مَا يَنظُرُونَ إِلَّا صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ تَأۡخُذُهُمۡ وَهُمۡ يَخِصِّمُونَ
Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hawangojei hawa washirikina wanaolifanyia haraka agizo la Mwenyezi Mungu kwao, isipokuwa mvuvio wa fazaa wakati Kiyama kitakaposimama, kitawachukua ghafla, na hali wao wanagombana katika mambo ya maisha yao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس