uliopokewa kutoka kwa watu wa mwanzo waliopita.
Verse 25
ﭬﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Haikuwa hi Qur’ani isipokuwa ni maneno ya viumbe ambayo Muhammad amejifunza kutoka kwao kisha akadai kuwa yanatoka kwa Mwenyezi Mungu.»
Verse 26
ﭲﭳ
ﭴ
Basi nitamuingiza kwenye moto wa Jahanamu ili alionje joto lake na achomeke kwa moto wake.
Verse 27
ﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Na ni lipi lililokujulisha wewe ni kitu gani hiyo Jahanamu?
Verse 28
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Haibakishi nyama wala haiachi mfupa isipokuwa huvichoma.
Verse 29
ﭿﮀ
ﮁ
Unageuza ngozi ya mwili, unazifanya ngozi kuwa nyeusi na unazichoma.
Verse 30
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Wanasimamia mambo yake na kushikilia kazi ya kuwatesa watu wake Malaika kumi na tisa katika washika zamu wa Motoni wenye nguvu.
Na hatukuwafanya washika hazina wa Motoni isipokuwa miongoni mwa Malaika washupavu. Na hatukuiweka idadi hiyo isipokuwa kuwatahini wale waliomkufuru Mwenyezi Mungu, na ili imani ya yakini ipatikane kwa wale Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu kwamba yaliyokuja ndani ya Qur’ani juu ya washika hazina wa Motoni ni ukweli utokao kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, kwani hayo yanaafikiana na vitabu vyao, na ili Waumini wazidi kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na waifuate Sheria Yake kivitendo, na ili wasilifanyie shaka hilo wale Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu wala wale wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na ili wapate kusema wale wenye unafiki ndani ya nyoyo zao na makafiri, «Ni lipi alilolikusudia Mwenyezi Mungu kwa idadi hii ya ajabu?» Kwa mfano wa hayo yaliyotajwa, Mwenyezi Mungu Anampoteza Anayetaka kumpoteza na Anamuongoza Anayetaka kumuongoza. Na hakuna ajuwaye idadi ya askari wa Mola wako, na miongoni mwao ni Malaika, isipokuwa Mwenyezi Mungu Peke Yake. Na haukuwa huu Moto isipokuwa ni ukumbusho na mazingatio kwa watu.
Verse 32
ﯥﯦ
ﯧ
Mambo sivyo kama walivyotaja ya ukanushaji Mtume katika yale aliyokuja nayo! Anaapa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu, kwa mwezi,
Verse 33
ﯨﯩﯪ
ﯫ
na kwa usiku unapogeuka kwenda zake,
Verse 34
ﯬﯭﯮ
ﯯ
na kwa asubuhi inapotoa mwangaza na kufunuka,
Verse 35
ﯰﯱﯲ
ﯳ
hakika Moto ni mojawapo ya mambo makubwa,
Verse 36
ﯴﯵ
ﯶ
kwa ajili ya kuwaonya na kuwatisha watu,
Verse 37
kwa anayetaka miongoni mwenu kujiweka karibu na Mola wake kwa kufanya matendo ya utiifu, au kujikalisha nyuma kwa kufanya matendo ya uasi.
Verse 38
ﯿﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Kila nafsi imefungwa na kuwekwa rahani kwa ilichokitenda, miongoni mwa matendo mema au mabaya, kwa kukichuma. Haifunguliwi mpaka itekeleze haki zilizo juu ya lazima yake na ipatiwe mateso yanayostahili kupatiwa.
Verse 39
ﰅﰆﰇ
ﰈ
Isipokuwa Waislamu waliotakaswa, watu wa upande wa kulia waliojikomboa shingo zao kwa utiifu.
Verse 40
ﰉﰊﰋ
ﰌ
Wao watakuwa kwenye mabustani ya Peponi ambayo sifa zake hazifikiwi ukomo. Watakuwa wakiulizana wao kwa wao
Verse 41
ﰍﰎ
ﰏ
kuhusu makafiri waliojikosea nafsi zao,
Verse 42
ﰐﰑﰒﰓ
ﰔ
«Ni lipi lililowaingiza kwenye moto wa Jahanamu na likawafanya
Verse 43
ﰕﰖﰗﰘﰙ
ﰚ
mlionje joto lake lililo kali sana?» Wahalifu waseme , «Hatukuwa ni miongoni mwa wanaoswali duniani,
Verse 44
ﰛﰜﰝﰞ
ﰟ
na hatukuwa tukitoa sadaka na kuwafanyia wema wahitaji na maskini,
Verse 45
ﰠﰡﰢﰣ
ﰤ
na tulikuwa tukizungumza maneno ya ubatilifu na watu wa upotofu na upotevu,
Verse 46
ﰥﰦﰧﰨ
ﰩ
na tulikuwa tukiikanusha Siku ya kuhesabiwa na kulipwa,
Verse 47
ﰪﰫﰬ
ﰭ
mpaka kifo kikatujia na hali sisi tuko kwenye mambo hayo mabaya ya upotevu.
Verse 48
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Basi hayatawafalia neno maombezi ya wenye kuombea wote, miongoni mwa Malaika, Manabii na wengineo, kwa kuwa aombewaye ni yule aliyechaguliwa na Mwenyezi Mungu na akamuidhinisha mwenye kumuombea.
Verse 49
ﭖﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Basi wana nini hawa washirikina wamejiepusha na Qur’ani na
Verse 50
ﭜﭝﭞ
ﭟ
mawaidha yaliyomo ndani yake? Kama kwamba wao ni pundamilia wanaobabaika
Verse 51
ﭠﭡﭢ
ﭣ
wanaomkimbia simba mshambulizi.
Verse 52
Lakini kila mmoja, miongoni mwa hawa washirikina, ana matumaini ateremshiwe kitabu kutoka mbinguni kilichokunjuliwa kama kile kilichoteremshiwa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Verse 53
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Mambo si hivyo kama wanavyodai. Ukweli ni kwamba wao hawaiogopi Akhera wala hawaamini kuwa kuna kufufuliwa na kulipwa.
Verse 54
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Ni kweli kwamba Qur’ani ni mawaidha yenye ufasaha, yanayotosha kuwafanya wao wawaidhike.
Verse 55
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Anayetaka kuwaidhika, basi na awaidhike kwa yaliyomo ndani yake na anufaike na uongofu wake.
Verse 56
Na hawawaidhiki kwayo isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Amewatakia kuongoka. Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Anayestahiki kuogopewa na kutiiwa, na Ndiye Anayestahiki kumsamehe anayemuamini Yeye na kumtii.
تقدم القراءة