ترجمة معاني سورة يس باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭬ
ﭭ
Yasin
Ya-Sin (Y. S.).
آية رقم 2
ﭮﭯ
ﭰ
Kwa Haki ya Qur'ani yenye hikima!
آية رقم 3
ﭱﭲﭳ
ﭴ
Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,
آية رقم 4
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Juu ya Njia Iliyo Nyooka.
آية رقم 5
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
آية رقم 6
Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi wao wamekuwa wenye kughafilika.
آية رقم 7
Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.
آية رقم 8
Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.
آية رقم 9
Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.
آية رقم 10
Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.
آية رقم 11
Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.
آية رقم 12
Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha.
آية رقم 13
Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.
آية رقم 14
Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.
آية رقم 15
Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.
آية رقم 16
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
ﭼ
Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu.
آية رقم 17
ﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.
آية رقم 18
Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu.
آية رقم 19
Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka.
آية رقم 20
Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa.
آية رقم 21
Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.
آية رقم 22
NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?
آية رقم 23
Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.
آية رقم 24
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.
آية رقم 25
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!
آية رقم 26
Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua
آية رقم 27
Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa.
آية رقم 28
Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.
آية رقم 29
Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!
آية رقم 30
Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
آية رقم 31
Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.
آية رقم 32
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.
آية رقم 33
Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanazila!
آية رقم 34
Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem ndani yake,
آية رقم 35
Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?
آية رقم 36
Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.
آية رقم 37
Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.
آية رقم 38
Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.
آية رقم 39
Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.
آية رقم 40
Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.
آية رقم 41
Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.
آية رقم 42
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda.
آية رقم 43
Na tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi,
آية رقم 44
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Isipo kuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.
آية رقم 45
Na wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa...
آية رقم 46
Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni wenye kuipuuza.
آية رقم 47
Na wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru huwaambia walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli walisha mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri.
آية رقم 48
Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?
آية رقم 49
Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.
آية رقم 50
Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.
آية رقم 51
Na litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao Mlezi.
آية رقم 52
Watasema: Ole wetu! Nani aliye tufufua kwenye malazi yetu? Haya ndiyo aliyo yaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.
آية رقم 53
Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhuruishwa mbele yetu.
آية رقم 54
Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyo kuwa mkiyatenda.
آية رقم 55
Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi.
آية رقم 56
Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fakhari.
آية رقم 57
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakacho kitaka.
آية رقم 58
ﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
"Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu.
آية رقم 59
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na enyi wakosefu! Jitengeni leo!
آية رقم 60
Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet'ani? Hakika yeye ni adui dhaahiri kwenu.
آية رقم 61
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
آية رقم 62
Na bila ya shaka yeye amekwisha lipoteza kundi kubwa miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkifikiri?
آية رقم 63
ﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Hii basi ndiyo Jahannamu mliyo kuwa mkiahidiwa.
آية رقم 64
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Ingieni leo kwa vile mlivyo kuwa mkikufuru.
آية رقم 65
Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyo kuwa wakiyachuma.
آية رقم 66
Na tungeli penda tungeli yafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wange ionaje?
آية رقم 67
Na tungeli taka tunge wageuza sura hapo hapo walipo, basi wasinge weza kwenda wala kurudi.
آية رقم 68
Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii?
آية رقم 69
Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur'ani inayo bainisha.
آية رقم 70
Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri.
آية رقم 71
Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyo fanya mikono yetu wanyama wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki.
آية رقم 72
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanao wapanda, na baadhi yao wanawala.
آية رقم 73
Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?
آية رقم 74
Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati wapate kusaidiwa!
آية رقم 75
Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio watakuwa askari wao watakao hudhurishwa.
آية رقم 76
Basi maneno yao yasikuhuzunishe. Hakika Sisi tunayajua wanayo yaweka siri na wanayo yatangaza.
آية رقم 77
Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri!
آية رقم 78
Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika?
آية رقم 79
Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba.
آية رقم 80
Aliye kujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo mnawasha.
آية رقم 81
Kwani aliye ziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi.
آية رقم 82
Hakika amri yake anapo taka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa.
آية رقم 83
Basi Ametakasika yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake Yeye mtarejeshwa.
تقدم القراءة