ترجمة معاني سورة الحجر باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation

Ali Muhsin Al - Swahili translation

آية رقم 16

Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
آية رقم 18

Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
آية رقم 34

(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!
آية رقم 36

Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.
آية رقم 37

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula
آية رقم 43

Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.
آية رقم 46

(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.
آية رقم 62

Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.
آية رقم 64

Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.
آية رقم 72

Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
آية رقم 76

Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.
آية رقم 79

Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
آية رقم 92

Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
آية رقم 95

Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
آية رقم 98

Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
تقدم القراءة