يَٰحَسۡرَةً عَلَى ٱلۡعِبَادِۚ مَا يَأۡتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ni hasara iliyoje na majuto yalioje ya waja Siku ya Kiyama watakapoiona adhabu! Hawajiwi na mtume yoyote kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, isipokuwa huwa wakimfanyia shere na maskhara.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس