ترجمة معاني سورة المدّثر باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮪﮫ
ﮬ
Al-Muddasir
Ewe uliye jigubika!
آية رقم 2
ﮭﮮ
ﮯ
Simama uonye!
آية رقم 3
ﮰﮱ
ﯓ
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
آية رقم 4
ﯔﯕ
ﯖ
Na nguo zako, zisafishe.
آية رقم 5
ﯗﯘ
ﯙ
Na yaliyo machafu yahame!
آية رقم 6
ﯚﯛﯜ
ﯝ
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
آية رقم 7
ﯞﯟ
ﯠ
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
آية رقم 8
ﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Basi litapo pulizwa barugumu,
آية رقم 9
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
آية رقم 10
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
آية رقم 11
ﯰﯱﯲﯳ
ﯴ
Niache peke yangu na niliye muumba;
آية رقم 12
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
آية رقم 13
ﯺﯻ
ﯼ
Na wana wanao onekana,
آية رقم 14
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
آية رقم 15
ﰁﰂﰃﰄ
ﰅ
Kisha anatumai nimzidishie!
آية رقم 16
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
ﰌ
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
آية رقم 17
ﰍﰎ
ﰏ
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
آية رقم 18
ﰐﰑﰒ
ﰓ
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
آية رقم 19
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
آية رقم 20
ﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
آية رقم 21
ﭚﭛ
ﭜ
Kisha akatazama,
آية رقم 22
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
آية رقم 23
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
آية رقم 24
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
ﭫ
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
آية رقم 25
ﭬﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
آية رقم 26
ﭲﭳ
ﭴ
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
آية رقم 27
ﭵﭶﭷﭸ
ﭹ
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
آية رقم 28
ﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Haubakishi wala hausazi.
آية رقم 29
ﭿﮀ
ﮁ
Unababua ngozi iwe nyeusi.
آية رقم 30
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Juu yake wapo kumi na tisa.
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
آية رقم 32
ﯥﯦ
ﯧ
Hasha! Naapa kwa mwezi!
آية رقم 33
ﯨﯩﯪ
ﯫ
Na kwa usiku unapo kucha!
آية رقم 34
ﯬﯭﯮ
ﯯ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
آية رقم 35
ﯰﯱﯲ
ﯳ
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
آية رقم 36
ﯴﯵ
ﯶ
Ni onyo kwa binaadamu,
آية رقم 37
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
آية رقم 38
ﯿﰀﰁﰂﰃ
ﰄ
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
آية رقم 39
ﰅﰆﰇ
ﰈ
Isipo kuwa watu wa kuliani.
آية رقم 40
ﰉﰊﰋ
ﰌ
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
آية رقم 41
ﰍﰎ
ﰏ
Khabari za wakosefu:
آية رقم 42
ﰐﰑﰒﰓ
ﰔ
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
آية رقم 43
ﰕﰖﰗﰘﰙ
ﰚ
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.
آية رقم 44
ﰛﰜﰝﰞ
ﰟ
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
آية رقم 45
ﰠﰡﰢﰣ
ﰤ
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
آية رقم 46
ﰥﰦﰧﰨ
ﰩ
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
آية رقم 47
ﰪﰫﰬ
ﰭ
Mpaka yakini ilipo tufikia.
آية رقم 48
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
آية رقم 49
ﭖﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
آية رقم 50
ﭜﭝﭞ
ﭟ
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
آية رقم 51
ﭠﭡﭢ
ﭣ
Wanao mkimbia simba!
آية رقم 52
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
آية رقم 53
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
ﭴ
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
آية رقم 54
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
آية رقم 55
ﭹﭺﭻ
ﭼ
Basi anaye taka atakumbuka.
آية رقم 56
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
تقدم القراءة