ترجمة معاني سورة المؤمنون باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Al-Muminu
HAKIKA wamefanikiwa Waumini,
آية رقم 2
ﭕﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Ambao ni wanyenyekevu katika Sala zao,
آية رقم 3
ﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi,
آية رقم 4
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Na ambao wanatoa Zaka,
آية رقم 5
ﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Na ambao wanazilinda tupu zao,
آية رقم 6
Isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa.
آية رقم 7
Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka.
آية رقم 8
ﭾﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Na ambao wanazitimiza amana zao na ahadi zao,
آية رقم 9
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na ambao Sala zao wanazihifadhi -
آية رقم 10
ﮊﮋﮌ
ﮍ
Hao ndio warithi,
آية رقم 11
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Ambao watairithi Pepo ya Firdausi, wadumu humo.
آية رقم 12
Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo.
آية رقم 13
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.
آية رقم 14
Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.
آية رقم 15
ﯜﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Kisha hakika nyinyi baada ya hayo mtakufa.
آية رقم 16
ﯢﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Kisha hakika nyinyi Siku ya Kiyama mtafufuliwa.
آية رقم 17
Na kwa yakini tumeziumba juu yenu njia saba. Nasi hatukuwa wenye kughafilika na viumbe.
آية رقم 18
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi na tukayatuliza katika ardhi. Na hakika Sisi tunaweza kuyaondoa.
آية رقم 19
Kwa maji hayo tukakufanyieni bustani za mitende na mizabibu, mnapata humo matunda mengi, na katika hayo mnakula;
آية رقم 20
Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao.
آية رقم 21
Na hakika mnayo mazingatio makubwa katika nyama hoa - tunakunywesheni katika vile viliomo matumboni mwao, na nyinyi mnapata katika hao manufaa mengi, na pia mnawala.
آية رقم 22
ﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Na juu yao na juu ya marikebu mnabebwa.
آية رقم 23
Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna mungu asiye kuwa Yeye. Basi je! Hamwogopi?
آية رقم 24
Walisema wale wakuu walio kufuru katika watu wake: Huyu si chochote ila ni mtu tu kama nyinyi. Anataka kujipa ubora juu yenu. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu amependa basi yakini angeli teremsha Malaika. Hatukusikia haya kwa baba zetu wa zamani.
آية رقم 25
Huyu si lolote ila ni mtu mwenye wazimu. Basi mngojeeni tu kwa muda.
آية رقم 26
ﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Akasema (Nuhu): Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa kuwa wamenikanusha.
آية رقم 27
Tukampa wahyi: Unda jahazi mbele ya macho yetu na uwongozi wetu! Basi itapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa.
آية رقم 28
Basi utakapo tulia wewe na walio pamoja nawe humo marikebuni, sema: Alhamdulillahi Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, aliye tuokoa na watu madhaalimu!
آية رقم 29
Na sema: Mola wangu Mlezi! Niteremshe mteremsho wenye baraka, na Wewe ni Mbora wa wateremshaji.
آية رقم 30
Hakika katika hayo yapo mazingatio. Na kwa yakini Sisi ni wenye kuwafanyia mtihani.
آية رقم 31
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Kisha baada yao tukaanzisha kizazi kingine.
آية رقم 32
Tukawapelekea Mtume miongoni mwao, kuwaambia: Muabuduni Mwenyezi Mungu! Hamna mungu asiye kuwa Yeye. Jee, hamwogopi?
آية رقم 33
Na wakubwa katika watu wake walio kufuru na wakakanusha mkutano wa Akhera, na tukawadekeza kwa starehe katika maisha ya dunia, walisema: Huyu si chochote ila ni binaadamu kama nyinyi; anakula mlacho, na anakunywa mnywacho.
آية رقم 34
Na nyinyi mkimt'ii mtu kama nyinyi basi hakika mtakuwa khasarani.
آية رقم 35
Hivyo anakuahidini ati ya kwamba mtakapo kufa na mkawa udongo na mifupa kuwa mtatolewa?
آية رقم 36
ﯖﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Hayawi! Hayawi hayo mnayo ahidiwa.
آية رقم 37
Hapana ila uhai wetu wa duniani tu, tunakufa na kuishi basi. Wala sisi hatutafufuliwa.
آية رقم 38
Huyu si lolote ila ni mtu anaye mzulia Mwenyezi Mungu uwongo, wala sisi sio wa kumuamini.
آية رقم 39
ﯴﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa sababu wananikanusha.
آية رقم 40
ﯺﯻﯼﯽﯾ
ﯿ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Baada ya muda mchache watakuwa wenye kujuta.
آية رقم 41
Basi ukawanyakua ukelele kwa haki, na tukawafanya kama takataka zinazo elea juu ya maji. Ikapotelea mbali kaumu ya madhaalimu!
آية رقم 42
ﰊﰋﰌﰍﰎﰏ
ﰐ
Kisha tukaleta baada yao vizazi vingine.
آية رقم 43
Hapana umma uwezao kutanguliza ajali yake wala kuikawiza.
آية رقم 44
Kisha tukawatuma Mitume wetu, mmoja baada ya mmoja. Kila umma alipo wafikia Mtume wao walimkanusha. Tukawafuatanisha hawa baada ya hawa, na tukawafanya ni hadithi za kusimuliwa. Wakapotelea mbali watu wasio amini.
آية رقم 45
Kisha tukamtuma Musa na nduguye, Haaruni, pamoja na ishara zetu na hoja zilizo wazi.
آية رقم 46
Kumwendea Firauni na wakuu wake. Lakini walijivuna, nao walikuwa watu majeuri.
آية رقم 47
Wakasema: Je, tuwaamini wanaadamu wawili hawa kama sisi, na ambao watu wao ni watumwa wetu?
آية رقم 48
ﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Basi wakawakanusha, na wakawa miongoni mwa walio angamizwa.
آية رقم 49
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Na hakika tulimpa Musa Kitabu ili wapate kuongoka.
آية رقم 50
Na tukamfanya mwana wa Mariamu na mama yake kuwa ni Ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipo inuka penye utulivu na chemchem za maji.
آية رقم 51
Enyi Mitume! Kuleni vyakula vizuri na tendeni mema. Hakika Mimi ni Mjuzi wa mnayo yatenda.
آية رقم 52
Na kwa yakini huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi, basi nicheni Mimi.
آية رقم 53
Lakini walikatiana jambo lao mapande mbali mbali. Kila kundi likifurahia kwa waliyo nayo.
آية رقم 54
ﯣﯤﯥﯦﯧ
ﯨ
Basi waache katika ghafla yao kwa muda.
آية رقم 55
Je! Wanadhani ya kuwa kwa vile tunavyo wapa mali na watoto
آية رقم 56
Ndio tunawahimizia kheri? Lakini wenyewe hawatambui.
آية رقم 57
Kwa hakika hao ambao kwa kumwogopa Mola wao Mlezi wananyenyekea,
آية رقم 58
ﰂﰃﰄﰅﰆ
ﰇ
Na wale ambao Ishara za Mola wao Mlezi wanaziamini,
آية رقم 59
ﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Na wale ambao Mola wao Mlezi hawamshirikishi,
آية رقم 60
Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinagopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi,
آية رقم 61
Basi wote hao ndio wanao kimbilia katika mambo ya kheri, na ndio watakao tangulia kuyafikia.
آية رقم 62
Na hatuilazimishi nafsi ila kwa kadri ya uwezo wake. Na tunacho kitabu kisemacho kweli. Nao hawatadhulumiwa.
آية رقم 63
Lakini nyoyo zao zimeghafilika na hayo, na wanavyo vitendo vinginevyo wanavyo vifanya.
آية رقم 64
Hata tutakapo watia katika adhabu wale walio dekezwa kwa starehe kati yao, hapo ndipo watapo yayatika.
آية رقم 65
Msiyayatike leo! Hakika nyinyi hamtanusurika nasi.
آية رقم 66
Hakika zilikuwa Aya zangu mkisomewa, nanyi mkirudi nyuma juu ya visigino vyenu,
آية رقم 67
ﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Na huku mkitakabari na usiku mkiizungumza (Qur'ani) kwa dharau.
آية رقم 68
Je, hawakuifikiri kauli, au yamewajia yasiyo wafikia baba zao wa zamani?
آية رقم 69
Au hawakumjua Mtume wao, ndio maana wanamkataa?
آية رقم 70
Au wanasema: Ana wazimu? Bali amewajia kwa Haki, na wengi wao wanaichukia Haki.
آية رقم 71
Na lau kuwa Haki ingeli fuata matamanio yao, basi zingeli haribika mbingu na ardhi na waliomo ndani. Bali tumewaletea ukumbusho wao, nao wanajitenga mbali na ukumbusho wao.
آية رقم 72
Au unawaomba ujira? Lakini ujira wa Mola wako Mlezi ni bora, na Yeye ndiye Mbora wa wanao ruzuku.
آية رقم 73
ﯿﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Na kwa yakini wewe unawaita kwenye Njia Iliyo Nyooka.
آية رقم 74
Na hakika wale wasio iamini Akhera wanajitenga na Njia hiyo.
آية رقم 75
Na lau tungeli warehemu na tukawaondolea shida waliyo nayo bila ya shaka wangeli endelea katika upotofu wao vile vile, wakitangatanga.
آية رقم 76
Na hakika tuliwatia adhabu kali; lakini hawakuelekea kwa Mola wao Mlezi wala hawakunyenyekea.
آية رقم 77
Mpaka tulipo wafungulia mlango wa adhabu kali, hapo ndipo wakawa wenye kukata tamaa.
آية رقم 78
Na Yeye ndiye aliye kuumbieni kusikia na kuona na nyoyo za kufahamu. Ni kuchache mno kushukuru kwenu.
آية رقم 79
Na Yeye ndiye aliye kuenezeni katika ardhi, na kwake Yeye mtakusanywa.
آية رقم 80
Na Yeye ndiye anaye huisha na kufisha, na yake Yeye mabadiliko ya usiku na mchana. Basi je! Hamfahamu?
آية رقم 81
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Bali wanasema kama walivyo sema watu wa kwanza.
آية رقم 82
Walisema: Je! Tukisha kufa tukawa udongo na mifupa ndio tutafufuliwa?
آية رقم 83
Tuliahidiwa haya sisi na baba zetu zamani. Hayakuwa haya ila ni visa vya uwongo vya watu wa zamani.
آية رقم 84
Sema: Ni ya nani ardhi na viliomo ndani yake, kama nyinyi mnajua?
آية رقم 85
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu! Sema: Basi, je, hamkumbuki?
آية رقم 86
Sema: Ni nani Mola Mlezi wa mbingu saba na Mola Mlezi wa A'rshi Kuu?
آية رقم 87
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu. Sema: Basi je, hamwogopi?
آية رقم 88
Sema: Ni nani mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu, naye ndiye anaye linda, wala hakilindwi asicho taka, kama mnajua?
آية رقم 89
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
ﰇ
Watasema: (Ufalme huo) ni wa Mwenyezi Mungu. Sema: Basi vipi mnadanganyika?
آية رقم 90
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Bali tumewaletea Haki, na kwa yakini hao ni waongo.
آية رقم 91
Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.
آية رقم 92
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Mjuzi wa siri na dhaahiri, na ametukuka juu ya hayo wanayo mshirikisha nayo.
آية رقم 93
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Sema: Mola wangu Mlezi! Ukinionyesha adhabu waliyo ahidiwa,
آية رقم 94
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Mola wangu Mlezi! Usinijaalie katika watu madhaalimu hao.
آية رقم 95
Na hakika Sisi ni waweza wa kukuonyeshsa tuliyo waahidi.
آية رقم 96
Kinga maovu kwa kutenda yaliyo mema zaidi. Sisi tunajua wayasemayo.
آية رقم 97
Na sema: Mola wangu Mlezi! Najikinga kwako na wasiwasi wa mashet'ani.
آية رقم 98
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na najikinga kwako, Mola wangu Mlezi, wasinikaribie.
آية رقم 99
Mpaka yanapo mfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu Mlezi! Nirudishe.
آية رقم 100
Ili nitende mema sasa badala ya yale niliyo yaacha. Wapi! Hii ni kauli aisemayo yeye tu. Na nyuma yao kipo kizuizi mpaka siku watapo fufuliwa.
آية رقم 101
Basi litapo pulizwa baragumu hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana.
آية رقم 102
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa.
آية رقم 103
Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia khasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu.
آية رقم 104
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
ﰉ
Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizo kunjana.
آية رقم 105
Je! Hazikuwa Aya zangu mkisomewa, na nyinyi mkizikanusha?
آية رقم 106
Mola wetu Mlezi! Tulizidiwa na uovu wetu na tukawa watu tulio potea.
آية رقم 107
Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena basi kweli sisi ni wenye kudhulumu.
آية رقم 108
ﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Atasema Mwenyezi Mungu: Tokomeeni humo, wala msinisemeze.
آية رقم 109
Bila ya shaka lilikuwapo kundi katika waja wangu likisema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini; basi tusamehe na uturehemu, nawe ndiwe Mbora wa wanao rehemu.
آية رقم 110
Lakini nyinyi mliwakejeli hata wakakusahaulisheni kunikumbuka, na mlikuwa mkiwacheka.
آية رقم 111
Hakika Mimi leo nimewalipa kwa vile walivyo subiri. Bila ya shaka hao ndio wenye kufuzu.
آية رقم 112
Atasema: Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka?
آية رقم 113
Watasema: Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu.
آية رقم 114
Atasema: Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti ingeli kuwa mnajua.
آية رقم 115
Je! Mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa?
آية رقم 116
Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki, hapana mungu ila Yeye, Mola Mlezi wa A'rshi Tukufu.
آية رقم 117
Na anaye muomba - pamoja na Mwenyezi Mungu - mungu mwenginewe hana ushahidi wa hili; basi bila ya shaka hisabu yake iko kwa Mola wake Mlezi. Kwa hakika makafiri hawafanikiwi.
آية رقم 118
Nawe sema: Mola wangu Mlezi! Samehe na urehemu nawe ni Mbora wa wanao rehemu.
تقدم القراءة