ترجمة معاني سورة الحجر باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
A-Hijr
Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.
آية رقم 2
HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
آية رقم 3
Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
آية رقم 4
Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
آية رقم 5
Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
آية رقم 6
Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
آية رقم 7
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
آية رقم 8
Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
آية رقم 9
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
آية رقم 10
Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
آية رقم 11
Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
آية رقم 12
ﮰﮱﯓﯔﯕ
ﯖ
Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
آية رقم 13
Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
آية رقم 14
Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
آية رقم 15
Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
آية رقم 16
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
آية رقم 17
ﭙﭚﭛﭜﭝ
ﭞ
Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
آية رقم 18
Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
آية رقم 19
Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.
آية رقم 20
Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
آية رقم 21
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.
آية رقم 22
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
آية رقم 23
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
آية رقم 24
Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
آية رقم 25
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.
آية رقم 26
Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
آية رقم 27
Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
آية رقم 28
Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
آية رقم 29
Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
آية رقم 30
ﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
آية رقم 31
Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
آية رقم 32
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?
آية رقم 33
Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.
آية رقم 34
ﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!
آية رقم 35
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
ﭲ
Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
آية رقم 36
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.
آية رقم 37
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula
آية رقم 38
ﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Mpaka siku ya wakati maalumu.
آية رقم 39
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
آية رقم 40
ﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Ila waja wako walio safika.
آية رقم 41
ﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.
آية رقم 42
Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.
آية رقم 43
ﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.
آية رقم 44
Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.
آية رقم 45
ﯕﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
آية رقم 46
ﯛﯜﯝ
ﯞ
(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.
آية رقم 47
Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.
آية رقم 48
Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.
آية رقم 49
Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
آية رقم 50
ﯻﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!
آية رقم 51
ﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.
آية رقم 52
Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.
آية رقم 53
Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.
آية رقم 54
Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?
آية رقم 55
Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.
آية رقم 56
Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?
آية رقم 57
ﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?
آية رقم 58
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!
آية رقم 59
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
آية رقم 60
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.
آية رقم 61
ﮘﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,
آية رقم 62
ﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.
آية رقم 63
Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.
آية رقم 64
ﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.
آية رقم 65
Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.
آية رقم 66
Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.
آية رقم 67
ﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.
آية رقم 68
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.
آية رقم 69
ﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
آية رقم 70
ﯻﯼﯽﯾﯿ
ﰀ
Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?
آية رقم 71
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.
آية رقم 72
ﭘﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
آية رقم 73
ﭞﭟﭠ
ﭡ
Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
آية رقم 74
Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.
آية رقم 75
ﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.
آية رقم 76
ﭱﭲﭳ
ﭴ
Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.
آية رقم 77
ﭵﭶﭷﭸﭹ
ﭺ
Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
آية رقم 78
ﭻﭼﭽﭾﭿ
ﮀ
Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
آية رقم 79
ﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
آية رقم 80
ﮇﮈﮉﮊﮋ
ﮌ
Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.
آية رقم 81
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.
آية رقم 82
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
آية رقم 83
ﮚﮛﮜ
ﮝ
Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
آية رقم 84
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.
آية رقم 85
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.
آية رقم 86
ﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.
آية رقم 87
Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu.
آية رقم 88
Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
آية رقم 89
ﯵﯶﯷﯸﯹ
ﯺ
Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.
آية رقم 90
ﯻﯼﯽﯾ
ﯿ
Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,
آية رقم 91
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.
آية رقم 92
ﭖﭗﭘ
ﭙ
Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
آية رقم 93
ﭚﭛﭜ
ﭝ
Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
آية رقم 94
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.
آية رقم 95
ﭥﭦﭧ
ﭨ
Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
آية رقم 96
Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!
آية رقم 97
Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
آية رقم 98
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
آية رقم 99
ﮂﮃﮄﮅﮆ
ﮇ
Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
تقدم القراءة