ترجمة معاني سورة القلم باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
ﰡ
آية رقم 1
ﮉﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
Al-Kalam
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
آية رقم 2
ﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
آية رقم 3
ﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
آية رقم 4
ﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Na hakika wewe una tabia tukufu.
آية رقم 5
ﮠﮡ
ﮢ
Karibu utaona, na wao wataona,
آية رقم 6
ﮣﮤ
ﮥ
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
آية رقم 7
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
آية رقم 8
ﯓﯔﯕ
ﯖ
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
آية رقم 9
ﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
آية رقم 10
ﯜﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
آية رقم 11
ﯢﯣﯤ
ﯥ
Mtapitapi, apitaye akifitini,
آية رقم 12
ﯦﯧﯨﯩ
ﯪ
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
آية رقم 13
ﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
آية رقم 14
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
آية رقم 15
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
آية رقم 16
ﯾﯿﰀ
ﰁ
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
آية رقم 17
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
آية رقم 18
ﭜﭝ
ﭞ
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
آية رقم 19
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
آية رقم 20
ﭧﭨ
ﭩ
Likawa kama usiku wa giza.
آية رقم 21
ﭪﭫ
ﭬ
Asubuhi wakaitana.
آية رقم 22
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
آية رقم 23
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
آية رقم 24
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
آية رقم 25
ﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
آية رقم 26
ﮅﮆﮇﮈﮉ
ﮊ
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
آية رقم 27
ﮋﮌﮍ
ﮎ
Bali tumenyimwa!
آية رقم 28
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
آية رقم 29
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
ﮝ
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
آية رقم 30
ﮞﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
آية رقم 31
ﮤﮥﮦﮧﮨ
ﮩ
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
آية رقم 32
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
آية رقم 33
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
آية رقم 34
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
آية رقم 35
ﯨﯩﯪ
ﯫ
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
آية رقم 36
ﯬﯭﯮﯯ
ﯰ
Mna nini? Mnahukumu vipi?
آية رقم 37
ﯱﯲﯳﯴﯵ
ﯶ
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
آية رقم 38
ﯷﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
آية رقم 39
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
آية رقم 40
ﰊﰋﰌﰍ
ﰎ
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
آية رقم 41
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
آية رقم 42
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
آية رقم 43
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
آية رقم 44
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
آية رقم 45
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
ﭰ
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
آية رقم 46
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
آية رقم 47
ﭹﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
آية رقم 48
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
آية رقم 49
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
آية رقم 50
ﮖﮗﮘﮙﮚ
ﮛ
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
آية رقم 51
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
آية رقم 52
ﮩﮪﮫﮬﮭ
ﮮ
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
تقدم القراءة