ترجمة معاني سورة مريم باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation

Ali Muhsin Al - Swahili translation

آية رقم 1

Marya


Kaf Ha Ya A'yn S'ad
آية رقم 2

Huu ni Ukumbusho wa rehema ya Mola wako Mlezi kwa mja wake, Zakariya.

(Malaika) akasema: Hakika mimi ni mwenye kutumwa na Mola wako Mlezi ili nikubashirie tunu ya mwana aliye takasika.

Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
آية رقم 68

Basi naapa kwa Mola wako Mlezi! Kwa yakini tutawakusanya wao pamoja na mashet'ani; kisha tutawahudhurisha kuizunguka Jahannamu, nao wamepiga magoti!
آية رقم 78

Kwani yeye amepata khabari za ghaibu, au amechukua ahadi kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema?
آية رقم 80

Na tutamrithi hayo anayo yasema, na atatufikia mtupu peke yake!
آية رقم 85

Siku tutayo wakusanya wachamngu kuwapeleka kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni wageni wake.
آية رقم 86

Na tukawachunga wakhalifu kuwapeleka Jahannamu hali ya kuwa wana kiu.
آية رقم 88

Na wao ati husema kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana!
آية رقم 91

Kwa kudai kwao kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana.
آية رقم 94

Yeye hakika amewadhibiti na amewahisabu sawa sawa.
تقدم القراءة