ترجمة معاني سورة الدّخان باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭑ
ﭒ
Ad-Dukhan
H'a Mim
آية رقم 2
ﭓﭔ
ﭕ
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
آية رقم 3
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
آية رقم 4
ﭠﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
آية رقم 5
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
آية رقم 6
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
آية رقم 7
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
آية رقم 8
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
آية رقم 9
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Lakini wao wanacheza katika shaka.
آية رقم 10
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
آية رقم 11
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
آية رقم 12
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
آية رقم 13
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
آية رقم 14
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
آية رقم 15
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
آية رقم 16
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
آية رقم 17
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
آية رقم 18
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
آية رقم 19
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
آية رقم 20
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
آية رقم 21
ﭣﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
آية رقم 22
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
آية رقم 23
ﭰﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
آية رقم 24
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
آية رقم 25
ﭾﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
آية رقم 26
ﮄﮅﮆ
ﮇ
Na mimea na vyeo vitukufu!
آية رقم 27
ﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
آية رقم 28
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
آية رقم 29
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
آية رقم 30
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
آية رقم 31
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
آية رقم 32
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
آية رقم 33
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
آية رقم 34
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Hakika hawa wanasema:
آية رقم 35
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
آية رقم 36
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
آية رقم 37
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
آية رقم 38
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
آية رقم 39
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
آية رقم 40
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
آية رقم 41
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
آية رقم 42
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
آية رقم 43
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Hakika Mti wa Zaqqum,
آية رقم 44
ﭯﭰ
ﭱ
Ni chakula cha mwenye dhambi.
آية رقم 45
ﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
آية رقم 46
ﭷﭸ
ﭹ
Kama kutokota kwa maji ya moto.
آية رقم 47
ﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
آية رقم 48
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
آية رقم 49
ﮈﮉﮊﮋﮌ
ﮍ
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
آية رقم 50
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
آية رقم 51
ﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
آية رقم 52
ﮛﮜﮝ
ﮞ
Katika mabustani na chemchem,
آية رقم 53
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
آية رقم 54
ﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
آية رقم 55
ﮪﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
آية رقم 56
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
آية رقم 57
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
آية رقم 58
ﯦﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
آية رقم 59
ﯬﯭﯮ
ﯯ
Ngoja tu, na wao wangoje pia.
تقدم القراءة