ترجمة معاني سورة الرحمن باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭷ
ﭸ
Ar-Rahman
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
آية رقم 2
ﭹﭺ
ﭻ
Amefundisha Qur'ani.
آية رقم 3
ﭼﭽ
ﭾ
Amemuumba mwanaadamu,
آية رقم 4
ﭿﮀ
ﮁ
Akamfundisha kubaini.
آية رقم 5
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
آية رقم 6
ﮆﮇﮈ
ﮉ
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
آية رقم 7
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
آية رقم 8
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Ili msidhulumu katika mizani.
آية رقم 9
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
آية رقم 10
ﮛﮜﮝ
ﮞ
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
آية رقم 11
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
آية رقم 12
ﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
آية رقم 13
ﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
آية رقم 14
ﮯﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
آية رقم 15
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
آية رقم 16
ﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
آية رقم 17
ﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
آية رقم 18
ﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 19
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
آية رقم 20
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
آية رقم 21
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 22
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
آية رقم 23
ﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 24
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
آية رقم 25
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 26
ﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Kila kilioko juu yake kitatoweka.
آية رقم 27
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
ﮀ
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
آية رقم 28
ﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 29
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
آية رقم 30
ﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 31
ﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
آية رقم 32
ﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 33
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
آية رقم 34
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 35
Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
آية رقم 36
ﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 37
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
آية رقم 38
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 39
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
آية رقم 40
ﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 41
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
ﰇ
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
آية رقم 42
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 43
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
آية رقم 44
ﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
آية رقم 45
ﭣﭤﭥﭦ
ﭧ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 46
ﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
آية رقم 47
ﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 48
ﭳﭴ
ﭵ
Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
آية رقم 49
ﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 50
ﭻﭼﭽ
ﭾ
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
آية رقم 51
ﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 52
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
آية رقم 53
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 54
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
آية رقم 55
ﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 56
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
آية رقم 57
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 58
ﮮﮯﮰ
ﮱ
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
آية رقم 59
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
آية رقم 60
ﯘﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
آية رقم 61
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 62
ﯣﯤﯥ
ﯦ
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
آية رقم 63
ﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 64
ﯬ
ﯭ
Za kijani kibivu.
آية رقم 65
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 66
ﯳﯴﯵ
ﯶ
Na chemchem mbili zinazo furika.
آية رقم 67
ﯷﯸﯹﯺ
ﯻ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 68
ﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
آية رقم 69
ﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 70
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Humo wamo wanawake wema wazuri.
آية رقم 71
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 72
ﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
آية رقم 73
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 74
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
آية رقم 75
ﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 76
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
آية رقم 77
ﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
آية رقم 78
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
تقدم القراءة