Tafsiri ya Sura Al-Buruj kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu zenye njia za kupitia jua na mwezi.
Verse 2
ﭟﭠ
ﭡ
Na kwa Siku ya Kiyama ambayo Amewaahidi viumbe kuwa Atawakusanya.
Verse 3
ﭢﭣ
ﭤ
Na kwa shahidi, mwenye kutoa ushahidi, na mwenye kutolewa ushahidi juu yake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Anachokitaka. Lakini kiumbe hafai kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Verse 4
ﭥﭦﭧ
ﭨ
Wamelaaniwa waliofukua chini ya ardhi shimo kubwa ili kuwatesa Waumini.
Verse 5
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Wakawasha moto mkubwa wenye kuni nyingi.
Verse 6
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Wakawa wamekaa kwenye kingo za shimo hilo.
Verse 7
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Wakishuhudia vitendo vya mateso na adhabu wanavyowafanyia Waumini.
Verse 8
Na hawakuwatesa mateso hayo isipokuwa wenye kuteswa walikuwa wanamuamini Mwenyezi Mungu Mshindi Asiyeshindwa, Mhimidiwa wa maneno Yake vitendo Vyake na sifa Zake.
Verse 9
Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi Ambaye, kutakasika na sifa za upungufu ni kwake, Anashuhudia kila kitu, hakuna kinachofichika kwake.
Verse 10
Hakika, wale waliowachoma kwa moto Waumini, wa kike na wa kiume, ili kuwazuia watu na dini ya Mwenyezi Mungu, kisha wasitubie, watapata, Siku ya Akhera, adhabu ya Jahanamu na watapata adhabu kali yenye kuchoma.
Verse 11
Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya amali njema, watapata Pepo ambayo chini ya majumba yake ya kifahari yapita mito. Huko ni kufaulu kukubwa.
Verse 12
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Hakika malipizo ya Mola wako kwa maadui Zake na mateso Yake juu yao ni mazito.
Verse 13
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Ndiye Yeye Mwenye kuanzisha kuumba na kisha kurudisha.
Verse 14
ﯙﯚﯛ
ﯜ
Ndiye Yeye Mwingi wa kusamehe kwa wenye kutubia, Mwingi wa mapenzi kwa wanaoikurubisha kwake.
Verse 15
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Mwenye Arshi tukufu.
Verse 16
ﯡﯢﯣ
ﯤ
Mfanya Alitakalo: hakuna kitu Anachotaka kiwe kisiwe.
Verse 17
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Je, ewe Mtume, imekufikia habari ya makundi yaliyokufuru na kukanusha Mitume walioletwa, ya
Verse 18
ﯪﯫ
ﯬ
Firauni na Thamūd, misiba na adhabu iliyowashukia? Hawakuzingatia kwa habari hiyo.
Verse 19
ﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Bali waliokufuru waendelea kukanusha kwao, kama walivyokuwa waliokuja kabla yao.
Verse 20
ﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na Mwenyezi Mungu Amewazunguka kwa Ujuzi na Uweza Wake, hakuna chenye kufichika Kwake kuhusu wao na vitendo vyao. Hii Qu’ani siyo kama wanavyodai wenye kukanusha katika washirikina kuwa ni mashairi na uchawi ndipo wakaikanusha.
Verse 21
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Bali hii ni Qur’ani kubwa iliyo tukufu,
Verse 22
ﯽﯾﯿ
ﰀ
iliyomo kwenye Ubao Uliohifadhiwa, haufikiwi na kubadilishwa wala kupotoshwa.
تقدم القراءة