Tafsiri ya Sura Al-Fajr kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭤ
ﭥ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa alfajiri
Verse 2
ﭦﭧ
ﭨ
na masiku kumi ya kwanza ya Mfungotatu na kwa kile kilichoyafanya yawe matukufu,
Verse 3
ﭩﭪ
ﭫ
kwa kila idadi igawanyikayo na isiyogawanyika,
Verse 4
ﭬﭭﭮ
ﭯ
kwa usiku upitapo na giza lake.
Verse 5
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Kwani hakuna katika kiapo kiliyotajwa chenye kukinaisha kwa mwenye akili?
Verse 6
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
ﭽ
Huoni, ewe Mtume, vipi Mola wako
Verse 7
ﭾﭿﮀ
ﮁ
Alivyoiangamiza kaumu ya Ād'. kabila la Irama lenye nguvu na majengo yaliyoinuliwa juu ya vipia,
Verse 8
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
ambalo hakukuumbwa mfano wake katika miji, kwa ukubwa wa miili na wingi wa nguvu?
Verse 9
ﮉﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Na vipi Alivyowafanya Thamūd, kaumu ya Ṣāliḥ, ambao waliweza kuchonga jabali na kufanya nyumba ndani yake?
Verse 10
ﮏﮐﮑ
ﮒ
Na vipi Alivyomfanya Firauni, mfalme wa Misri, aliyekuwa na askari waliouhami ufalme wake na kuutilia nguvu.
Verse 11
ﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Hawa ndio waliokitumia nguvu na kudhulumu mijini.
Verse 12
ﮘﮙﮚ
ﮛ
Wakaeneza humo, kwa dhuluma zao, uharibifu.
Verse 13
ﮜﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Mwenyezi Mungu Akawamiminia adhabu kali.
Verse 14
ﮢﮣﮤ
ﮥ
Hakika Mola wako,ewe Mtume, Anamwangalia mwenye kumuasi kwa kumpa muhula kidogo, kisha Humpatiliza kwa uwezo na ushindi..
Verse 15
Huyu binadamu, Mola wake Anapompa mtihani wa neema, Anapomkunjulia riziki yake na kumpa maisha mazuri, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye ana cheo kwa Mola wake na huwa akisema :»Mola wangu Amenitukuza.»
Verse 16
Na Anapomuonja na Akambania riziki yake, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye amefanywa mnyonge na Mwenyezi Mungu na huwa akisema: «Mola wangu Amenifanya mnyonge.».
Verse 17
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
ﯤ
Hali ya mambo si kama anavyodhania binadamu huyu, kwani mtu hutukuzwa kwa kumtii Mwenyzi Mungu na hufanywa mnyonge kwa kumuasi Mwenyezi Mungu. Na nyinyi hamwakirimu mayatima na kuwatendea wema.
Verse 18
ﯥﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Wala hamhimizani kulisha maskini.
Verse 19
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Na mnakula haki za watu, katika kurithi, kwa pupa.
Verse 20
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Na mnapenda mali kupita kiasi.
Verse 21
Basi hali zenu zisiwe namna hiyo. Kumbukeni pindi ardhi itakapotikiswa na kuvunjwavunjwa.
Verse 22
ﯽﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Na Akaja Mola wako kutoa uamuzi kwa waja Wake hali Malaika wamepiga safu.
Verse 23
Na ukaletwa, Siku Hiyo kubwa, moto wa Jahanamu. Hiyo ndiyo Siku kafiri atakumbuka na kutubia. Kutamfalia nini sasa kukumbuka kwake na kutubia, na yeye katika ulimwengu alikuwa ameyapuuza hayo, na wakati wake umekwisha kupita?
Verse 24
ﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Atakuwa akisema: ‘Laiti mimi nilitanguliza ulimwenguni amali zenye kunifaa katika maisha yangu ya Akhera’.
Verse 25
ﭡﭢﭣﭤﭥ
ﭦ
Katika Siku Hiyo ngumu yenye vituko, hakuna atakaye kuweza kuadhibu kama adhabu ya Mwenyezi Mungu kwa anayemuasi.
Verse 26
ﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Na hakuna atakaye kuweza kufunga kama kifungo Chake wala kufikia hadi yake.
Verse 27
ﭬﭭﭮ
ﭯ
Ewe nafsi iliyotulia kwa kumtaja Mwenyezi Mungu, kumwamini Yeye na kuamini starehe ya Pepo Aliyowaandalia waumini!
Verse 28
ﭰﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Rudi kwa Mola wako hali ya kuridhika na takrima ya Mwenyezi Mungu kwako na hali ya kuwa Mwenyezi Mungu Ameridhika na wewe.
Verse 29
ﭶﭷﭸ
ﭹ
Ingia miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu walio wema
Verse 30
ﭺﭻ
ﭼ
na ingia kwenye Pepo yangu.
تقدم القراءة