ترجمة معاني سورة مريم باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭑ
ﭒ
Marya
Kaf Ha Ya A'yn S'ad
آية رقم 2
ﭓﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
Huu ni Ukumbusho wa rehema ya Mola wako Mlezi kwa mja wake, Zakariya.
آية رقم 3
ﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Alipo mwita Mola wake Mlezi kwa siri.
آية رقم 4
Akasema: Mola wangu Mlezi! Mafupa yangu yamedhoofika, na kichwa kinameremeta kwa mvi; wala, Mola wangu Mlezi, sikuwa mwenye bahati mbaya kwa kukuomba Wewe.
آية رقم 5
Na hakika mimi nawakhofia jamaa zangu baada yangu. Na mke wangu ni tasa. Basi nipe mrithi kutoka kwako.
آية رقم 6
Atakaye nirithi mimi na awarithi ukoo wa Yaaqub. Ewe Mola wangu Mlezi! Na umjaalie awe mwenye kuridhisha.
آية رقم 7
(Akaambiwa): Ewe Zakariya! Hakika Sisi tunakubashiria mwana; jina lake ni Yahya. Hatujapata kumpa jina hilo yeyote kabla yake.
آية رقم 8
Akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Vipi nitakuwa na mwana na hali mke wangu ni tasa, na mimi nimesha fikia ukongwe katika uzee?
آية رقم 9
Akasema: Ndio hivyo hivyo amesema Mola wako Mlezi: Haya ni mepesi kwangu. Na hakika Mimi nilikwisha kuumba wewe zamani na hali hukuwa kitu.
آية رقم 10
Akasema: Mola wangu Mlezi nijaalie Ishara. Akasema Ishara yako ni kuwa hutasema na watu kwa masiku matatu, na hali ni mzima.
آية رقم 11
Basi akawatokea watu wake kutoka mihirabuni. Akawaashiria: Msabihini Mwenyezi Mungu asubuhi na jioni.
آية رقم 12
Ewe Yahya! Kishike Kitabu kwa nguvu! Nasi tulimpa hikima angali mtoto.
آية رقم 13
Na tukampa huruma itokayo kwetu, na utakaso, na akawa mchamungu.
آية رقم 14
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Na akawa mwema kwa wazazi wake, wala hakuwa jabari mua'si.
آية رقم 15
Na amani iwe juu yake siku ya kuzaliwa, na siku ya kufa, na siku ya kufufuliwa.
آية رقم 16
Na mtaje Maryamu katika Kitabu, pale alipo jitenga na jamaa zake mahali upande wa mashariki;
آية رقم 17
Na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea Roho wetu, akajifananisha kwake sawa na mtu.
آية رقم 18
(Maryamu) akasema: Hakika mimi najikinga kwa Mwingi wa Rehema aniepushe nawe, ukiwa ni mchamngu.
آية رقم 19
(Malaika) akasema: Hakika mimi ni mwenye kutumwa na Mola wako Mlezi ili nikubashirie tunu ya mwana aliye takasika.
آية رقم 20
Akasema: Nitampataje mwana hali mwanaadamu yeyote hajanigusa, wala mimi si kahaba?
آية رقم 21
(Malaika) akasema: Ndio hivyo hivyo! Mola wako Mlezi amesema: Haya ni mepesi kwangu! Na ili tumfanye kuwa ni Ishara kwa watu, na Rehema itokayo kwetu, na hilo ni jambo lilio kwisha hukumiwa.
آية رقم 22
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali.
آية رقم 23
Kisha uchungu ukampeleka kwenye shina la mtende; akasema: Laiti ningeli kufa kabla ya haya, na nikawa niliye sahaulika kabisa!
آية رقم 24
Pakatangazwa kutoka chini yake: Usihuzunike! Hakika Mola wako Mlezi amejaalia chini yako kijito kidogo cha maji!
آية رقم 25
Na litikise kwako hilo shina la mtende, utakuangushia tende nzuri zilizo mbivu.
آية رقم 26
Basi kula, na kunywa, na litue jicho lako. Na pindi ukimwona mtu yeyote basi sema: Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu ya kufunga; kwa hivyo leo sitasema na mtu.
آية رقم 27
Akenda naye (mwanawe) kwa jamaa zake amembeba. Wakasema: Ewe Maryamu! Hakika umeleta kitu cha ajabu!
آية رقم 28
Ewe dada yake Harun! Baba yako hakuwa mtu muovu, wala mama yako hakuwa kahaba.
آية رقم 29
Akawaashiria (mtoto). Wakasema: Vipi tumsemeze aliye bado mdogo yumo katika mlezi?
آية رقم 30
(Mtoto) akasema: Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu. Amenipa Kitabu, na amenifanya Nabii.
آية رقم 31
Na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo. Na ameniusia Sala na Zaka maadamu ni hai,
آية رقم 32
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Na nimtendee wema mama yangu. Wala hakunifanya niwe jeuri, mwovu.
آية رقم 33
Na amani iko juu yangu siku niliyo zaliwa, na siku nitakayo kufa, na siku nitakayo fufuliwa kuwa hai.
آية رقم 34
Huyo ndiye Isa mwana wa Maryamu. Ndiyo kauli ya haki ambayo wanaifanyia shaka.
آية رقم 35
Haiwi kwa Mwenyezi Mungu kuwa na mwana, Subhanahu, Yeye ametakasika! Anapo lihukumia jambo basi huliambia tu: Kuwa! Likawa.
آية رقم 36
Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
آية رقم 37
Lakini makundi yakakhitalifiana wao kwa wao. Basi ole wao hao walio kufuru kwa kuhudhuria Siku iliyo kuu!
آية رقم 38
Watasikia na wataona vizuri vilioje Siku watakayo tufikia! Lakini madhaalimu sasa wamo katika upotofu ulio dhaahiri.
آية رقم 39
Na waonye siku ya majuto itapo katwa amri. Nao wamo katika ghafla, wala hawaamini.
آية رقم 40
Hakika Sisi tutairithi ardhi na walio juu yake. Na kwetu watarejeshwa.
آية رقم 41
Na mtaje katika Kitabu Ibrahim. Hakika yeye alikuwa mkweli, Nabii.
آية رقم 42
Alipo mwambia baba yake: Ewe baba yangu! Kwa nini unaabudu visivyo sikia, na visivyo ona, na visivyo kufaa chochote?
آية رقم 43
Ewe baba yangu! Kwa yakini imenifikia ilimu isiyo kufikia wewe. Basi nifuate mimi, nami nitakuongoza Njia Iliyo Sawa.
آية رقم 44
Ewe baba yangu! Usimuabudu Shet'ani. Hakika Shet'ani ni mwenye kumuasi Mwingi wa Rehema.
آية رقم 45
Ewe baba yangu! Hakika mimi naogopa isikupate adhabu inayo toka kwa Mwingi wa Rehema ukaja kuwa mwenziwe Shet'ani.
آية رقم 46
(Baba) akasema: Unaichukia miungu yangu, ewe Ibrahim? Kama huachi, basi lazima nitakupiga mawe. Na niondokelee mbali kwa muda!
آية رقم 47
(Ibrahim) akasema: Salamun a'laika! Amani iwe juu yako! Mimi nitakuombea msamaha kwa Mola wangu Mlezi. Hakika Yeye ananihurumia sana.
آية رقم 48
Nami najitenga nanyi na hayo mnayo yaabudu badala ya Mwenyezi Mungu. Na ninamwomba Mola wangu Mlezi; asaa nisiwe mwenye kukosa bahati kwa kumwomba Mola wangu Mlezi.
آية رقم 49
Basi alipo jitenga nao na yale waliyo kuwa wakiyaabudu badala ya Mwenyezi Mungu, tulimpa Is-haq na Yaaqub, na kila mmoja tukamfanya Nabii.
آية رقم 50
Na tukawapa rehema zetu na tukawajaalia kupewa sifa za kweli tukufu.
آية رقم 51
Na mtaje Musa katika Kitabu. Hakika yeye alikuwa ni mwenye kuchaguliwa, na alikuwa Mtume, Nabii.
آية رقم 52
Na tulimwita upande wa kulia wa mlima na tukamsogeza kunong'ona naye.
آية رقم 53
Nasi kwa rehema zetu tukampa nduguye, Harun, awe Nabii.
آية رقم 54
Na mtaje katika Kitabu Ismail. Bila ya shaka yeye alikuwa ni mkweli wa ahadi, na alikuwa Mtume, Nabii.
آية رقم 55
Na alikuwa akiwaamrisha watu wake Sala na Zaka, na alikuwa mbele ya Mola wake Mlezi mwenye kuridhiwa.
آية رقم 56
Na mtaje katika Kitabu Idris. Hakika yeye alikuwa ni mkweli Nabii.
آية رقم 57
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Na tulimuinua daraja ya juu.
آية رقم 58
Hao ndio alio waneemesha Mwenyezi Mungu miongoni mwa Manabii katika uzao wa Adam, na katika uzao wa wale tulio wapandisha pamoja na Nuhu, na katika uzao wa Ibrahim na Israil, na katika wale tulio waongoa na tukawateuwa. Wanapo somewa Aya za Mwingi wa Rehema huanguka kusujudu na kulia.
آية رقم 59
Lakini wakaja baada yao walio wabaya, wakaacha Sala, na wakafuata matamanio. Basi watakuja kuta malipo ya ubaya.
آية رقم 60
Isipo kuwa walio tubu, wakaamini, na wakatenda mema. Hao, basi, wataingia Peponi wala hawatadhulumiwa chochote.
آية رقم 61
Bustani za milele alizo waahidi Rahmani waja wake katika siri. Hakika ahadi yake hapana shaka itafika.
آية رقم 62
Humo hawatasikia upuuzi, ila Salama tu. Na watapata humo riziki zao asubuhi na jioni.
آية رقم 63
Hiyo ndiyo Pepo tutayo warithisha katika waja wetu walio kuwa wachamngu.
آية رقم 64
(Nao watasema:) Wala hatuteremki ila kwa amri ya Mola wako Mlezi. Ni yake Yeye yaliyoko mbele yetu na yaliyoko nyuma yetu, na yaliyomo katikati ya hayo. Na Mola wako Mlezi si mwenye kusahau.
آية رقم 65
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake. Basi muabudu Yeye tu, na udumu katika ibada yake. Je, mnamjua mwenye jina kama lake?
آية رقم 66
Na mwanaadamu husema: Hivyo, nitakapo kufa, ni kweli nitafufuliwa niwe hai tena?
آية رقم 67
Je! Hakumbuki mwanaadamu ya kwamba tulimuumba kabla, na hali hakuwa chochote?
آية رقم 68
Basi naapa kwa Mola wako Mlezi! Kwa yakini tutawakusanya wao pamoja na mashet'ani; kisha tutawahudhurisha kuizunguka Jahannamu, nao wamepiga magoti!
آية رقم 69
Kisha kwa yakini tutawatoa katika kila kundi wale miongoni mwao walio zidi kumuasi Arrahmani, Mwingi wa Rahema..
آية رقم 70
Tena hakika Sisi tunawajua vyema zaidi wanao stahiki kuunguzwa humo.
آية رقم 71
Wala hapana yeyote katika nyinyi ila ni mwenye kuifikia. Hiyo ni hukumu ya Mola wako Mlezi ambayo lazima itimizwe.
آية رقم 72
Kisha tutawaokoa wale walio mchamngu; na tutawaacha madhaalimu humo wamepiga magoti.
آية رقم 73
Na wanapo somewa Aya zetu zilizo wazi, walio kufuru huwaambia walio amini: Lipi katika makundi mawili lenye cheo kizuri na lilio bora barazani?
آية رقم 74
Na kaumu ngapi tuliziangamiza zilizo kuwa na mapambo mazuri zaidi na wazuri zaidi kwa kuwatazama!
آية رقم 75
Sema: Walio katika upotofu basi Arrahmani Mwingi wa Rahema atawapururia muda mpaka wayaone waliyo onywa - ama ni adhabu au ni Saa. Hapo ndipo watapo jua ni nani mwenye makao mabaya na mwenye askari dhaifu.
آية رقم 76
Na Mwenyezi Mungu huwazidishia uwongofu wenye kushika uwongofu. Na mema yenye kudumu ni bora katika malipo mbele ya Mola wako Mlezi na yana mwisho mwema.
آية رقم 77
Je, umemwona aliye zikanya Ishara zetu na akasema: Kwa hakika mimi nitapewa mali na wana!
آية رقم 78
Kwani yeye amepata khabari za ghaibu, au amechukua ahadi kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema?
آية رقم 79
Hasha! Tutaandika anayo yasema, tutamkunjulia muda wa adhabu.
آية رقم 80
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na tutamrithi hayo anayo yasema, na atatufikia mtupu peke yake!
آية رقم 81
Na wamechukua miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati iwape nguvu.
آية رقم 82
Sivyo kabisa! Wataikataa hiyo ibada yao, na watakuwa ndio dhidi yao.
آية رقم 83
Kwani huoni ya kwamba tumewatuma mashet'ani kwa makafiri wawachochee kwa uchochezi?
آية رقم 84
Basi usiwafanyie haraka. Sisi tunawahisabia idadi ya siku zao.
آية رقم 85
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Siku tutayo wakusanya wachamngu kuwapeleka kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni wageni wake.
آية رقم 86
ﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Na tukawachunga wakhalifu kuwapeleka Jahannamu hali ya kuwa wana kiu.
آية رقم 87
Hawatakuwa na mamlaka ya uombezi ila wale walio chukua ahadi kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema..
آية رقم 88
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Na wao ati husema kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana!
آية رقم 89
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Hakika mmeleta jambo la kuchusha mno!
آية رقم 90
Zinakaribia mbingu kutatuka kwa hilo, na ardhi kupasuka, na milima kuanguka vipande vipande.
آية رقم 91
ﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Kwa kudai kwao kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana.
آية رقم 92
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Wala hahitajii Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa na mwana.
آية رقم 93
Hapana yeyote aliomo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni mtumwa wake.
آية رقم 94
ﯺﯻﯼﯽ
ﯾ
Yeye hakika amewadhibiti na amewahisabu sawa sawa.
آية رقم 95
ﯿﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Na kila mmoja katika wao atamfikia Siku ya Kiyama peke yake.
آية رقم 96
Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi.
آية رقم 97
Na hakika tumeifanya nyepesi (Qur'ani) kwa ulimi wako, ili uwabashirie kwayo wachamngu, na uwaonye kwayo watu wabishi.
آية رقم 98
Na kaumu ngapi tumezihiliki kabla yao. Je! Unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao?
تقدم القراءة