ٱتَّبِعُواْ مَن لَّا يَسۡـَٔلُكُمۡ أَجۡرٗا وَهُم مُّهۡتَدُونَ
Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wafuateni wale wasiotaka mali kutoka kwenu kwa kufikisha Ujumbe na hali wao wako kwenye uongofu katika kile wanachowaitia cha kumuabudu Mwenyezi Mungu Peke Yake.» Katika hii kuna kueleza ubora wa mwenye kukimbilia kuamrisha mema na kukataza maovu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس