ترجمة معاني سورة الصافات باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation

Ali Muhsin Al - Swahili translation

آية رقم 1

As-Saffat


Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
آية رقم 2

Na kwa wenye kukataza mabaya.
آية رقم 3

Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
آية رقم 4

Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
آية رقم 5

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
آية رقم 12

Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
آية رقم 31

Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
آية رقم 32

Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
آية رقم 33

Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
آية رقم 36

Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
آية رقم 38

Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
آية رقم 40

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
آية رقم 48

Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
آية رقم 49

Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
آية رقم 52

Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
آية رقم 57

Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
آية رقم 63

Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
آية رقم 65

Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
آية رقم 68

Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
آية رقم 71

Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
آية رقم 74

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
آية رقم 78

Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
آية رقم 80

Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
آية رقم 95

Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
آية رقم 96

Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
آية رقم 98

Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
آية رقم 99

Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
آية رقم 100

Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
آية رقم 101

Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
آية رقم 103

Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
آية رقم 107

Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
آية رقم 108

Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
آية رقم 110

Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
آية رقم 112

Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
آية رقم 116

Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
آية رقم 117

Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
آية رقم 118

Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
آية رقم 119

Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
آية رقم 122

Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
آية رقم 123

Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
آية رقم 126

Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
آية رقم 127

Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
آية رقم 128

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
آية رقم 129

Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
آية رقم 133

Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
آية رقم 135

Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
آية رقم 141

Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
آية رقم 142

Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
آية رقم 149

Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
آية رقم 152

Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
آية رقم 159

Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
آية رقم 160

Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
آية رقم 165

Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
آية رقم 166

Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
آية رقم 169

Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
آية رقم 171

Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
آية رقم 172

Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
آية رقم 176

Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
آية رقم 180

Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
آية رقم 182

Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
تقدم القراءة