ترجمة معاني سورة البروج باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Al-Buruj
Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
آية رقم 2
ﭟﭠ
ﭡ
Na kwa siku iliyo ahidiwa!
آية رقم 3
ﭢﭣ
ﭤ
Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
آية رقم 4
ﭥﭦﭧ
ﭨ
Wameangamizwa watu wa makhandaki
آية رقم 5
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Yenye moto wenye kuni nyingi,
آية رقم 6
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Walipo kuwa wamekaa hapo,
آية رقم 7
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
آية رقم 8
Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
آية رقم 9
Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
آية رقم 10
Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
آية رقم 11
Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
آية رقم 12
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
آية رقم 13
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
آية رقم 14
ﯙﯚﯛ
ﯜ
Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
آية رقم 15
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
آية رقم 16
ﯡﯢﯣ
ﯤ
Atendaye ayatakayo.
آية رقم 17
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
آية رقم 18
ﯪﯫ
ﯬ
Ya Firauni na Thamudi?
آية رقم 19
ﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
آية رقم 20
ﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
آية رقم 21
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Bali hii ni Qur'ani tukufu
آية رقم 22
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.
تقدم القراءة