ترجمة معاني سورة الحاقة باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮯ
ﮰ
Al-Hakkah
Tukio la haki.
آية رقم 2
ﮱﯓ
ﯔ
Nini hilo Tukio la haki?
آية رقم 3
ﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
آية رقم 4
ﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
آية رقم 5
ﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
آية رقم 6
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
آية رقم 7
Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
آية رقم 8
ﯼﯽﯾﯿﰀ
ﰁ
Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?
آية رقم 9
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.
آية رقم 10
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.
آية رقم 11
Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,
آية رقم 12
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.
آية رقم 13
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,
آية رقم 14
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,
آية رقم 15
ﭼﭽﭾ
ﭿ
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
آية رقم 16
ﮀﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
آية رقم 17
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
آية رقم 18
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
آية رقم 19
Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
آية رقم 20
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
آية رقم 21
ﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,
آية رقم 22
ﮭﮮﮯ
ﮰ
Katika Bustani ya juu,
آية رقم 23
ﮱﯓ
ﯔ
Matunda yake yakaribu.
آية رقم 24
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.
آية رقم 25
Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!
آية رقم 26
ﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.
آية رقم 27
ﯮﯯﯰ
ﯱ
Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.
آية رقم 28
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Mali yangu hayakunifaa kitu.
آية رقم 29
ﯸﯹﯺ
ﯻ
Madaraka yangu yamenipotea.
آية رقم 30
ﯼﯽ
ﯾ
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
آية رقم 31
ﯿﰀﰁ
ﰂ
Kisha mtupeni Motoni!
آية رقم 32
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!
آية رقم 33
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
ﰑ
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,
آية رقم 34
ﰒﰓﰔﰕﰖ
ﰗ
Wala hahimizi kulisha masikini.
آية رقم 35
ﰘﰙﰚﰛﰜ
ﰝ
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,
آية رقم 36
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
آية رقم 37
ﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
آية رقم 38
ﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Basi naapa kwa mnavyo viona,
آية رقم 39
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Na msivyo viona,
آية رقم 40
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
آية رقم 41
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
آية رقم 42
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
آية رقم 43
ﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 44
ﮀﮁﮂﮃﮄ
ﮅ
Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,
آية رقم 45
ﮆﮇﮈ
ﮉ
Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,
آية رقم 46
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!
آية رقم 47
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
ﮕ
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.
آية رقم 48
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.
آية رقم 49
ﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.
آية رقم 50
ﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
آية رقم 51
ﮥﮦﮧ
ﮨ
Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
آية رقم 52
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
تقدم القراءة