ترجمة معاني سورة الإنفطار باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Al-Infitar
Mbingu itapo chanika,
آية رقم 2
ﭕﭖﭗ
ﭘ
Na nyota zitapo tawanyika,
آية رقم 3
ﭙﭚﭛ
ﭜ
Na bahari zitakapo pasuliwa,
آية رقم 4
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Na makaburi yatapo fukuliwa,
آية رقم 5
ﭡﭢﭣﭤﭥ
ﭦ
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
آية رقم 6
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
آية رقم 7
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
آية رقم 8
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
آية رقم 9
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
آية رقم 10
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
آية رقم 11
ﮃﮄ
ﮅ
Waandishi wenye hishima,
آية رقم 12
ﮆﮇﮈ
ﮉ
Wanayajua mnayo yatenda.
آية رقم 13
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
آية رقم 14
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
آية رقم 15
ﮔﮕﮖ
ﮗ
Wataingia humo Siku ya Malipo.
آية رقم 16
ﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Na hawatoacha kuwamo humo.
آية رقم 17
ﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
آية رقم 18
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
آية رقم 19
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
تقدم القراءة