Tafsiri ya Sura Al-Balad kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
Verse 1
ﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mji huu mtakatifu wa Makkah.
Verse 2
ﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Na wewe, ewe Nabii, ni mkazi wa mji huu mtakatifu.
Verse 3
ﮇﮈﮉ
ﮊ
Na Anaapa kwa mzazi wa wanaadamu, ambaye ni Ādam, amani imshukie, na kilichozalikana na yeye.
Verse 4
ﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Hakika Tumemuumba binadamu katika usumbufu na shida za kilimwengu.
Verse 5
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Kwani anadhani kwa mali aliyoyakusanya kuwa Mwenyezi Mungu Hatakuwa na uwezo juu yake?
Verse 6
ﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Huwa akisema kwa kujigamba: «Nimetumia mali mengi.»
Verse 7
ﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Kwani anadhani, kwa kitendo chake hiko, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda, Hamuoni wala hatamhesabu juu ya kubwa na dogo?
Verse 8
ﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Kwani hatukumpa macho mawili ya kuonea,
Verse 9
ﮨﮩ
ﮪ
ulimi na midomo miwili ya kusemea
Verse 10
ﮫﮬ
ﮭ
na kumfafanulia njia mbili: ya kheri na ya shari?
Verse 11
ﮮﮯﮰ
ﮱ
Basi ajiepushe na janga la Akhera kwa kutoa mali yake ili aokoke.
Verse 12
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Ni kitu gani kilichojulisha ni lipi hilo janga la Akhera na ni mambo gani yenye kusaidia kujiepusha nalo?
Verse 13
ﯘﯙ
ﯚ
Ni kuacha huru shingo iliyoamini kuikomboa na utumwa.
Verse 14
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Au kulisha, wakati wa shida ya njaa,
Verse 15
ﯢﯣﯤ
ﯥ
yatima mwenye ujamaa, ili ipatikane fadhila ya sadaka na ya kuunga kizazi,
Verse 16
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
au masikini asiyekuwa na kitu.
Verse 17
Kisha akawa, baada ya kufanya amali njema zilizotajwa, ni miongoni mwa waliotakasa Imani yao kwa Mwenyezi Mungu, wakausiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu kwa kufuata maamrisho Yake na kujiepusha na vitendo vya kumuasi na wakausiana kuwahurumia viumbe.
Verse 18
ﯵﯶﯷ
ﯸ
Wenye kufanya hayo ndiwo watu wa kulia ambao watapelekwa Siku ya Kiyama upande wa kulia kuelekea Peponi.
Verse 19
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Na wale waliokanusha Qur’ani ndio ambao watapelekwa, Siku ya Kiyama, upande wa kushoto kuelekea Motoni.
Verse 20
ﭘﭙﭚ
ﭛ
Malipo yao ni Moto wa Jahanamu wenye kuwafinika na kuwaziba.
تقدم القراءة