سورة البلد

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Tafsiri ya Sura Al-Balad kwa السواحلية kutoka الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

Verse 3
Na Anaapa kwa mzazi wa wanaadamu, ambaye ni Ādam, amani imshukie, na kilichozalikana na yeye.
Kwani anadhani kwa mali aliyoyakusanya kuwa Mwenyezi Mungu Hatakuwa na uwezo juu yake?
Kwani anadhani, kwa kitendo chake hiko, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda, Hamuoni wala hatamhesabu juu ya kubwa na dogo?
Verse 10
na kumfafanulia njia mbili: ya kheri na ya shari?
Verse 11
Basi ajiepushe na janga la Akhera kwa kutoa mali yake ili aokoke.
Verse 12
Ni kitu gani kilichojulisha ni lipi hilo janga la Akhera na ni mambo gani yenye kusaidia kujiepusha nalo?
Verse 13
Ni kuacha huru shingo iliyoamini kuikomboa na utumwa.
Verse 15
yatima mwenye ujamaa, ili ipatikane fadhila ya sadaka na ya kuunga kizazi,
Kisha akawa, baada ya kufanya amali njema zilizotajwa, ni miongoni mwa waliotakasa Imani yao kwa Mwenyezi Mungu, wakausiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu kwa kufuata maamrisho Yake na kujiepusha na vitendo vya kumuasi na wakausiana kuwahurumia viumbe.
Verse 18
Wenye kufanya hayo ndiwo watu wa kulia ambao watapelekwa Siku ya Kiyama upande wa kulia kuelekea Peponi.
Na wale waliokanusha Qur’ani ndio ambao watapelekwa, Siku ya Kiyama, upande wa kushoto kuelekea Motoni.
Verse 20
Malipo yao ni Moto wa Jahanamu wenye kuwafinika na kuwaziba.
تقدم القراءة