ترجمة معاني سورة الذاريات باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﯤﯥ
ﯦ
Az-Zariyat
Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
آية رقم 2
ﯧﯨ
ﯩ
Na zinazo beba mizigo,
آية رقم 3
ﯪﯫ
ﯬ
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
آية رقم 4
ﯭﯮ
ﯯ
Na zinazo gawanya kwa amri,
آية رقم 5
ﯰﯱﯲ
ﯳ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
آية رقم 6
ﯴﯵﯶ
ﯷ
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
آية رقم 7
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Naapa kwa mbingu zenye njia,
آية رقم 8
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
آية رقم 9
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
آية رقم 10
ﭟﭠ
ﭡ
Wazushi wameangamizwa.
آية رقم 11
ﭢﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Ambao wameghafilika katika ujinga.
آية رقم 12
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
آية رقم 13
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
آية رقم 14
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
آية رقم 15
ﭻﭼﭽﭾﭿ
ﮀ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
آية رقم 16
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
آية رقم 17
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
آية رقم 18
ﮓﮔﮕ
ﮖ
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
آية رقم 19
ﮗﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
آية رقم 20
ﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
آية رقم 21
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
آية رقم 22
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
آية رقم 23
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
آية رقم 24
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
ﯟ
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
آية رقم 25
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
آية رقم 26
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
آية رقم 27
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
آية رقم 28
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
آية رقم 29
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
آية رقم 30
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
آية رقم 31
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
آية رقم 32
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
آية رقم 33
ﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Tuwatupie mawe ya udongo,
آية رقم 34
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
آية رقم 35
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
آية رقم 36
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
آية رقم 37
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
آية رقم 38
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
آية رقم 39
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
آية رقم 40
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
آية رقم 41
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
آية رقم 42
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
آية رقم 43
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
آية رقم 44
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
آية رقم 45
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
آية رقم 46
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
آية رقم 47
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
آية رقم 48
ﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
آية رقم 49
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
آية رقم 50
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
آية رقم 51
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
آية رقم 52
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
آية رقم 53
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
آية رقم 54
ﭧﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
آية رقم 55
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
آية رقم 56
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
آية رقم 57
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
آية رقم 58
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
آية رقم 59
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
آية رقم 60
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
تقدم القراءة