ترجمة معاني سورة الصافات باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭑﭒ
ﭓ
As-Saffat
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
آية رقم 2
ﭔﭕ
ﭖ
Na kwa wenye kukataza mabaya.
آية رقم 3
ﭗﭘ
ﭙ
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
آية رقم 4
ﭚﭛﭜ
ﭝ
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
آية رقم 5
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
آية رقم 6
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
آية رقم 7
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
آية رقم 8
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
آية رقم 9
ﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
آية رقم 10
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
آية رقم 11
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
آية رقم 12
ﮙﮚﮛ
ﮜ
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
آية رقم 13
ﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
آية رقم 14
ﮢﮣﮤﮥ
ﮦ
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
آية رقم 15
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
آية رقم 16
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
آية رقم 17
ﯗﯘ
ﯙ
Hata baba zetu wa zamani?
آية رقم 18
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
آية رقم 19
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
آية رقم 20
ﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
آية رقم 21
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
آية رقم 22
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
آية رقم 23
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
آية رقم 24
ﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
آية رقم 25
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
آية رقم 26
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Bali hii leo, watasalimu amri.
آية رقم 27
ﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
آية رقم 28
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
آية رقم 29
ﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
آية رقم 30
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
آية رقم 31
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
آية رقم 32
ﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
آية رقم 33
ﮇﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
آية رقم 34
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
آية رقم 35
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
آية رقم 36
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
آية رقم 37
ﮤﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
آية رقم 38
ﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
آية رقم 39
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
ﯖ
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
آية رقم 40
ﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
آية رقم 41
ﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
آية رقم 42
ﯡﯢﯣ
ﯤ
Matunda, nao watahishimiwa.
آية رقم 43
ﯥﯦﯧ
ﯨ
Katika Bustani za neema.
آية رقم 44
ﯩﯪﯫ
ﯬ
Wako juu ya viti wamekabiliana.
آية رقم 45
ﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
آية رقم 46
ﯳﯴﯵ
ﯶ
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
آية رقم 47
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
آية رقم 48
ﯿﰀﰁﰂ
ﰃ
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
آية رقم 49
ﰄﰅﰆ
ﰇ
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
آية رقم 50
ﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
آية رقم 51
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
آية رقم 52
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
آية رقم 53
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
آية رقم 54
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
آية رقم 55
ﭣﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
آية رقم 56
ﭩﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
آية رقم 57
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
آية رقم 58
ﭶﭷﭸ
ﭹ
Je! Sisi hatutakufa,
آية رقم 59
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
ﮀ
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
آية رقم 60
ﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
آية رقم 61
ﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
آية رقم 62
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
آية رقم 63
ﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
آية رقم 64
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
آية رقم 65
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
آية رقم 66
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
آية رقم 67
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
آية رقم 68
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
آية رقم 69
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
آية رقم 70
ﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
آية رقم 71
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
آية رقم 72
ﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
آية رقم 73
ﯯﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
آية رقم 74
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
آية رقم 75
ﯺﯻﯼﯽﯾ
ﯿ
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
آية رقم 76
ﰀﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
آية رقم 77
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
آية رقم 78
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
آية رقم 79
ﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
آية رقم 80
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
آية رقم 81
ﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
آية رقم 82
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Kisha tukawazamisha wale wengine.
آية رقم 83
ﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
آية رقم 84
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
آية رقم 85
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
آية رقم 86
ﮂﮃﮄﮅﮆ
ﮇ
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
آية رقم 87
ﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
آية رقم 88
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
آية رقم 89
ﮒﮓﮔ
ﮕ
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
آية رقم 90
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
آية رقم 91
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
آية رقم 92
ﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Mna nini hata hamsemi?
آية رقم 93
ﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
آية رقم 94
ﮫﮬﮭ
ﮮ
Basi wakamjia upesi upesi.
آية رقم 95
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
آية رقم 96
ﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
آية رقم 97
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
آية رقم 98
ﯢﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
آية رقم 99
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
آية رقم 100
ﯯﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
آية رقم 101
ﯵﯶﯷ
ﯸ
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
آية رقم 102
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
آية رقم 103
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
آية رقم 104
ﭖﭗﭘ
ﭙ
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
آية رقم 105
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
آية رقم 106
ﭣﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
آية رقم 107
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
آية رقم 108
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
آية رقم 109
ﭲﭳﭴ
ﭵ
Iwe salama kwa Ibrahim!
آية رقم 110
ﭶﭷﭸ
ﭹ
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
آية رقم 111
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
آية رقم 112
ﭿﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
آية رقم 113
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
آية رقم 114
ﮑﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
آية رقم 115
ﮗﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
آية رقم 116
ﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
آية رقم 117
ﮢﮣﮤ
ﮥ
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
آية رقم 118
ﮦﮧﮨ
ﮩ
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
آية رقم 119
ﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
آية رقم 120
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
آية رقم 121
ﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
آية رقم 122
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
آية رقم 123
ﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
آية رقم 124
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
آية رقم 125
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
آية رقم 126
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
آية رقم 127
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
آية رقم 128
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
آية رقم 129
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
آية رقم 130
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Iwe salama kwa Ilyas.
آية رقم 131
ﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
آية رقم 132
ﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
آية رقم 133
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
آية رقم 134
ﭳﭴﭵﭶ
ﭷ
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
آية رقم 135
ﭸﭹﭺﭻ
ﭼ
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
آية رقم 136
ﭽﭾﭿ
ﮀ
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
آية رقم 137
ﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
آية رقم 138
ﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
آية رقم 139
ﮋﮌﮍﮎ
ﮏ
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
آية رقم 140
ﮐﮑﮒﮓﮔ
ﮕ
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
آية رقم 141
ﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
آية رقم 142
ﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
آية رقم 143
ﮠﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
آية رقم 144
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
آية رقم 145
ﮭﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
آية رقم 146
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
آية رقم 147
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
آية رقم 148
ﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
آية رقم 149
ﯦﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
آية رقم 150
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
آية رقم 151
ﯳﯴﯵﯶﯷ
ﯸ
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
آية رقم 152
ﯹﯺﯻﯼ
ﯽ
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
آية رقم 153
ﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
آية رقم 154
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
آية رقم 155
ﭖﭗ
ﭘ
Hamkumbuki?
آية رقم 156
ﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Au mnayo hoja iliyo wazi?
آية رقم 157
ﭞﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
آية رقم 158
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
آية رقم 159
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
آية رقم 160
ﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
آية رقم 161
ﭺﭻﭼ
ﭽ
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
آية رقم 162
ﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Hamwezi kuwapoteza
آية رقم 163
ﮃﮄﮅﮆﮇ
ﮈ
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
آية رقم 164
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
ﮏ
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
آية رقم 165
ﮐﮑﮒ
ﮓ
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
آية رقم 166
ﮔﮕﮖ
ﮗ
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
آية رقم 167
ﮘﮙﮚ
ﮛ
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
آية رقم 168
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
آية رقم 169
ﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
آية رقم 170
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
آية رقم 171
ﮮﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
آية رقم 172
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
آية رقم 173
ﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
آية رقم 174
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Basi waachilie mbali kwa muda.
آية رقم 175
ﯣﯤﯥ
ﯦ
Na watazame, nao wataona.
آية رقم 176
ﯧﯨ
ﯩ
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
آية رقم 177
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
آية رقم 178
ﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Na waache kwa muda.
آية رقم 179
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Na tazama, na wao wataona.
آية رقم 180
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
آية رقم 181
ﰁﰂﰃ
ﰄ
Na Salamu juu ya Mitume.
آية رقم 182
ﰅﰆﰇﰈ
ﰉ
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
تقدم القراءة