ترجمة معاني سورة الرعد باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
الترجمة الإنجليزية - صحيح انترناشونال
المنتدى الإسلامي
الترجمة الإنجليزية
الترجمة الفرنسية - المنتدى الإسلامي
نبيل رضوان
الترجمة الإسبانية
محمد عيسى غارسيا
الترجمة الإسبانية - المنتدى الإسلامي
الترجمة الإسبانية (أمريكا اللاتينية) - المنتدى الإسلامي
المنتدى الإسلامي
الترجمة البرتغالية
حلمي نصر
الترجمة الألمانية - بوبنهايم
عبد الله الصامت
الترجمة الألمانية - أبو رضا
أبو رضا محمد بن أحمد بن رسول
الترجمة الإيطالية
عثمان الشريف
الترجمة التركية - مركز رواد الترجمة
فريق مركز رواد الترجمة بالتعاون مع موقع دار الإسلام
الترجمة التركية - شعبان بريتش
شعبان بريتش
الترجمة التركية - مجمع الملك فهد
مجموعة من العلماء
الترجمة الإندونيسية - شركة سابق
شركة سابق
الترجمة الإندونيسية - المجمع
وزارة الشؤون الإسلامية الأندونيسية
الترجمة الإندونيسية - وزارة الشؤون الإسلامية
وزارة الشؤون الإسلامية الأندونيسية
الترجمة الفلبينية (تجالوج)
مركز رواد الترجمة بالتعاون مع موقع دار الإسلام
الترجمة الفارسية - دار الإسلام
فريق عمل اللغة الفارسية بموقع دار الإسلام
الترجمة الفارسية - حسين تاجي
حسين تاجي كله داري
الترجمة الأردية
محمد إبراهيم جوناكري
الترجمة البنغالية
أبو بكر محمد زكريا
الترجمة الكردية
حمد صالح باموكي
الترجمة البشتوية
زكريا عبد السلام
الترجمة البوسنية - كوركت
بسيم كوركورت
الترجمة البوسنية - ميهانوفيتش
محمد مهانوفيتش
الترجمة الألبانية
حسن ناهي
الترجمة الأوكرانية
ميخائيلو يعقوبوفيتش
الترجمة الصينية
محمد مكين الصيني
الترجمة الأويغورية
محمد صالح
الترجمة اليابانية
روايتشي ميتا
الترجمة الكورية
حامد تشوي
الترجمة الفيتنامية
حسن عبد الكريم
الترجمة الكازاخية - مجمع الملك فهد
خليفة الطاي
الترجمة الكازاخية - جمعية خليفة ألطاي
جمعية خليفة الطاي الخيرية
الترجمة الأوزبكية - علاء الدين منصور
علاء الدين منصور
الترجمة الأوزبكية - محمد صادق
محمد صادق محمد
الترجمة الأذرية
علي خان موساييف
الترجمة الطاجيكية - عارفي
فريق متخصص مكلف من مركز رواد الترجمة بالشراكة مع موقع دار الإسلام
الترجمة الطاجيكية
خوجه ميروف خوجه مير
الترجمة الهندية
مولانا عزيز الحق العمري
الترجمة المليبارية
عبد الحميد حيدر المدني
الترجمة الغوجراتية
رابيلا العُمري
الترجمة الماراتية
محمد شفيع أنصاري
الترجمة التلجوية
مولانا عبد الرحيم بن محمد
الترجمة التاميلية
عبد الحميد الباقوي
الترجمة السنهالية
فريق مركز رواد الترجمة بالتعاون مع موقع دار الإسلام
الترجمة الأسامية
رفيق الإسلام حبيب الرحمن
الترجمة الخميرية
جمعية تطوير المجتمع الاسلامي الكمبودي
الترجمة النيبالية
جمعية أهل الحديث المركزية
الترجمة التايلاندية
مجموعة من جمعية خريجي الجامعات والمعاهد بتايلاند
الترجمة الصومالية
محمد أحمد عبدي
الترجمة الهوساوية
الترجمة الأمهرية
محمد صادق
الترجمة اليورباوية
أبو رحيمة ميكائيل أيكوييني
الترجمة الأورومية
الترجمة التركية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الفرنسية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الإندونيسية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الفيتنامية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة البوسنية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الإيطالية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الفلبينية (تجالوج) للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
الترجمة الفارسية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
مركز تفسير للدراسات القرآنية
Dr. Ghali - English translation
Muhsin Khan - English translation
Pickthall - English translation
Yusuf Ali - English translation
Azerbaijani - Azerbaijani translation
Sadiq and Sani - Amharic translation
Farsi - Persian translation
Finnish - Finnish translation
Muhammad Hamidullah - French translation
Korean - Korean translation
Maranao - Maranao translation
Abdul Hameed and Kunhi Mohammed - Malayalam translation
Salomo Keyzer - Flemish (Dutch) translation
Norwegian - Norwegian translation
Samir El - Portuguese translation
Polish - Polish translation
Romanian - Romanian translation
Elmir Kuliev - Russian translation
Albanian - Albanian translation
Tatar - Tatar translation
Japanese - Japanese translation
محمد جوناگڑھی - Urdu translation
Ma Jian - Chinese translation
Turkish - Turkish translation
King Fahad Quran Complex - Thai translation
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Abdullah Muhammad Basmeih - Malay translation
Hamza Roberto Piccardo - Italian translation
Indonesian - Indonesian translation
Bubenheim & Elyas - German / Deutsch translation
Bosnian - Bosnian translation
Hasan Efendi Nahi - Albanian translation
Sherif Ahmeti - Albanian translation
Sahih International - English translation
Czech - Czech translation
Abul Ala Maududi(With tafsir) - English translation
Tajik - Tajik translation
Alikhan Musayev - Azerbaijani translation
Muhammad Saleh - Uighur; Uyghur translation
Abdul Haleem - English translation
Mufti Taqi Usmani - English translation
Muhammad Karakunnu and Vanidas Elayavoor - Malayalam translation
Sheikh Isa Garcia - Spanish; Castilian translation
Divehi - Divehi; Dhivehi; Maldivian translation
Abubakar Mahmoud Gumi - Hausa translation
Mahmud Muhammad Abduh - Somali translation
Knut Bernström - Swedish translation
Jan Trust Foundation - Tamil translation
Mykhaylo Yakubovych - Ukrainian translation
Uzbek - Uzbek translation
Diyanet Isleri - Turkish translation
Ministry of Awqaf, Egypt - Russian translation
Abu Adel - Russian translation
Burhan Muhammad - Kurdish translation
Dr. Mustafa Khattab, The Clear Quran - English translation
Dr. Mustafa Khattab - English translation
الترجمة الإنجليزية - مركز رواد الترجمة
الترجمة الفرنسية - محمد حميد الله
الترجمة البوسنية - مركز رواد الترجمة
الترجمة الصربية - مركز رواد الترجمة - جار العمل عليها
الترجمة الألبانية - مركز رواد الترجمة - جار العمل عليها
الترجمة اليابانية - سعيد ساتو
الترجمة التاميلية - عمر شريف
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
الترجمة اللوغندية - المؤسسة الإفريقية للتنمية
الترجمة الإنكو بامبارا - ديان محمد
الترجمة العبرية
الترجمة الإنجليزية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
الترجمة الروسية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
الترجمة البنغالية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
الترجمة الصينية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
الترجمة اليابانية للمختصر في تفسير القرآن الكريم
ترجمة معاني القرآن الكريم - عادل صلاحي
عادل صلاحي
ﰡ
آية رقم 1
Alif, Lām, Mīm. Maelezo kuhusu herufi ziliokatwa na kutengwa yametangulia mwanzo wa sura ya Al-Baqarah. Hizi ni aya za Qur’ani zenye cheo kitukufu. Na Qur’ani hii uliyoteremshiwa, ewe Mtume, ndiyo haki, na sivyo kama vile wanavyosema washirikina kwamba wewe mwenyewe ndio uliyoileta. Pamoja na hili, wengi wa watu hawaiamini wala hawaifuati kivitendo.
آية رقم 2
Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Ndiye Aliyeziinua mbingu saba kwa uweza Wake bila ya nguzo, kama vile ambavyo mnaziona, kisha akalingana - yaani akawa juu - ya Arshi kulingana kunakonasibiana na utukufu Wake na ukubwa Wake, na Akalidhalilisha jua na mwezi kwa manufaa ya waja, kila moja wapo ya viwili hivyo kinazunguka kwenye anga lake mpaka Siku ya Kiyama. Anapekesha, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, mambo ya ulimwenguni na Akhera, Anawafafanulia dalili zenye kuonyesha uweza Wake na kwamba yeye hakuna mungu isipokuwa Yeye, ili muwe na Imani ya kikweli kwa Mwenyezi Mungu na mjiyakinishe kurudi Kwake, mpate kuamini ahadi Yake ya thawabu na adhabu na mumtakasiye ibada Peke Yake.
آية رقم 3
Na Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Ambaye Aliifanya ardhi iwe kunjufu iliyonyoshwa, Akaitayarisha kwa maisha yenu, Akayaweka humo majabali yenye kuithibitisha na mito ya nyinyi kunywa na kunufaika, Akaweka humo aina mbili za kila matunda, katika hayo kukawa kuna meupe na meusi, tamu na kali, na Akaufanya usiku ufinike mchana kwa giza lake. Hakika katika hayo yote pana mazingatio kwa wenye kuyafikiri wakawaidhika.
آية رقم 4
Na kwenye ardhi kuna sehemu zinaopakana, kati ya hizo kuna zilizo nzuri zenye kuota mimea inayowafaa watu na kati ya hizo kuna kavu zenye chumvi zisizootesha chochote. Na katika ardhi nzuri kuna mashamba ya zabibu, na Amejaalia humo aina tafauti za makulima na mitende iliyokusanyika mahali pamoja na isiyokusanyika hapo, vyote hivyo viko katika mchanga mmoja na vinakunywa maji mamoja, isipokuwa vinatafautiana katika matunda, ukubwa, utamu na mengineyo: hili ni tamu na hili ni kali, na mengine ni bora kuliko mengine katika kula. Katika hilo kuna dalili kwa mwenye moyo unaoyaelewa maamrisho ya Mwenyezi Mungu na makatazo Yake.
آية رقم 5
Ukiona ajabu , ewe Mtume, ya makafiri kutoamini baada ya dalili hizi, basi ajabu kubwa zaidi ni kusema kwao, «Je, tukifa na tukawa mchanga tutafufuliwa upya?» Hao ndio wenye kumkanusha Mola wao Aliyewafanya waweko kutoka kwenye hali ya kutokuwako. Na hao kutakuwa na minyororo kwenye shingo zao Siku ya Kiyama. Na hao wataingia Motoni na hawatatoka kabisa.
آية رقم 6
Na wale wakanushaji wanakuharakisha uwaletee adhabu ambayo mimi sikuwaharakishia kabla ya kuamini Imani ambayo kwayo kunatarajiwa usalama na matendo mema. Na yashapita mateso ya wakanushaji kabla yao, kwa nini wao hawawi ni wenye kuwaidhika na wao? Hakika Mola wako ni Mwenye msamaha wa dhambi za watu waliotubia dhambi zao juu ya udhalimu wao, Atawafungulia mlango wa msamaha na Atawaita waingie, na huku wao wanazidhulumu nafsi zao kwa kumuasi Mola wao. Hakika Mola Wako ni Mkali wa mateso juu ya walioendelea kwenye ukafiri, upotevu na kumuasi Mwenyezi Mungu.
آية رقم 7
Na makafiri wa Makkah wanasema, «Basi si ajiwe na miujiza inayoonekana kama fimbo ya Mūsā na ngamia wa Ṣāliḥ.» Na hilo haliko kwenye mkono wako, ewe Mtume; hukuwa wewe isipokuwa ni mwenye kuwafikishia na ni mwenye kuwatisha adhabu ya Mwenyezi Mungu. Na kila ummah una mjumbe wa kuwaongoza kwenye njia ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka.
آية رقم 8
Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Anakijua alichokibeba kila mwanamke ndani ya tumbo lake: ni cha kiume au ni cha kike, ni chema au ni kibaya. Na anakijua kile ambacho zao zinakipunguza kikazaliwa kimekufa au kabla ya kutimia myezi tisa au kikapita muda huo. Na kila kitu, chenye kuzidi au kupungua, kimekadiriwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa kipimo kisichopitisha kiasi.
آية رقم 9
ﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyofichika na macho na yanayoonekana, Aliye Mkubwa wa dhati, majina na sifa , Aliye juu ya viumbe Vyake vyote kwa dhati Yake, uweza Wake na kutendesha nguvu Kwake.
آية رقم 10
Analingana, katika ujuzi Wake Aliyetukuka, yule anayesirisha maneno, katika nyinyi, na anayedhihirisha. Na analingana Kwake yule anayefanya matendo yake kwa siri ndani ya giza la usiku na yule mwenye kuyafanya waziwazi kwenye mwangaza wa mchana.
آية رقم 11
Na Mwenyezi Mungu Anayetukuka Ana Malaika wanaompitia binadamu, kundi baada ya kundi, mbele yake na nyuma yake, wanamhifadhi kwa amri ya Mwenyezi Mungu na kuyadhibiti yanayofanywa na yeye, mema au maovu. Hakika Mwenyezi Mungu , Aliyetakata na kutukuka, Hageuzi neema aliyowaneemesha watu mpaka wakiwa wao watayageuza yale waliyoamrishwa na Mola wao na wakamuasi. Na Mwenyezi Mungu Akiwatakia watu mitihani basi hakuna namna ya kuyakimbia, na hawana wao asiyekuwa Mwenyezi Mungu msimamizi yoyote wa kuyasimamia mambo yao, akawaletea yanayopendwa na akawakinga na yanayochukiwa.
آية رقم 12
Yeye Ndiye Ambaye anawaonesha umeme, nao ni mwangaza unaong’aa kutoka ndani ya mawingu, mkawa mnaogopa msishukiwe na vimondo venye kuchoma kutokana na umeme huo, na pia mkawa mnatazamia mvua inyeshe. Na kwa uweza Wake, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, anayleta mawingu yanayobebeshwa maji mengi kwa ajili ya manufaa yenu.
آية رقم 13
Na radi linamtakasia Mwenyezi Mungu sifa Zake njema, matakaso yanayoonyesha dalili kwamba linamnyenyekea Mola Wake. Na Malaika wanamwepusha Mola wao na kila la upungufu kwa kumuogopa kwao Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu Anatuma vimondo vyenye kuangamiza, Akawaangamiza kwavyo anaowataka kati ya viumbe vyake. Na makafiri wanabisha juu ya upweke wa Mwenyezi Mungu na uweza Wake kufufufua, na hali Yeye Ana uweza mwingi na nguvu na ujabari wa kuwatesa waliomuasi.
آية رقم 14
Ni wa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Peke Yake, ulinganizi wa tawhīd «Hapana mola isipokuwa Mwenyezi Mungu.» Haabudiwi wala haombwi isipokuwa Yeye. Na waungu ambao wao wanawaabudu badala ya Mwenyezi Mungu hawaitiki maombi ya mwenye kuwaomba. Na hali yao pamoja na hao waungu ni kama hali ya mwenye kiu anayenyosha vitanga vyake viwili vya mkono kwenye maji kutoka mbali ili yafike kwenye kinywa chake, yakawa hayafiki. Na maombi ya makafiri kwa hao waungu hayakuwa isipokuwa yako mbali na usawa, kwa kuwa wao wanamshirikisha wengine pamoja na Mwenyezi Mungu.
آية رقم 15
Na Mwenyezi Mungu Peke Yake wanamsujudia, wakinyenyekea na kufuata, walioko mbinguni na ardhini wote, Waumini wanamsujudia na kumnyenyekea kwa ridhaa na hiari, na makafiri wanamnyenyekea kwa nguvu, kwa kuwa wao wanafanya kiburi kumuabudu na hali yao na maumbile yao yanawakanusha juu ya hilo. Na vivuli vya viumbe vinafuata utukufu wa Mwenyezi Mungu, vinatembea kulingana na matakwa Yake mwanzo wa mchana na mwisho wake.
آية رقم 16
Waambie washirikina, ewe Mtume, «Ni nani muumba mbingu na ardhi na mwenye kuziendesha?» Sema, «Mwenyezi Mungu Ndiye Muuumba Mwenye kuziendesha. Na nyinyi mnalikubali hilo.» Kisha waambie ukiwalazimisha hoja, «Je, mnawafanya wasiokuwa Yeye ni waabudiwa wenu, na hali ya kuwa wao hawawezi kuzinufaisha nafsi zao au kuzidhuru, wacha kule kuwanufaisha nyinyi au kuwadhuru, na mkaacha kumuabudu mwenye kuwamiliki wao?» Waambie, «Kwani analingana kwenu nyinyi kafiri, ambaye ni kama kipofu, na Muumini, ambaye ni kama anayeona? Au kwani unalingana kwenu nyinyi ukafiri, ambao ni kama giza, na Imani, ambayo ni kama mwangaza? Au ni kwamba wale wasimamizi wao wanaowafanya ni washirika wa Mwenyezi Mungu wanaumba kama Anavyoumba, vikawatatiza viumbe vya washirika na viumbe vya Mwenyezi Mungu, ndipo wakaitakidi kwamba wao wanastahiki kuabudiwa?» Waambie, ewe Mtume, «Mwenyezi Mungu Aliyetukuka ni Muumba kila kilichoko ambacho hakikuwako; Yeye Ndiye Anayestahiki kuabudiwa Peke Yake na Yeye Ndiye Aliye mmoja Mwenye kutendesha nguvu Anayestahiki uungu na ibada, na sio masanamu na mizimu isiyodhuru wala kunufaisha.»
آية رقم 17
Kisha Mwenyezi Mungu Akapiga mfano wa ukweli na urongo kuwa ni kama maji Aliyoyateremsha kutoka juu, yakapita kwenye mabonde ya ardhi kwa kadiri ya udogo wake na ukubwa wake, mikondo ya maji ikabeba povu likiwa juu yake lisilo na faida. Na akapiga mfano mwingine wa madini ambayo watu huyachoma moto ili kuyayeyusha kutaka kutengeneza pambo, kama vile dhahabu na fedha, au kutaka manufaa ya kujinufaisha, kama vile shaba, ukatoka uchafu wake usio na faida kama ule uliokuwa pamoja na maji. Kwa mfano huu, Mwenyezi Mungu Apigia mfano ukweli na urongo. Urongo ni kama povu la maji, linapotea au linatupwa kwa kuwa halina faida, na ukweli ni kama maji safi na madini yaliyotakasika, yanasalia kwenye ardhi kwa kunufaika nayo. Kama Alivyowafafanulia nyinyi mifano hii, hivyo ndivyo Anavyoipiga kwa watu upate kufunuka wazi ukweli ujitenge na urongo, na uongofu ujitenge na upotevu.
آية رقم 18
Pepo ni ya wenye kuamini ambao wanamtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na Moto ni wa wale ambao hawakumtii na wakamkanusha. Na lau walikuwa wanamiliki kila kilichoko ardhini na zaidi ya kama hiko pamoja nacho, wangalikitoa kwa kujikomboa nafsi zao na adhabu ya Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama, na hakingalikubaliwa kutoka kwao. Wao watafanyiwa hesabu kwa kila tendo baya walilolitenda. Na makazi yao ya kukaa ni Jahanamu, itakuwa ni tandiko kwao. Na tandiko baya mno ni hilo walilojitayarishia nafsi zao.
آية رقم 19
Je, yule anayejua kwamba kile ulichokuja nacho, ewe Mtume, ndicho ukweli unaotoka kwa Mwenyezi Mungu na akauamini ni kama kipofu asiyeuona ukweli ambaye hakuamini? Hakika wanaowaidhika ni wenye akili timamu
آية رقم 20
ambao wanatekeleza ahadi ya Mwenyezi Mungu Ambayo Aliwaamrisha kwayo na wasiitangue ahadi ya mkazo ambayo walimuahidi nayo Mwenyezi Mungu.
آية رقم 21
Nao ndio ambao wanawaunga wale ambao Mwenyezi Mungu Amewaamrisha wawaunge kama jamaa wa karibu na wahitaji, wanamtunza Mola wao na wanaogopa Asiwahesabu kwa madhambi yao yote na Asiwasamehe chochote katika hayo.
آية رقم 22
Nao ndio ambao walivumilia udhia na kusimama juu ya utiifu na kujiepusha na uasi kwa kutafuta radhi za Mola wao, walitekeleza Swala kwa namna iliyotimia zaidi, walitekeleza Zaka za lazima za mali yao na matumizi yanayopendekezwa kwa siri na kwa dhahiri na wakawa wanaondoa baya kwa zuri lenye kulifuta. Hao wanaosifika kwa sifa hizi watakuwa na mwisho wenye kusifiwa huko Akhera.
آية رقم 23
Mwisho wao ni mabustani ya Pepo ya 'Adn, watakaa humo, hawataondoka kutoka humo, na pamoja nao watakuwamo waliokuwa wema miongoni mwa mababa, wake na watoto waume kwa wake, na huku malaika waingia kwao kutoka kila mlango wakipongeza na kuingia Peponi.
آية رقم 24
Malaika watawaambia, «Amani iwashukie, yakiwa ni maamkizi yenu peke yenu, na msalimike na kila baya kwa uvumilivu wenu katika kumtii Mwenyezi Mungu. Neema ya nyumba ya mwisho ni Pepo.»
آية رقم 25
Ama waovu, wamesifiwa kwa sifa kinyume na zile za Waumini. Wao ni wale ambao hawatekelezi ahadi za Mwenyezi Mungu kwa kumpwekesha, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, kwa ibada baada ya kujitukulia ahadi ya mkazo. Na wao ni wale wanaokata kile ambacho Mwenyezi Mungu amewaamrisha kukiunga kama vile kukata zao na mengineyo na wanafanya uharibifu katika ardhi kwa kufanya maasia. Hao waliosifiwa kwa sifa hizi mbaya watakalolipata ni kufukuzwa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu na watakuwa na mambo ambayo ni mabaya kwao ya adhabu kali katika Nyumba ya Akhera.
آية رقم 26
Mwenyezi Mungu Peke Yake Anamkunjulia riziki Anayemtaka miongoni mwa waja Wake na Anambania Anayemtaka kati yao. Na makafiri waliufurahia ukunjufu duniani. Na dunia hii haikuwa ikilinganishwa na Akhera isipokuwa ni kitu kidogo cha kustarehe nacho, na kwa haraka sana kinaondoka.
آية رقم 27
Na makafiri wanasema kwa kushindana, «Si ateremshiwe Muhammad miujiza inayoonekena kama miujiza ya Mūsā na 'Īsā. Waambie kwamba Mwenyezi Mungu Anampoteza Anayemtaka miongoni mwa washindani wasiotaka uongofu na haimfai miujiza na Anawaongoza kwenye dini Yake ya haki anayerejea Kwake na kutaka radhi Zake.
آية رقم 28
Na Anawaongoza wale ambao nyoyo zao zimetulia kwa kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kumtaja zikapata utulivu. Jua utanabahi kwamba kumtii Mwenyezi Mungu, kumtaja na malipo mema kutoka Kwake yanafanya nyoyo zitulie na zipumbae.
آية رقم 29
Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya matendo mema watakuwa na furaha, kipumbazi cha jicho, hali nzuri na marejeo mema kwenye Pepo ya Mwenyezi Mungu na radhi Zake.
آية رقم 30
Kama tulivyowatuma Mitume kabla yako, tulikutuma, ewe Mtume, katika ummah waliopita kabla yao ummah wa Mitume, ili uwasomee ummah huu Qur’ani iliyoteremshwa kwako, na hali ya watu wako ni kuukanusha upweke wa Mwingi wa rehema. Waambie, ewe Mtume, «Mwingi wa rehema Ambaye hamkumpwekesha na mkamfanya ni Mola mmoja Ndiye Mola wangu, Peke Yake; hakuna mwenye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Yeye. Kwake Yeye nimetegemea na nina imani, na Kwake Yeye ndio marejeo yangu na makimbilio yangu.
Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anawarudi makafiri ambao walitaka kwamba Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ateremshiwe miujiza yenye kuonekana, kwakuwaambia, «Lau kulikuwa na Qur’ani itakayosomwa ikafanya majabali yaondoke mahali pake au ardhi ipasuke itoe mito au wafu wafufuke na waseme, kama walivyotaka kwako, hii Qur’ani ingalikuwa ndiyo yenye kusifika na hayo na si kitu kingine, na pia hawangaliamini.. Bali ni ya Mwenyezi Mungu amri juu ya miujiza na mengineyo. Kwani hawakujua Waumini kwamba lau Mwenyezi Mungu Anataka, watu wote wa ardhini wangaliamini bila ya miujiza? Na hawataacha makafiri kuendelea kuteremkiwa na mkasa kwa sababu ya ukafiri wao, kama kuuawa na kutekwa katika vita vya Waislamu, au kuteremkiwa na mkasa huo karibu na nyumba zao, mpaka ahadi ya Mwenyezi Mungu ije ya kuwapa ushindi juu yao. Hakika Mwenyezi Mungu Haendi kinyume na ahadi Yake.
آية رقم 32
Na iwapo wameufanyia shere ulinganizi wako, ewe Mtume, basi kuna ummah kabla yako waliwafanyia shere Mitume wao. Basi usiwe na masikitiko, niliwapa muhula wale waliokufuru kisha nikawapatiliza kwa mateso yangu; na yalikuwa ni mateso makali.
آية رقم 33
Je, Yule Anayesimamia kila nafsi Akiyadhibiti yale inayoyafanya, ni mwenye haki zaidi ya kuabudiwa au ni hivi viumbe visivyojiweza? Na wao, kwa ujinga wao walimfanyia Mwenyezi Mungu washirika miongoni mwa viumbe Wake wakawa wanawaabudu. Waambie, ewe Mtume, «Tajeni majina yao na sifa zao.» Na hawatapata kwenye sifa zao chochote cha kuwafanya wao wastahiki kuabudiwa. Au nyinyi mnampasha habari Mwenyezi Mungu kuwa Ana washirika katika ardhi Yake ambao Hawajui? Au mnawaita ni washirika kimaneno tu bila ya kuwa na hakika? Bali Shetani aliwapambia makafiri neno lao la ubatilifu na akawazuia njia ya Mwenyezi Mungu. Na yule ambaye Mwenyezi Mungu Hakumwafikia kuongoka basi hakuna yoyote mwenye kumuongoza na kumwafikia kwenye haki na uongofu.
آية رقم 34
Makafiri hawa wenye kuzuia njia ya Mwenyezi Mungu watakuwa na adhabu ngumu katika maisha ya ulimwenguni kwa kuuawa, kutekwa na kuhiziwa. Na kwa hakika, adhabu yao huko Akhera ni nzito zaidi na ni kali zaidi, na hawatakuwa na kizuizi chenye kuwazuia wasipate adhabu ya Mwenyezi mungu.
آية رقم 35
Sifa ya Pepo ambayo Mwenyezi Mungu Amewaahidi nayo wale wanaomuogopa na kwamba mito inapita chini ya miti yake na majumba yake ya fahari, Matunda yake hayamaliziki na kivuli chake hakiondoki. Malipo mema hayo ya Pepo ndio mwisho wa waliomuogopa Mwenyezi Mungu wakajiepusha na mambo ya kumuasi na wakatekeleza faradhi Zake. Na mwisho wa makafiri ni Moto.
آية رقم 36
Na wale ambao tuliwapa Kitabu, miongoni mwa Mayahudi na Wanaswara, yoyote kati yao mwenye kukuamini, kama 'Abdullāh bin Salām na Najashi, wanaifurahia Qur’ani uliyoteremshiwa kwa kuwa inaenda sambamba na kile walichonacho. Na miongoni mwa wale wanaojiweka pamoja kukupinga, kama Sayyid na 'Aqib: maaskofu wawili wa Najran , na Ka'b bin al-Ashraf, wanaokanusha baadhi ya yale uliyoteremshiwa. Waambie, «Mwenyezi Mungu Ameniamrisha nimuabudu Yeye Peke Yake na nisimshirikishe chochote. Nawaita watu wamuabudu, na Kwake Peke Yake ndio marejeo yangu na marudio.
آية رقم 37
Na kama tulivyowateremshia Mitume Vitabu kwa lugha zao, tulikuteremshia wewe, ewe Mtume, Qur’ani kwa lugha ya Kiarabu, ili uitumie katika kuhukumu. Na lau ulifuata mapendeleo ya washirikina katika kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu, baada ya haki iliyokujia kutoka kwa Mwenyezi Mungu, hutakuwa na msaidizi yoyote mwenye kukuhami na kuzuia adhabu ya Mwenyezi Mungu isikufikie.
آية رقم 38
Na kumbuka waliposema, «Una nini, ewe Mtume, unaoa wanawake?» Hakika tulituma kabla yako Mitume kati ya wanadamu na kuwafanya wawe na wake na watoto. Na pia utaje waliposema, «Lau alikuwa ni Mtume angalituletea miujiza tuliyoitaka.» Haiko kwenye uwezo wa Mtume yoyote, kuleta miujiza ambayo watu wake waliitaka isipokuwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Kila jambo alilolihukumu Mwenyezi Mungu lina maandishi na wakati, Mwenyezi Mungu Ameliandika hapo Kwake, halitangulii wala halichelewi.
آية رقم 39
Mwenyezi Mungu Anakifuta Akitakacho miongoni mwa hukumu na mengineyo, na Anakiacha kisalie Akitakacho miongoni mwa hizo kwa hekima fulani Anayoijua. Na Kwake kuna asili ya Kitabu, nacho ni Al-Lawh„ Al-Mah,fūd,: Ubao uliohifadhiwa ambao yamethibitishwa ndani yake kimaandishi hali za viumbe mpaka Siku ya Kiyama.
آية رقم 40
Na tukikuonesha , ewe Mtume, baadhi ya mateso tuliyowaahidi maadui zako ya kuhizika na kuungulika ulimwenguni, basi hayo ni yale tuliyowaharakishia. Na tukikufisha kabla hujaona hayo, basi wajibu wako haukuwa isipokuwa ni kutekeleza ulinganizi, na hesabu na malipo ni juu yetu.
آية رقم 41
Kwani hawaoni hawa makafiri kwamba sisi tunaijia ardhi na kuipunguza pambizoni mwake kwa kuwapa Waislamu ushindi wa kuiteka miji ya makafiri na kuishikanisha na miji ya Kiislamu? Na Mwenyezi Mungu Anaamua, hakuna Mwenye kuurudi uamuzi Wake na hukumu Yake. Na Yeye ni Mpesi wa kuhesabu, basi wasifanye haraka ya kutaka kuletewa adhabu, kwani kila lenye kuja liko karibu.
آية رقم 42
Hakika wale waliokuwa kabla yao waliwapangia njama Mitume wao, kama vile hawa walivyokufanyia. Basi vitimbi vyote vina Mwenyezi Mungu, Anatangua vitimbi vyao na kuwarudishia wenyewe wapite patupu na wajute. Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu Kwake, Anakijua kile ambacho kila mtu anakichuma, chema au kibaya, na atalipwa kwa hicho. Na watajuwa makafiri, watakapofika kwa Mola wao, ni nanani atakuwa na mwisho mwema baada ya dunia hii. Huo ni wa wafuasi wa Mitume. Katika haya kuna onyo na tishio kwa makafiri.
آية رقم 43
Na wenye kumkanusha Nabii wa Mwenyezi Mungu wanasema, «Ewe Muhammad, hukutumilizwa na Mwenyezi Mungu.» Waambie, «Inatosha kuwa Mwenyezi Mungu ni shahidi juu ya ukweli wangu na urongo wenu, na unatosha ushahidi wa wenye ujuzi wa Kitabu miongoni mwa Mayahudi na Wanaswara kati ya wale waliouamini utume wangu na kwamba yale niliokuja nayo yanatoka kwa Mwenyezi Mungu na akaufuata ukweli na akatoa ushahidi huo waziwazi na asiufiche.
تقدم القراءة