ترجمة معاني سورة الطور باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮞ
ﮟ
At-Tur
Naapa kwa mlima wa T'ur,
آية رقم 2
ﮠﮡ
ﮢ
Na Kitabu kilicho andikwa
آية رقم 3
ﮣﮤﮥ
ﮦ
Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
آية رقم 4
ﮧﮨ
ﮩ
Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
آية رقم 5
ﮪﮫ
ﮬ
Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
آية رقم 6
ﮭﮮ
ﮯ
Na kwa bahari iliyo jazwa,
آية رقم 7
ﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
آية رقم 8
ﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Hapana wa kuizuia.
آية رقم 9
ﯛﯜﯝﯞ
ﯟ
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
آية رقم 10
ﯠﯡﯢ
ﯣ
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
آية رقم 11
ﯤﯥﯦ
ﯧ
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
آية رقم 12
ﯨﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
آية رقم 13
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
آية رقم 14
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
ﯻ
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
آية رقم 15
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
آية رقم 16
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
آية رقم 17
ﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
آية رقم 18
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
آية رقم 19
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
آية رقم 20
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
آية رقم 21
Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
آية رقم 22
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
آية رقم 23
Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
آية رقم 24
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
آية رقم 25
ﯓﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Wataelekeana wakiulizana.
آية رقم 26
Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
آية رقم 27
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
آية رقم 28
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
آية رقم 29
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
آية رقم 30
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
آية رقم 31
ﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
آية رقم 32
Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
آية رقم 33
Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
آية رقم 34
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
آية رقم 35
Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
آية رقم 36
Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
آية رقم 37
Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
آية رقم 38
Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
آية رقم 39
ﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
آية رقم 40
Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
آية رقم 41
ﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
آية رقم 42
Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
آية رقم 43
Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
آية رقم 44
Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
آية رقم 45
Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
آية رقم 46
Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
آية رقم 47
Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
آية رقم 48
Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
آية رقم 49
ﰋﰌﰍﰎﰏ
ﰐ
Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.
تقدم القراءة