ترجمة معاني سورة نوح باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
Nouh
Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.
آية رقم 2
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,
آية رقم 3
ﮎﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.
آية رقم 4
Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!
آية رقم 5
Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,
آية رقم 6
ﮱﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.
آية رقم 7
Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!
آية رقم 8
ﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Tena niliwaita kwa uwazi,
آية رقم 9
Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.
آية رقم 10
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.
آية رقم 11
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.
آية رقم 12
Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.
آية رقم 13
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
ﭦ
Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?
آية رقم 14
ﭧﭨﭩ
ﭪ
Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?
آية رقم 15
Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?
آية رقم 16
Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?
آية رقم 17
ﭼﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi kama mimea.
آية رقم 18
ﮂﮃﮄﮅﮆ
ﮇ
Kisha atakurudsheni humo na atakutoeni tena.
آية رقم 19
ﮈﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.
آية رقم 20
ﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.
آية رقم 21
Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara.
آية رقم 22
ﮡﮢﮣ
ﮤ
Na wakapanga vitimbi vikubwa.
آية رقم 23
Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.
آية رقم 24
Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
آية رقم 25
Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Mwenyezi Mungu.
آية رقم 26
Na Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!
آية رقم 27
Hakika ukiwaacha watawapoteza waja wako, wala wao hawatazaa ila waovu makafiri.
آية رقم 28
Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
تقدم القراءة