Tafsiri ya Sura Al-Adiyat kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﮱﯓ
ﯔ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa farasi wenye kwenda shoti katika njia Yake kumkabili adui, wakitoa sauti kwa kasi ya kukimbia. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Verse 2
ﯕﯖ
ﯗ
Na wenye kutoa cheche za moto kwa kwato zao ngumu wanapokimbia kwa kasi.
Verse 3
ﯘﯙ
ﯚ
Wenye kushambulia maadui kipindi cha asubuhi.
Verse 4
ﯛﯜﯝ
ﯞ
Wakarusha vumbi kwa mbio zao.
Verse 5
ﯟﯠﯡ
ﯢ
Wakautia kati, kwa kuuzunguka kwa vipando vyao, mkusanyiko wa maadui.
Verse 6
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Hakika binadamu ni mkanushaji sana neema za Mola wake.
Verse 7
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Na yeye anakubali ukanushaji wake.
Verse 8
ﭛﭜﭝﭞ
ﭟ
Na yeye ana pupa sana la mali.
Verse 9
Kwani binadamu hajui linalomngojea mbele yake, pindi Mwenyezi Mungu Atakapowatoa wafu makaburini waende kuhesabiwa na kulipwa?
Verse 10
ﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Na (kwani yeye hajui) yakatolewa yaliyo ndani ya vifua: mema au maovu?.
Verse 11
ﭮﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Hakika Mola wao kwao na kwa amali zao, Siku Hiyo, ni Mtambuzi; hakuna chenye kufichamana Kwake.
تقدم القراءة