ترجمة معاني سورة المعارج باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Al-Ma'arij
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
آية رقم 2
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
آية رقم 3
ﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
آية رقم 4
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
آية رقم 5
ﯪﯫﯬ
ﯭ
Basi subiri kwa subira njema.
آية رقم 6
ﯮﯯﯰ
ﯱ
Hakika wao wanaiona iko mbali,
آية رقم 7
ﯲﯳ
ﯴ
Na Sisi tunaiona iko karibu.
آية رقم 8
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
آية رقم 9
ﯺﯻﯼ
ﯽ
Na milima itakuwa kama sufi.
آية رقم 10
ﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
آية رقم 11
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
آية رقم 12
ﭜﭝ
ﭞ
Na mkewe, na nduguye,
آية رقم 13
ﭟﭠﭡ
ﭢ
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
آية رقم 14
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
آية رقم 15
ﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
آية رقم 16
ﭯﭰ
ﭱ
Unao babua ngozi ya kichwa!
آية رقم 17
ﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
آية رقم 18
ﭷﭸ
ﭹ
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
آية رقم 19
ﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Hakika mtu ameumbwa na papara.
آية رقم 20
ﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Inapo mgusa shari hupapatika.
آية رقم 21
ﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na inapo mgusa kheri huizuilia.
آية رقم 22
ﮊﮋ
ﮌ
Isipo kuwa wanao sali,
آية رقم 23
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Ambao wanadumisha Sala zao,
آية رقم 24
ﮓﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
آية رقم 25
ﮙﮚ
ﮛ
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
آية رقم 26
ﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
آية رقم 27
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
آية رقم 28
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
آية رقم 29
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Na ambao wanahifadhi tupu zao.
آية رقم 30
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
آية رقم 31
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
آية رقم 32
ﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
آية رقم 33
ﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
آية رقم 34
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
آية رقم 35
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
آية رقم 36
ﯽﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
آية رقم 37
ﰃﰄﰅﰆﰇ
ﰈ
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
آية رقم 38
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
آية رقم 39
ﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
ﰘ
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
آية رقم 40
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
آية رقم 41
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
آية رقم 42
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
آية رقم 43
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
آية رقم 44
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.
تقدم القراءة