ترجمة معاني سورة القيامة باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Al-Kiyama
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
آية رقم 2
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
آية رقم 3
ﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
آية رقم 4
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
آية رقم 5
ﮡﮢﮣﮤﮥ
ﮦ
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
آية رقم 6
ﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
آية رقم 7
ﮬﮭﮮ
ﮯ
Basi jicho litapo dawaa,
آية رقم 8
ﮰﮱ
ﯓ
Na mwezi utapo patwa,
آية رقم 9
ﯔﯕﯖ
ﯗ
Na likakusanywa jua na mwezi,
آية رقم 10
ﯘﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
آية رقم 11
ﯞﯟﯠ
ﯡ
La! Hapana pa kukimbilia!
آية رقم 12
ﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
آية رقم 13
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
آية رقم 14
ﯮﯯﯰﯱﯲ
ﯳ
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
آية رقم 15
ﯴﯵﯶ
ﯷ
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
آية رقم 16
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
ﯾ
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
آية رقم 17
ﯿﰀﰁﰂ
ﰃ
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
آية رقم 18
ﰄﰅﰆﰇ
ﰈ
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
آية رقم 19
ﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
آية رقم 20
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
آية رقم 21
ﭖﭗ
ﭘ
Na mnaacha maisha ya Akhera.
آية رقم 22
ﭙﭚﭛ
ﭜ
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
آية رقم 23
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
آية رقم 24
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
آية رقم 25
ﭥﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
آية رقم 26
ﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
آية رقم 27
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
آية رقم 28
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
آية رقم 29
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
آية رقم 30
ﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
آية رقم 31
ﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
آية رقم 32
ﮇﮈﮉ
ﮊ
Bali alikanusha, na akageuka.
آية رقم 33
ﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
آية رقم 34
ﮑﮒﮓ
ﮔ
Ole wako, ole wako!
آية رقم 35
ﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Kisha Ole wako, ole wako!
آية رقم 36
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
آية رقم 37
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
ﮦ
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
آية رقم 38
ﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
آية رقم 39
ﮭﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
آية رقم 40
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
تقدم القراءة