ترجمة معاني سورة الشعراء باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﭑ
ﭒ
As-Shu'ara
T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)
آية رقم 2
ﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
آية رقم 3
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
آية رقم 4
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
آية رقم 5
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
آية رقم 6
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
آية رقم 7
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
آية رقم 8
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
آية رقم 9
ﮖﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
آية رقم 10
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
آية رقم 11
ﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Watu wa Firauni. Hawaogopi?
آية رقم 12
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰ
ﮱ
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
آية رقم 13
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
آية رقم 14
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
آية رقم 15
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
آية رقم 16
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 17
ﯵﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
آية رقم 18
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?
آية رقم 19
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?
آية رقم 20
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
آية رقم 21
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
آية رقم 22
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
آية رقم 23
ﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
آية رقم 24
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
آية رقم 25
ﭾﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
آية رقم 26
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
آية رقم 27
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
آية رقم 28
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
آية رقم 29
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
آية رقم 30
ﮦﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
آية رقم 31
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.
آية رقم 32
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.
آية رقم 33
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
آية رقم 34
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
آية رقم 35
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
آية رقم 36
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
آية رقم 37
ﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
آية رقم 38
ﰁﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
آية رقم 39
ﰇﰈﰉﰊﰋ
ﰌ
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
آية رقم 40
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
آية رقم 41
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?
آية رقم 42
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
آية رقم 43
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
آية رقم 44
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
آية رقم 45
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
آية رقم 46
ﮈﮉﮊ
ﮋ
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.
آية رقم 47
ﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 48
ﮑﮒﮓ
ﮔ
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
آية رقم 49
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
آية رقم 50
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
آية رقم 51
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.
آية رقم 52
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
آية رقم 53
ﯭﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
آية رقم 54
ﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
آية رقم 55
ﯸﯹﯺ
ﯻ
Nao wanatuudhi.
آية رقم 56
ﯼﯽﯾ
ﯿ
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
آية رقم 57
ﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
آية رقم 58
ﰅﰆﰇ
ﰈ
Na makhazina, na vyeo vya hishima,
آية رقم 59
ﰉﰊﰋﰌﰍ
ﰎ
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
آية رقم 60
ﰏﰐ
ﰑ
Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.
آية رقم 61
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!
آية رقم 62
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
آية رقم 63
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
آية رقم 64
ﭱﭲﭳ
ﭴ
Na tukawajongeza hapo wale wengine.
آية رقم 65
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
آية رقم 66
ﭻﭼﭽ
ﭾ
Kisha tukawazamisha hao wengine.
آية رقم 67
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.
آية رقم 68
ﮉﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
آية رقم 69
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na wasomee khabari za Ibrahim.
آية رقم 70
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
آية رقم 71
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
ﮡ
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
آية رقم 72
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?
آية رقم 73
ﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?
آية رقم 74
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
آية رقم 75
ﯕﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-
آية رقم 76
ﯛﯜﯝ
ﯞ
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
آية رقم 77
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 78
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,
آية رقم 79
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
آية رقم 80
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.
آية رقم 81
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
آية رقم 82
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
آية رقم 83
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
ﰉ
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.
آية رقم 84
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
آية رقم 85
ﭘﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
آية رقم 86
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
آية رقم 87
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.
آية رقم 88
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
آية رقم 89
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
ﭷ
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
آية رقم 90
ﭸﭹﭺ
ﭻ
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.
آية رقم 91
ﭼﭽﭾ
ﭿ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
آية رقم 92
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
آية رقم 93
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
آية رقم 94
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
آية رقم 95
ﮔﮕﮖ
ﮗ
Na majeshi ya Ibilisi yote.
آية رقم 96
ﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
آية رقم 97
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
آية رقم 98
ﮤﮥﮦﮧ
ﮨ
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 99
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.
آية رقم 100
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Basi hatuna waombezi.
آية رقم 101
ﯔﯕﯖ
ﯗ
Wala rafiki wa dhati.
آية رقم 102
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
آية رقم 103
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
آية رقم 104
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
آية رقم 105
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
آية رقم 106
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
آية رقم 107
ﯽﯾﯿﰀ
ﰁ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
آية رقم 108
ﰂﰃﰄ
ﰅ
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
آية رقم 109
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 110
ﰓﰔﰕ
ﰖ
Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
آية رقم 111
ﰗﰘﰙﰚﰛﰜ
ﰝ
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
آية رقم 112
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?
آية رقم 113
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!
آية رقم 114
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
آية رقم 115
ﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
آية رقم 116
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
آية رقم 117
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
آية رقم 118
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.
آية رقم 119
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.
آية رقم 120
ﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.
آية رقم 121
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.
آية رقم 122
ﮛﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
آية رقم 123
ﮡﮢﮣ
ﮤ
Kina A'd waliwakanusha Mitume.
آية رقم 124
Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?
آية رقم 125
ﮭﮮﮯﮰ
ﮱ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
آية رقم 126
ﯓﯔﯕ
ﯖ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
آية رقم 127
Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 128
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
آية رقم 129
ﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!
آية رقم 130
ﯯﯰﯱﯲ
ﯳ
Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.
آية رقم 131
ﯴﯵﯶ
ﯷ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
آية رقم 132
ﯸﯹﯺﯻﯼ
ﯽ
Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.
آية رقم 133
ﯾﯿﰀ
ﰁ
Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.
آية رقم 134
ﰂﰃ
ﰄ
Na mabustani na chemchem.
آية رقم 135
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
ﰋ
Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.
آية رقم 136
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
آية رقم 137
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
آية رقم 138
ﭗﭘﭙ
ﭚ
Wala sisi hatutaadhibiwa.
آية رقم 139
Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
آية رقم 140
ﭨﭩﭪﭫﭬ
ﭭ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
آية رقم 141
ﭮﭯﭰ
ﭱ
Kina Thamud waliwakanusha Mitume.
آية رقم 142
Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?
آية رقم 143
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
آية رقم 144
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
آية رقم 145
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 146
ﮐﮑﮒﮓﮔ
ﮕ
Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
آية رقم 147
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Katika mabustani, na chemchem?
آية رقم 148
ﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.
آية رقم 149
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
آية رقم 150
ﮥﮦﮧ
ﮨ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
آية رقم 151
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,
آية رقم 152
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
ﯕ
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.
آية رقم 153
ﯖﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.
آية رقم 154
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
آية رقم 155
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
آية رقم 156
Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.
آية رقم 157
ﯺﯻﯼ
ﯽ
Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.
آية رقم 158
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
آية رقم 159
ﰋﰌﰍﰎﰏ
ﰐ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
آية رقم 160
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.
آية رقم 161
Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?
آية رقم 162
ﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
آية رقم 163
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.
آية رقم 164
Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 165
ﭴﭵﭶﭷ
ﭸ
Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
آية رقم 166
Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!
آية رقم 167
Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!
آية رقم 168
ﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.
آية رقم 169
ﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
آية رقم 170
ﮛﮜﮝ
ﮞ
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,
آية رقم 171
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.
آية رقم 172
ﮤﮥﮦ
ﮧ
Kisha tukawaangamiza wale wengine.
آية رقم 173
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.
آية رقم 174
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
آية رقم 175
ﯛﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
آية رقم 176
ﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
آية رقم 177
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?
آية رقم 178
ﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
آية رقم 179
ﯲﯳﯴ
ﯵ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
آية رقم 180
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 181
Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.
آية رقم 182
ﰋﰌﰍ
ﰎ
Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;
آية رقم 183
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.
آية رقم 184
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.
آية رقم 185
ﭗﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.
آية رقم 186
Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
آية رقم 187
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
آية رقم 188
ﭱﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.
آية رقم 189
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.
آية رقم 190
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
آية رقم 191
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
آية رقم 192
ﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
آية رقم 193
ﮘﮙﮚﮛ
ﮜ
Ameuteremsha Roho muaminifu,
آية رقم 194
ﮝﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,
آية رقم 195
ﮣﮤﮥ
ﮦ
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
آية رقم 196
ﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
آية رقم 197
Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?
آية رقم 198
ﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,
آية رقم 199
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.
آية رقم 200
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.
آية رقم 201
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
آية رقم 202
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.
آية رقم 203
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Na watasema: Je, tutapewa muhula?
آية رقم 204
ﯽﯾ
ﯿ
Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?
آية رقم 205
ﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,
آية رقم 206
ﰅﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,
آية رقم 207
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?
آية رقم 208
Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -
آية رقم 209
ﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
آية رقم 210
ﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,
آية رقم 211
ﭪﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
آية رقم 212
ﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Hakika hao wametengwa na kusikia.
آية رقم 213
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.
آية رقم 214
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
آية رقم 215
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.
آية رقم 216
Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.
آية رقم 217
ﮒﮓﮔﮕ
ﮖ
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
آية رقم 218
ﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Ambaye anakuona unapo simama,
آية رقم 219
ﮜﮝﮞ
ﮟ
Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.
آية رقم 220
ﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
آية رقم 221
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?
آية رقم 222
ﮬﮭﮮﮯﮰ
ﮱ
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
آية رقم 223
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.
آية رقم 224
ﯘﯙﯚ
ﯛ
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
آية رقم 225
Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
آية رقم 226
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?
آية رقم 227
Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.
تقدم القراءة