ترجمة معاني سورة الزخرف باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮀ
ﮁ
Az-Zukhruf
H'a Mim
آية رقم 2
ﮂﮃ
ﮄ
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha.
آية رقم 3
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
Hakika Sisi tumeifanya Qur'ani kwa Kiarabu ili mfahamu.
آية رقم 4
Na hakika hiyo imo katika Asili ya Maandiko yalioko kwetu, ni tukufu na yenye hikima.
آية رقم 5
Je! Tuache kukukumbusheni kabisa kwa kuwa nyinyi ni watu mlio pita mipaka kwa ukafiri?
آية رقم 6
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Na Manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani!
آية رقم 7
Na hawajii Nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli.
آية رقم 8
Na tuliwaangamiza walio kuwa na nguvu kushinda wao. Na mfano wa watu wa zamani umekwisha pita.
آية رقم 9
Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi,
آية رقم 10
Ambaye amekufanyieni ardhi kama tandiko, na akakufanyieni ndani yake njia mpate kuongoka.
آية رقم 11
Na ambaye ndiye aliye teremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyo kufa. Na namna hivi ndivyo mtakavyo tolewa.
آية رقم 12
Na ambaye ndiye aliye umba katika kila kitu jike na dume, na akakufanyieni marikebu na wanyama mnao wapanda.
آية رقم 13
Ili mkae vizuri migongoni mwao, kisha mkumbuke neema za Mola wenu Mlezi mnapokaa sawa sawa juu yao na mseme: Ametakasika aliye mfanya huyu atutumikie, na tusingeli weza kufanya haya wenyewe.
آية رقم 14
ﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.
آية رقم 15
Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila aliye dhaahiri.
آية رقم 16
Au amejichukulia watoto wanawake katika vile alivyo viumba, na akakuteulieni nyinyi watoto wanaume?
آية رقم 17
Na anapo bashiriwa mmoja wao kwa yale aliyo mpigia mfano Mwenyezi Mungu, uso wake husawijika na hujaa hasira.
آية رقم 18
Ati aliye lelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema kwa bayana...?
آية رقم 19
Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa!
آية رقم 20
Nao husema: Angeli penda Mwingi wa Rehema tusingeli waabudu sisi. Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uwongo tu!
آية رقم 21
Kwani tuliwapa Kitabu kabla ya hichi, na ikawa wao wanakishikilia hicho?
آية رقم 22
Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, basi na sisi tunaongoza nyayo zao.
آية رقم 23
Na kadhaalika hatukumtuma mwonyaji kwenye mji wowote ila watu wake walio deka kwa starehe walisema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, na sisi tunafuata nyayo zao.
آية رقم 24
Akasema (Mwonyaji): Hata nikikuleteeni yenye uwongofu bora kuliko mlio wakuta nao baba zenu? Wakasema: Sisi tunayakataa tu hayo mliyo tumwa.
آية رقم 25
Basi tukawalipizia. Angalia ulikuwaje mwisho wa walio kadhibisha!
آية رقم 26
Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Hakika mimi ninajitenga mbali na hayo mnayo yaabudu,
آية رقم 27
ﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Isipo kuwa yule aliye niumba, kwani Yeye ataniongoa.
آية رقم 28
Na akalifanya hili liwe neno lenye kubaki katika vizazi vyake ili warejee.
آية رقم 29
Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka ikawafikia Haki na Mtume aliye bainisha.
آية رقم 30
Na ilipo wafikia Haki wakasema: Huu ni uchawi, na sisi hakika tunaukataa.
آية رقم 31
Na walisema: Kwa nini Qur'ani hii haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii?
آية رقم 32
Kwani wao ndio wanao gawa rehema za Mola wako Mlezi? Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani, na tukawanyanyua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja nyingi; kwa hivyo baadhi yao wanawafanya wenginewe wawatumikie. Na rehema za Mwenyezi Mungu ni bora kuliko hayo wanayo yakusanya.
آية رقم 33
Na lau isinge kuwa watu watakuwa kundi moja tungeli wajaalia wanao mkufuru Rahmani wana nyumba zao zina dari ya fedha, na ngazi zao pia wanazo pandia,
آية رقم 34
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Na milango ya nyumba zao na vitanda wanavyo egemea juu yake,
آية رقم 35
Na mapambo. Lakini hayo si chochote ila ni starehe ya maisha ya dunia tu, na Akhera iliyoko kwa Mola wako Mlezi ni ya wenye kumchamngu.
آية رقم 36
Anaye yafanyia upofu maneno ya Rahmani tunamwekea Shet'ani kuwa ndiye rafiki yake.
آية رقم 37
Na hakika wao wanawazuilia Njia na wenyewe wanadhani kuwa wameongoka.
آية رقم 38
Hata atakapo tujia atasema: Laiti ungeli kuwako baina yangu na wewe kama umbali baina ya mashariki na magharibi. Rafiki mwovu mno wewe!
آية رقم 39
Na kwa kuwa mlidhulumu, haitakufaeni kitu leo kwamba nyinyi mnashirikiana katika adhabu.
آية رقم 40
Je! Unaweza kuwasikilizisha viziwi, au unaweza kuwaongoa vipofu na waliomo katika upotofu ulio wazi?
آية رقم 41
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Na hata tukikuondoa, Sisi tutalipiza kisasi chetu kwao.
آية رقم 42
Au tutakuonyesha tulio waahidi. Nasi bila ya shaka tuna uweza juu yao.
آية رقم 43
Basi wewe yashike yaliyo funuliwa kwako. Hakika wewe uko kwenye Njia Iliyo Nyooka.
آية رقم 44
Na hakika haya ni ukumbusho kwako na kwa kaumu yako. Na mtakuja ulizwa.
آية رقم 45
Na waulize Mitume wetu tulio watuma kabla yako: Je! Tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Rah'mani?
آية رقم 46
Na bila ya shaka tulimtuma Musa kwa Ishara zetu ende kwa Firauni na waheshimiwa wake, na akasema: Hakika mimi ni Mtume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote!
آية رقم 47
Lakini alipo wajia na Ishara zetu wakaingia kuzicheka.
آية رقم 48
Na hatukuwaonyesha Ishara yoyote ila hiyo ilikuwa kubwa zaidi kuliko nyenginewe. Na tukawakamata kwa adhabu ili warejee.
آية رقم 49
Na wakasema: Ewe mchawi! Tuombee kwa Mola wako Mlezi kwa ile ahadi aliyo kuahidi; hakika sisi tutakuwa wenye kuongoka.
آية رقم 50
Basi tulipo waondolea adhabu hiyo, mara wakaingia kuvunja ahadi.
آية رقم 51
Na Firauni alitangaza kwa watu wake, akisema: Enyi watu wangu! Kwani mimi sinao huu ufalme wa Misri, na hii mito inapita chini yangu? Je! Hamwoni?
آية رقم 52
Au mimi si bora kuliko huyu aliye mnyonge, wala hawezi kusema waziwazi?
آية رقم 53
Basi mbona hakuvikwa vikuku vya dhahabu, au hawakuja Malaika pamoja naye wakamwandama?
آية رقم 54
Basi aliwachezea watu wake, na wakamt'ii. Kwa hakika hao walikuwa watu wapotovu.
آية رقم 55
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Walipo tukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote!
آية رقم 56
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Kisha tukawafanya kuwa watangulizi na mfano kwa wa baadaye.
آية رقم 57
Na alipo pigiwa mfano Mwana wa Mariamu, watu wako waliupiga ukelele.
آية رقم 58
Wakasema: Miungu yetu kwani si bora kuliko huyu? Hawakukupigia mfano huo ila kwa ubishi tu. Bali hao ni watu wagomvi!
آية رقم 59
Hakuwa yeye (Isa) ila ni Mtumwa tuliye mneemesha na tukamfanya ni mfano kwa Wana wa Israili.
آية رقم 60
Na tungeli penda tungeli wafanyia miongoni mwenu Malaika katika ardhi wakifuatana.
آية رقم 61
Na kwa hakika yeye ni alama ya Saa ya Kiyama. Basi usiitilie shaka, na nifuateni. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
آية رقم 62
Wala asikuzuilieni Shet'ani. Hakika yeye ni adui yenu wa dhaahiri.
آية رقم 63
Na alipo kuja Isa na dalili zilizo wazi, alisema: Nimekujieni na hikima, na ili nikuelezeni baadhi ya yale mliyo khitalifiana. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na mnit'ii mimi.
آية رقم 64
Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na ni Mola wenu Mlezi. Basi Muabuduni Yeye tu. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
آية رقم 65
Lakini makundi kwa makundi yao yalikhitalifiana wao kwa wao. Ole wao walio dhulumu kwa adhabu ya siku chungu.
آية رقم 66
Je! Nini wanangojea ila Saa iwajie kwa ghafla na wala wao hawatambui?
آية رقم 67
Siku hiyo marafiki watakuwa ni maadui, wao kwa wao, isipo kuwa wachamngu.
آية رقم 68
Enyi waja wangu! Hamtakuwa na khofu siku hiyo, wala hamtahuzunika.
آية رقم 69
ﮭﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Ambao waliziamini Ishara zangu na walikuwa Waislamu.
آية رقم 70
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Ingieni Peponi, nyinyi na wake zenu; mtafurahishwa humo.
آية رقم 71
Watakuwa wanapitishiwa sahani za dhahabu na vikombe; na vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia, na nyinyi mtakaa humo milele.
آية رقم 72
Na hiyo ni Pepo mliyo rithishwa kwa hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
آية رقم 73
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Mnayo humo matunda mengi mtakayo yala.
آية رقم 74
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Kwa hakika wakosefu watakaa katika adhabu ya Jahannamu.
آية رقم 75
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Hawatapumzishwa nayo na humo watakata tamaa.
آية رقم 76
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Wala Sisi hatukuwadhulumu, bali wao ndio walio kuwa madhaalimu.
آية رقم 77
Nao watapiga kelele waseme: Ewe Malik! Na atufishe Mola wako Mlezi! Naye aseme: Hakika nyinyi mtakaa humo humo!
آية رقم 78
Kwa yakini tulikuleteeni Haki, lakini wengi katika nyinyi mlikuwa mnaichukia Haki.
آية رقم 79
ﭸﭹﭺﭻﭼ
ﭽ
Au waliweza kupitisha amri yao? Bali ni Sisi ndio tunao pitisha.
آية رقم 80
Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong'ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika.
آية رقم 81
Sema: Ingeli kuwa Rahmani ana mwana, basi mimi ningeli kuwa wa kwanza kumuabudu.
آية رقم 82
Ametakasika Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, Mola Mlezi wa A'rshi, na hayo wanayo msifia.
آية رقم 83
Basi waache wapige porojo wakicheza mpaka wakutwe na hiyo siku yao waliyo ahidiwa.
آية رقم 84
Na Yeye ndiye Mungu mbinguni, na ndiye Mungu katika ardhi. Naye ndiye Mwenye hikima, Mwenye ujuzi.
آية رقم 85
Na ametukuka Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo ndani yake. Na uko kwake ujuzi wa Saa ya Kiyama, na kwake Yeye mtarudishwa.
آية رقم 86
Wala hao mnao waomba badala yake Yeye hawana uweza wa kumwombea mtu, isipo kuwa anaye shuhudia kwa haki, na wao wanajua.
آية رقم 87
Na ukiwauliza ni nani aliye waumba? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu! Basi ni wapi wanako geuziwa?
آية رقم 88
Na usemi wake (Mtume) ni: Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika hawa ni watu wasio amini.
آية رقم 89
Basi wasamehe, na uwambie maneno ya salama. Watakuja jua.
تقدم القراءة