ترجمة معاني سورة الإنشقاق باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Al-Inshikak
Itapo chanika mbingu,
آية رقم 2
ﭧﭨﭩ
ﭪ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
آية رقم 3
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Na ardhi itakapo tanuliwa,
آية رقم 4
ﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
آية رقم 5
ﭴﭵﭶ
ﭷ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
آية رقم 6
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
آية رقم 7
ﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
آية رقم 8
ﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
آية رقم 9
ﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Na arudi kwa ahali zake na furaha.
آية رقم 10
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
آية رقم 11
ﮘﮙﮚ
ﮛ
Basi huyo ataomba kuteketea.
آية رقم 12
ﮜﮝ
ﮞ
Na ataingia Motoni.
آية رقم 13
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
آية رقم 14
ﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
آية رقم 15
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
آية رقم 16
ﯔﯕﯖ
ﯗ
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
آية رقم 17
ﯘﯙﯚ
ﯛ
Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
آية رقم 18
ﯜﯝﯞ
ﯟ
Na kwa mwezi unapo pevuka,
آية رقم 19
ﯠﯡﯢﯣ
ﯤ
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
آية رقم 20
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Basi wana nini hawaamini?
آية رقم 21
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
آية رقم 22
ﯲﯳﯴﯵ
ﯶ
Bali walio kufuru wanakanusha tu.
آية رقم 23
ﯷﯸﯹﯺ
ﯻ
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
آية رقم 24
ﯼﯽﯾ
ﯿ
Basi wabashirie adhabu chungu!
آية رقم 25
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.
تقدم القراءة