فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ تَوۡصِيَةٗ وَلَآ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِمۡ يَرۡجِعُونَ
Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hawataweza hawa washirikina wakati wa kuvuviwa barugumu kumuusia yoyote kitu chochote, wala hawataweza kurejea kwa watu wao, bali watakufa wakiwa kwenye masoko yao na pale walipo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس