ترجمة معاني سورة القمر باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮬﮭﮮﮯ
ﮰ
Al-Kamar
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
آية رقم 2
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
آية رقم 3
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
آية رقم 4
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
آية رقم 5
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
آية رقم 6
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
آية رقم 7
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
آية رقم 8
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
آية رقم 9
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
آية رقم 10
ﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!
آية رقم 11
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
آية رقم 12
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
آية رقم 13
ﮅﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
آية رقم 14
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
آية رقم 15
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
آية رقم 16
ﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
آية رقم 17
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?
آية رقم 18
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
آية رقم 19
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
آية رقم 20
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
ﯞ
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.
آية رقم 21
ﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
آية رقم 22
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?
آية رقم 23
ﯬﯭﯮ
ﯯ
Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
آية رقم 24
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!
آية رقم 25
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!
آية رقم 26
ﰅﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
آية رقم 27
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.
آية رقم 28
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.
آية رقم 29
ﭛﭜﭝﭞ
ﭟ
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
آية رقم 30
ﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
آية رقم 31
Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
آية رقم 32
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?
آية رقم 33
ﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
آية رقم 34
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
آية رقم 35
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
آية رقم 36
ﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
آية رقم 37
Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!
آية رقم 38
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
آية رقم 39
ﮥﮦﮧ
ﮨ
Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!
آية رقم 40
Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?
آية رقم 41
ﮱﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.
آية رقم 42
Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.
آية رقم 43
Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?
آية رقم 44
ﯫﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
آية رقم 45
ﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
آية رقم 46
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
آية رقم 47
ﯽﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.
آية رقم 48
Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!
آية رقم 49
ﰍﰎﰏﰐﰑ
ﰒ
Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
آية رقم 50
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
آية رقم 51
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
آية رقم 52
ﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
آية رقم 53
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
آية رقم 54
ﭪﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
آية رقم 55
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
تقدم القراءة